Afrika tupo bize na kuamini uchawi, bado hatustuki tu kwamba uchawi ni adui wa maendeleo?

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
uchawi upo na hutuwezi kuuepuka kwa kuamini kwamba haupo, Kama wewe ni Mkristo au Muislam lazima uamini uwepo wa uchawi lakini hupaswi kuuamini kwa matumizi.

Hapa nazungumzia uchawi sio matambiko maana matambiko mengi yana lengo positive kuondoa tatizo japo kuna baadhi ya matambiko yapo kichawi, uchawi lengo lake huwa ni moja tu, KUHARIBU MAENDELEO YA WATU (waweza tajirika lakini masharti yakakunyima uhuru).

Ni sayansi ya nguvu za giza zenye lengo la kudhuru iwe ni kutupia mtu busha, kumtupia majini, kumsumbua usiku, kumuua, n.k. ilimradi mtu akwame kwenye maendeleo.

Mambo ya uchawi yamekuwa yana nafasi kubwa sana hata kwa viongozi wa juu hapa Afrika, hapa kwetu huwa tunajionea mambo haya live kipindi cha chaguzi za wabunge ambao huja kuwa mawaziri na baadae hata maraisi, Ukienda Afrika Kusini nako viongozi wanatembea na Muthi (Hirizi) kwa lengo la kujibusti, Nigeria nako nchi inayongoza kwa maendeleo bara la Afrika kwa nchi za sub saharan nao hawapo nyuma.

Kutumia Akili uliyopewa kuna nguvu kuzidi uchawi, hilo linadhihirishwa vita ya maji maji mtaalam wa kuitwa Kinjikitile Ngwale aliwatengenezea kinga babau zetu dhidi ya risasi na kilichotokea kimebaki kuwa historia ya aibu, watu wanaamini bado kupaa na nyungo wakati ndege zilishatengenezwa kitambo, wachezaji wazuri hasa wa kigeni wanasajiliwa na timu zetu lakini wanarogwa na wenzao wanaolazimisha kupewa namba uwanjani hata kama viwango vimeshuka, n.k.

Si Africa tu, hata nchi za huko Amerika ya kusini kama Haiti imejaa Waafrika ndio inaongozea kwa umasikini ila ndio kinara wa mambo ya uchawi ukanda huo.
 
Hakuna uchawi. Story za uchawi zinatamalaki kwenye jamii za watu wajinga na maskini ndo maana kila siku unasikia wafu wamefufuka na wengine kujifungua jiwe huko mikoani kwenye watu wengi wajinga na maskini kuliko Dar let alone Ulaya na Amerika. Mtu mjinga hata akiumwa malaria anaamini kalogwa.
 
Ipitishwe amri tu kila mchawi apigwe kiberiti, maana uchawi upo na hutuwezi kuuepuka kwa kutouamini lazima wanga wataku-win

Halaf hiz habari za sijui serikali haiamin uchawi ni upuuz wa hali ya juu, kwa intelligence gan kali walionayo
Wakat wenzao ulaya huko miaka hiyo wamewatembezea sana moto wachawi

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Hakuna uchawi. Story za uchawi zinatamalaki kwenye jamii za watu wajinga na maskini ndo maana kila siku unasikia watu wamefufuka na wengine kujifungua jiwe huko mikoani kwenye watu wengi wajinga na maskini kuliko Dar. Mtu mjinga hata akiumwa malaria anaamini kalogwa.
Kama huamini uchawi upo ni dhahiri humuamini hata Mwenyezi Mungu, uchawi umeshazungumziwa kwenye Biblia na Quran
 
Inasikitisha sana na ndo chanzo cha umaskini Kuna jamaa hapa mtaaani kwetu kigamboni yeye kazi yake kuwapiga wenzie juju ili wasipate vipato vyao vya kila mwezi.
 
Inasikitisha sana na ndo chanzo cha umaskini Kuna jamaa hapa mtaaani kwetu kigamboni yeye kazi yake kuwapiga wenzie juju ili wasipate vipato vyao vya Kila mwezi
Ni vitu wasivyoamini wengi lakini amini kwamba kuna watu wanaamka asubuhi kuwahi mabasi ya mikoani kwenda kwa wataalam kuroga wenzao ili warudi nyuma kimaendeleo,
 
Back
Top Bottom