Nimepata ajali, niombeeni wana JF

Nimepata ajali, niombeeni wana JF

Pole sana. Upande uliopigwa inaonyesha kweli ulikuwa unakwepa. Hivi hamna kamera zinazoweza kusaidia kumpata mhusika? Mji ungewekewa kamera.
Hili ni wazo zuri, kuwa na camera inachukua matukio kila siku, siku ikipita salama, unafuta, ili siku inayofuata uweze kuchukua tena.
 
Pole sana,
Ufike hospital kwa vipimo zaidi,

Hiyo barabara siku ya jumatatu watu wanakua na wazimu wengi wametoka kukesha kwenye mabar hapo kalewa halafu ana drive na bado litaenda kazini,

Dah! Ningekwambia uzungukie gereji kadhaa uchunguze gari ya Alteza itakayoenda kupatiwa huduma kwa wiki hii yote.
Tushauri Serikali zifunge CCTV camera mabarabarani.

Lakini pia tusiitegemee Serikali. Watu wafunge camera kwenye vyombo vyao vya moto.

Haya amepata Alteza inayifanyiwa service. Itamsaidia nini?
 
Habari Jf

Leo mida ya saa kumi na Moja Kamili, nikiwa na Bajaj yangu kazini.. natoka mji Mwema kwenda ferry kigamboni.

Nikiwa katika low speed ukizingatia hali ya hewa nikiwa upande wangu, gafra niliona artezza White imeovertake Iko mbele yangu,,,

Aisee, nilijitahidi kukwepa lakini alikuwa speed sana, baadae kakimbia sijui hata rangi ya gari, Nina maumivu kichwani na mguuni.


Bajaj yangu Ina Bima kubwa.
Askari wamepima na kuchora
Taratibu zingine zipoje nirudi kazini... View attachment 2558751View attachment 2558752View attachment 2558754
Tafsiri ya ndoto

 
Hili ni wazo zuri, kuwa na camera inachukua matukio kila siku, siku ikipita salama, unafuta, ili siku inayofuata uweze kuchukua tena.
Inafuta yenyewe kwa kuovewrite. Wewe unachofanya ni kuangalia tukio unalolihitaji na kulitoa kwenye card ila kama kuko shwari unaacha yenyewe inaendelea kujirekodia na kujifuta
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Hata hivo wewe ni dereva mzuri maana naona umekwepesha uso kwa uso ukampa ubavu.

Pole sana na Mungu akuponye na akurahisishie michakato upatiwe nyingine soon.
Nashukuru sana.
Nimejitahidi sana.
Alhamdulilah Mungu kanitetea
 
Hata hivo wewe ni dereva mzuri maana naona umekwepesha uso kwa uso ukampa ubavu.

Pole sana na Mungu akuponye na akurahisishie michakato upatiwe nyingine soon.
Inawezekana kupewa ingine?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom