Nimeona Samaki Aina ya Papa Mnadani Lamu Mombasa

Nimeona Samaki Aina ya Papa Mnadani Lamu Mombasa

Joined
Apr 19, 2018
Posts
59
Reaction score
69
Habari ya saa hii jameni,nimeona papa wa urefu kama futa tatu na ushee akiuzwa kwa soko ya samaki.

Swali nataka uliza😛apa analiwa? Because once nilipata kusikia wako wenye sumu hawafai kwa kukula.

Just curious mazee
 
Analiwa kuanzia nyama,mapezi Hadi mifupa...Wachina papá hawabakishi kitu.....
Sana sana mapezi yake ndiyo real sana

Ova
 
Huku Pwani papa anapakwa chumvi na kuzikwa ardhini. Anakauka taratibu, akifukuliwa huliwa mwaka mzima.

Huu ustaarabu niliuona pia Botswana, wao wakichinja ng’ombe nyama hupakwa chumvi na kuachwa juani. Mwaka mzima mnaweza kula taratibu
 
Huku Pwani papa anapakwa chumvi na kizikwa ardhini. Anakauka taratibu, akifukuliwa huliwa mwaka mzima.

Huu ustaarabu niliuona pia Botswana, wao wakochinja ng’ombe nyama hupakwa chumvi na kuachwa juani. Mwaka mzima mnaweza kula taratibu
Sasa hiyo nyama ya ng'ombe si itakuwa na chumvi nyingi sana
 
Huku Pwani papa anapakwa chumvi na kizikwa ardhini. Anakauka taratibu, akifukuliwa huliwa mwaka mzima.

Huu ustaarabu niliuona pia Botswana, wao wakichinja ng’ombe nyama hupakwa chumvi na kuachwa juani. Mwaka mzima mnaweza kula taratibu
Hata Serengeti inachukiliwa nyama inapondwa inawekewa chumvi inaanikwa inakaa mwaka mzima. Tabora(kasenga}) inapakwa chumvi inabanikwa
 
Huku Pwani papa anapakwa chumvi na kizikwa ardhini. Anakauka taratibu, akifukuliwa huliwa mwaka mzima.

Huu ustaarabu niliuona pia Botswana, wao wakichinja ng’ombe nyama hupakwa chumvi na kuachwa juani. Mwaka mzima mnaweza kula taratibu
Hata nyama pori unawezaipaka chumvi na kuianika.

Kwa papa nawezakumalizia ugali wako wa kilo mbili peke yangu. Apikwe na nazi, nyanya chungu (Ngogwe) bamia na pilipili. dah hapo sijaongezea mchunga wa nazi uliokamuliwa kidogo ukabakishwa ule uchungu kwa mbali😛😛😛
 
Hata nyama pori unawezaipaka chumvi na kuianika.

Kwa papa nawezakumalizia ugali wako wa kilo mbili peke yangu. Apikwe na nazi, nyanya chungu (Ngogwe) bamia na pilipili. dah hapo sijaongezea mchunga wa nazi uliokamuliwa kidogo ukabakishwa ule uchungu kwa mbali
Haha mchunga wakati wa masika huwa ninauanika, ukikauka ninaweka kwenye vifuko vya chakula ninahifadhi kwenye freezer. Wagosi wakinitembelea wanakula ugali na mchunga the whole year round
 
Haha mchunga wakati wa masika huwa ninauanika, ukikauka ninaweka kwenye vifuko vya chakula ninahifadhi kwenye freezer. Wagosi wakinitembelea wanakula ugali na mchunga the whole year round
Uwiiiii Mkuu unaishi wapi niwe mgeni wako. Ahsante kwa kunipa maujanja............ leo ntaendauchuma niuanike maana huwa naugua kabisa nikiukumbuka. Je nawezauanika ndani tu maana sasa hivi jua ni kama kuokota shilingi mia barabarani
 
Uwiiiii Mkuu unaishi wapi niwe mgeni wako. Ahsante kwa kunipa maujanja............ leo ntaendauchuma niuanike maana huwa naugua kabisa nikiukumbuka. Je nawezauanika ndani tu maana sasa hivi jua ni kama kuokota shilingi mia barabarani
Hauharibiki jua likitoka uanike, hata na kesho pia. Uzuri hili jua la mvua linakuwaga kali sana. Jua la siku tatu linatosha.
 
  • Thanks
Reactions: Mj1
Samaki kupakwa chumvi anaitwa"ngonda"

Ova
 
Huku Pwani papa anapakwa chumvi na kuzikwa ardhini. Anakauka taratibu, akifukuliwa huliwa mwaka mzima.

Huu ustaarabu niliuona pia Botswana, wao wakichinja ng’ombe nyama hupakwa chumvi na kuachwa juani. Mwaka mzima mnaweza kula taratibu
Hiyo kwa ng'ombe inakuwa kama Kimoro zile nyama za wanyama pori...
 
Mkuu hata papa anapakwa chumvi na kukaushwa juani. Ndio maana kuna papa mbichi na papa mkavu, nenda soko la Tandika wapo kibao
Najua hilo! Mm nmefanya biashara ya uvuvi pia papa Nlikuwa nafukuzia mapezi unajua kuna papá mweusi na Mweupe yaani aina ya sumbwi na sarawanzi hao ni aina ya papa

Ova
 
Najua hilo! Mm nmefanya biashara ya uvuvi pia papa Nlikuwa nafukuzia mapezi unajua kuna papá mweusi na Mweupe yaani aina ya sumbwi na sarawanzi hao ni aina ya papa

Ova
Utaacha lini Uongo wewe Mzee!?
 
Back
Top Bottom