PostGE2025 Nimeogopa sana! Kete yao ya mwisho ni udini

PostGE2025 Nimeogopa sana! Kete yao ya mwisho ni udini

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,704
Reaction score
861,050
Nimeogopa sana! Nimeogopa kupita kiasi... Banda yote kushindikana sasa wanataka kutumia kete ya dini! Mungu atusaidie sana
Walianza na figisu za kawaida
Wakaja na siasa majitaka
Wakaanza kurubuni wapinzani
Wakaanza kubambikia kesi
Wakawa wanateka
Wakawa wanateka na kupoteza watu
Wakawa wanaua.. Na kilele cha mauaji kikawa tar 29.10. Mpaka tar 3 November 2025.

Mpaka hapo wakazani wameshafanikiwa kuuza hofu.. Lakini wali ndio kwanza kama wamechokoza nyuki

Pengine walifadhiliwa mabilioni ili wakirudi kwenye power walipe fadhila kupitia rasilimali za wote..Sasa kitisho ni dhahiri. Wanaona wazi hawana pa kuchomokea
Kulinda maslahi yao na ya wafadhili wao ni wao kubakia kwenye power.. Hii ndio salama yao
Waliokwisha onja utamu wa maliasili lukuki za taifa hawako tayari kupokonywa tonge mdomoni.. Wako tayari kufanya lolote na chochote alimradi tu waendelee kuzifaidi

Hii kete ya udini ndio kete ya mwisho na hatari kuliko nyingine zote! Wameanza kea kasi kubwa na ya ajabu kupenyeza hiyo sumu kwenye jamii kupitia wachache wasiojutambua

Tunahitaji kudra kubwa za Mwenyezi Mungu tusije kufika wanakotaka kutufikisha.... 😭😭😭🚯
 
Mshana Jr usiogope hata kidogo, usiogope vita unapopigana na Mtu asiye na akili... Hawa hawana akili.

Mgogoro wa Dini unakuwa una nguvu pale unapokuwa na msingi wa kijamii ila sio hivi wavyofanya.

Pia mgogoro wa Dini inabidi uwe ideological zaidi
Uzuri waislamu wengi wao wamewadharau. Wengi wa waliouwawa ni waislamu kuliko hata hao wakristo.
 
Wapuuzi sana wanatumia mbinu bila kuangalia madhara wanayoweza kuleta, hivi hawa kikichafuka wataweza kubeba ndugu zao wote wa ukoo wao wakaishi nao huko mbali? Akili za hawa watu hata Wanyama wana nafuu
 
Ninachoogopa dini ni imani sasa kukishakuwa na mgogoro wa dini siku zote kitu kidogo kitaonekana kikubwa kisicho na uzito kitachukuliwa kwa uzito MUNGU asimame na sisi tu atuepushe na haya yanayo endelea kwa hawa viongozi wa dini zote mbili awe muislam awe mkristo. Sisi sote ni wamoja tumekuwa wamoja Dini zisitutofautishe katika namnq tunavyoishi na kushirikiana katika jamii zetu.
 
1763594218759.jpeg
 
Uzuri hata serikali yao mbumbumbu Ina watu wa dini zote, kwa kifupi Hawa wapumbavu akili zao zimekwisha tia nanga!!, na hata ukiwasikiliza wale mashekhee njaa wapayukaji ni wazi wamekuja kwa lengo la kupandikiza hofu lakini hawana ujasiri wa kuingia barabarani kukabiliana na hasira ya umma.
Sababu Kila anaetoa mdomo wake na kubwabwaja sasahivi ni manusura wa October 29, kwa kifupi wengi ni waoga kuliko panya , walikua wamejifungia chini ya vungu za vitanda vyao wakati vijana shupavu wakichuana na mashetani kwa kuweka roho zao rehani ..
wanatoa vitisho wasivyoweza kuviishi na bahati nzuri zaidi waTanganyika wanasimamia haki bila kujali upuuzi wa dini yoyote..Damu za vijana hazitoenda bure
 
Tena wamejitanabaisha wazi hasa kipindi kile cha kampeni waliitwa kwa makundi eti kuombea amani kuelekea uchaguzi ,

Wenye akili tuliona ni kampeni kwa mgongo wa dini huwezi ita viongozi wote bila kuwapa chochote tena wa upande mmoja.

Kibaya zaidi waraka wa TEC ulipaswa kujibiwa na serikali angalia sasa wanaoujibu waraka ule ni waislamu,

Katika waraka ule hakuna mahali TEC wameitaja BAKWATA lakini angalia sasa kinachoendelea ,

Viongozi wa dini waliopaswa kusimamia haki wamegeuka machawa wao watu Kutekwa na kuuwawa hawaoni tatizo ,

Watu wamepoteza maisha kwa kumiminiwa risasi wao hawaoni tatizo,
Mwenyezi Mungu wape hekima na busara viongozi wetu huu si utamduni wetu tuepushe na dhulma zote dhidi ya haki ya kuishi amani itakuja ikiwa haki itasimama mahali pake.
 
Na wamefeli kuitumia hiyo kete, maana Waislamu wengi wameshawakataa kitambo, na hata ukiwauliza wanasema BAKWATA ni sehemu ya Serikali kupitisha agenda zao na sio Baraza la Waislamu kama wanavyojitanabaisha.

TUPO PAZURI. UKISOMA COMMENTS ZA WAISLAMU MITANDAONI NDIO KABISA WANAWAKATAA.

SASAIVI HAIJALISHI UNATOKEA UPANDE GANI, UKIENDA TOFAUTI NA AGENDA YA WANANCHI WAUMINI WANAKUKATAA.

InaumaSana/ItHasAForkVery
 
Mshana Jr tumekubaliana hatutanunua wala kukubali kuuziwa tena bidhaa inayoitwa hofu, uoga wala wasiwasi.

Next time ukiandika Uzi wako usitumie neno kuogopa tafadhali.

Moderator na wote tukubaliane ilitokea yeyote anauza na kutangaza bidhaa ya hofu au uoga kama ni platinum member aonywe akikaidi avuliwe heshima ya kuwa platinum member. Na kama ni expert member ifanyike vivyo hivyo abakie kuwa member tu.
 
Mshana Jr tumekubaliana hatutanunua wala kukubali kuuziwa tena bidhaa inayoitwa hofu, uoga wala wasiwasi.

Next time ukiandika Uzi wako usitumie neno kuogopa tafadhali.

Moderator na wote tukubaliane ilitokea yeyote anauza na kutangaza bidhaa ya hofu au uoga kama ni platinum member aonywe akikaidi avuliwe heshima ya kuwa platinum member. Na kama ni expert member ifanyike vivyo hivyo abakie kuwa member tu.

View: https://www.facebook.com/share/v/17iQmQCKJ5/
 
Ninachoogopa dini ni imani sasa kukiahakuwa na.mgogoro wa dini sikubzote kitu kidogo kitaonekana kikubwa kisicho na uzito kitachukuliwa kwa uzito MUNGU asimame na sisi tu atuepushe na haya yanagoendelea kwa hawa viongozi wa dini zote mbili awe muislam awe mkristo.
Neno USIOGOPE limeandikwa zaidi ya mara 365 katika baadhi ya vitabu vya maandiko vinavyoaminika na wengi.

Maana yake katika siku 365 au mwaka mzima hutakiwi kuogopa hata siku moja.

Tukikosa na tusipo kubali Uoga maana yake wanapoteza mamlaka yao na sisi tunakuwa na kubaki na mamlaka na nguvu yetu.

Kamwe tusikibali kubadilishana ujasiri wetu na kuchukua hofu au uoga wao. Ujasiri wetu ndio nguvu, silaha na ngao yetu.

Mpaka dakika hii ujasiri wetu kwa pamoja umezidi na kuishinda maovu na hila za watesi wetu.
 
Nimeogopa sana! Nimeogopa kupita kiasi... Banda yote kushindikana sasa wanataka kutumia kete ya dini! Mungu atusaidie sana
Walianza na figisu za kawaida
Wakaja na siasa majitaka
Wakaanza kurubuni wapinzani
Wakaanza kubambikia kesi
Wakawa wanateka
Wakawa wanateka na kupoteza watu
Wakawa wanaua.. Na kilele cha mauaji kikawa tar 29.10. Mpaka tar 3 November 2025.

Mpaka hapo wakazani wameshafanikiwa kuuza hofu.. Lakini wali ndio kwanza kama wamechokoza nyuki

Pengine walifadhiliwa mabilioni ili wakirudi kwenye power walipe fadhila kupitia rasilimali za wote..Sasa kitisho ni dhahiri. Wanaona wazi hawana pa kuchomokea
Kulinda maslahi yao na ya wafadhili wao ni wao kubakia kwenye power.. Hii ndio salama yao
Waliokwisha onja utamu wa maliasili lukuki za taifa hawako tayari kupokonywa tonge mdomoni.. Wako tayari kufanya lolote na chochote alimradi tu waendelee kuzifaidi

Hii kete ya udini ndio kete ya mwisho na hatari kuliko nyingine zote! Wameanza kea kasi kubwa na ya ajabu kupenyeza hiyo sumu kwenye jamii kupitia wachache wasiojutambua

Tunahitaji kudra kubwa za Mwenyezi Mungu tusije kufika wanakotaka kutufikisha.... 😭😭😭🚯
Lengo lilikuwa hili la kukufikisha hapa kwenye kuogopa 😁😁😁
 
Ninachoogopa dini ni imani sasa kukiahakuwa na.mgogoro wa dini sikubzote kitu kidogo kitaonekana kikubwa kisicho na uzito kitachukuliwa kwa uzito MUNGU asimame na sisi tu atuepushe na haya yanagoendelea kwa hawa viongozi wa dini zote mbili awe muislam awe mkristo.
Neno USIOGOPE limeandikwa zaidi ya mara 365 katika baadhi ya vitabu vya maandiko vinavyoaminika na wengi.

Maana yake katika siku 365 au mwaka mzima hutakiwi kuogopa hata siku moja.

Tukikosa na kurokubali Uoga maana yake wanapoteza mamlaka yao na sisi tunakuwa na kubaki na mamlaka yetu.

Kamwe tusikibali kubadilishana ujasiri wetu na kuchukua hofu au uoga wao.

Mpaka dakika hii ujasiri wetu kwa pamoja umezidi na kuishinda hof ya watesi wetu.
 
Back
Top Bottom