Nimemsikiliza Naibu Katibu wa chama cha soka Burundi, nimeumia sana kuhusu Tanzania yangu

The Phylosopher

JF-Expert Member
Mar 11, 2015
1,503
2,046
Nimemsikiliza sana naibu katibu wa chama cha soka cha Burundi kuhusu mipango yao ya maendeleo, nikajaribu kuwaza kuhusu mwelekeo wa taifa letu kimichezo, nikaona bado tuna safari ndefu sana kufikia matamanio yetu kimichezo.

Alipoulizwa na mtangazaji wa chombo kimoja cha habari hapa nchini kuhusu siri ya mafanikio iliyonayo Burundi kimichezo hasa soka, alisema.

" Hii ni matokeo ya utashi wa serikali nzima kwani baada ya kumalizika vita tukawa na hukumu la kujenga amani. Baada ya kuona tumefanikiwa kujenga amani ikiwa zamu ya kujenga maendeleo.

Swali likawa tunajengaje maendeleo katika mazingira ambayo hatuna rasilimali watu ya kutosha kama mlivyo watanzania? Ndipo tukaja na wazo la kuinua viwango vya huduma ili tuuze huduma duniani.

Chini ya mpango huu tumefanikiwa kuzalisha makocha wengi marefaree wachezaji na watendaji wengine wenye ubora unaokidhi viwango vya kimataifa".

Ni Kwa muktadha huu sio ajabu Tanzania tumejaza makocha warundi wachezaji warundi yaani ni aibu tupu. Hata hivyo nieleweke vizuri sina tatizo na warundi kuja kufanya kazi as long as wana sifa na vigezo.

Hoja yangu ni kwamba tumewawezeshaje watu wetu kuteka masoko ya ajira zinazohusu vipaji vyao Kwa mataifa ya nje?.
 
Bwana wewe makocha wao sio wa viwango ya juu ni kwamba tuu hapa bongo kuna ujinga mwingi tuu....yaani kweli wewe ukampe timu ndariagije unamuacha mecky? Sii ujinga huo.

Hao warundinwana qualifications gani ambazo zinawazidi makocha wazawa? Advantage walionayo ni kwamba wanaongea kiswahili ndio maana bongo imekuwa chaka lao but sio kweli kwamba wana quality
 
Tanzania Rais wa tff anawekwa na Prime Minister unafikiri ataingia na maono au kulinda masilahi ya waliomuweka?
 
Soka la bongo Lina pesa Mzee. Hakuna Klabu Burundi inaweza kumlipa kocha mkubwa Kama Hemed Morroco,, au kumsajili japo Aziz Amndabwile
 
Mpira wa Tanzania siasa Sana. Rais wa tff aliwahi kumshambulia hadharni mgombea flani wa chama Cha siasa. Leo Tena unasikia hela ya serikali inakwenda kukarabati viwanja vya chama, umoja utatoka wap
 
Bwana wewe makocha wao sio wa viwango ya juu ni kwamba tuu hapa bongo kuna ujinga mwingi tuu....yaani kweli wewe ukampe timu ndariagije unamuacha mecky? Sii ujinga huo.

Hao warundinwana qualifications gani ambazo zinawazidi makocha wazawa? Advantage walionayo ni kwamba wanaongea kiswahili ndio maana bongo imekuwa chaka lao but sio kweli kwamba wana quality
Je refree mbona wao wapo wengi wanaochezesha michuano ya afcon ila Tanzania hata 1 hakuna
 
Sijaona ni kwa namna gani Burundi wanatuzidi kifutiboli kwenye uzi wako mzima.
 
Michezo mingi ni sekta muhimu ya uchumi kama serikali ikiamka. Wanariadha wa Kenya na Ethiopia wanachuma hela nzuri na kuingiza kipato kizuri kwenye uchumi wao. Wakirudi nyumbani wanajenga, wanafungua biashara na kuongeza ajira. Wacheza soka wa West Afrika nao wamefanikiwa. Timu ya Ufaransa imejaa Wasenegali na mapopo wengine. Hela ngapi wanatumia ndugu zao Afrika? Sisi mfumo wa ujamaa umetudumuza. Tunashindwa kufikiria nje ya boksi.
 
Bwana wewe makocha wao sio wa viwango ya juu ni kwamba tuu hapa bongo kuna ujinga mwingi tuu....yaani kweli wewe ukampe timu ndariagije unamuacha mecky? Sii ujinga huo.

Hao warundinwana qualifications gani ambazo zinawazidi makocha wazawa? Advantage walionayo ni kwamba wanaongea kiswahili ndio maana bongo imekuwa chaka lao but sio kweli kwamba wana quality
Ndugu yangu lazima tukubali kwamba tuna tatizo mahali kama makocha wetu ni wakubwa ni Kwa nini hawafundishi nje ya Tanzania? Na ikiwa viwango vya warundi ni vya kawaida mbona wamejaa kwenye vilabu vyetu?
 
Ndugu yangu lazima tukubali kwamba tuna tatizo mahali kama makocha wetu ni wakubwa ni Kwa nini hawafundishi nje ya Tanzania? Na ikiwa viwango vya warundi ni vya kawaida mbona wamejaa kwenye vilabu vyetu?
Kaka tatizo lipo. Ili uende nje ya nchi kaka ni lazima watu wakuone...watakuona kama una perform kwenye timu kubwa nchini kwenu. Hapa nchini kwetu top teams zinazo cheza internagional competitions ni hizo simba yanga azam ambao wao hawataki kuajiri local coaches.

Yanga waliona mecky anfanya vizuri kule kagera wakamtaka but suo kama head coach eti awe assistant huoni kuwa hao viongozi ni majanga?

Mosimane kabla ya kwenda al ahly, i managed sundows for no less than 4 seasons. Mmiliki alimuamini na akamwezesha kwa kumsomesha na kumlipa vile anavyostahili na ndio maana jamaa aka perform mpaka waarabu wakamtaka.

Hawa warundi wanaokuja hapa kweli wote walifanya maajabu kwenye caf competitions mpaka tuseme yes huyu kwwli ni quality material tumlete kwetu au ni kwamba tuu tunaleta mambo ya ten percent?
 
Back
Top Bottom