Nimemfumania mke wangu na baba mkwe, nifanyaje?

Nimemfumania mke wangu na baba mkwe, nifanyaje?

Usiogope hayo mbona ya kawaida tu. Wazee siku hizi si wazee bali vijamaa tu. Huyo hajaanza leo, kaanza siku nyingi tu mbona. Weye ni mtoto wa kiume wa ngapi? Kama una kaka zako nao wameoa basi jua kuwa nao wamefanyiwa hayo hayo ka weye.
Pili; kama bado unakaa na wazazi wako, hiyo umejitakia mwenyewe haswa kama huyo mzee ndiye mlishi wa familia. Anaona umemletea mzigo hivyo jasho lake lisiliwe bure.
Kuna mengi sana uliyo pungua weye kwa mkeo. Haswa kifedha, mkeo akaona hiyo bank iliyo karibu aitumie.
 
Kama wewe ni wa kwetu kaskazini samehe tuuu maana hiyo ni kawaida sana....
 
haya maisha tu, ilivyotokea ndio ilivyoandikwa, isingeweza kuzuilika, hakuna cha shetani hapo, hao ndio mchezo wao, na uyo baba ako na chanzo, na pili wee jitathimini upya kuanzia mfumo wako wa maisha, kama unaweza kuendelea na uyo mwanamke, au wapi ulikua unakosea sana, kilichotokea ni unyama wa kutisha sana.
 
Pole mkuu kwa hayo yote yaani sio peke yako uliyejeruhuka ni wewe na pamoja na mama yako pia naye kajeruhika kwa kisa hichi jipe moyo ongea na mkeo vizru ikiwezekana achana nae kwani ameshachafua ukoo huyo na huyo baba yako achana naye wala usimsemeshe jiondokee anza maisha mapya kifavyo mungu atakupa upenyo mwingine
 
ungekua umemfamania kweli ungekua na guts za kuandika Uzi hapa?
 
Usituzuge hapa wewe.. Umehadithiwa hii.. Ushauri gani unataka zaidi ya kuacha kuingiza alipoingiza babako?
Kwa hiyo umetulia mpaka jf ikupe maneno?
 
Mkuu tumia tolati kumaliza hiyo kadhia.
Yawezekana kabisa mdingi pengine yeye ndo alianza kumung'unya kabla yako!!!??? nawaza tu lakini....
 
Kama ni kweli Pole sana,
Ushauri wangu kwako Hapo ulipoingia siko,Jipange uchape lapa maisha yatasonga tuu...
 
Hapo mimi sijaelewa, baba mkwe wa mke wako au baba mkwe wako?
Kama ni baba mkwe wako ina maana umemfumania mke wako na baba yake?
Kama ni baba mkwe wa mkeo ina maana umemfumania mkeo na baba yako?

Naomba maelezo tafadhali!
 
Back
Top Bottom