Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 876
Nina amini sana kuwa huyu akipima atakutwa yupo vizuri sana.Pole kwa yaliyokukuta. Hapo kua mkeo alizaliwa nao na alikua hajui kuna mashaka, ukipima virusi vya ukimwi unapata majibu kama vipo au havipo, kua viliingia kwa njia gani huwezi kujua kwa kutumia vipimo labda kwa kutumia historia ya mwathirika unaweza kukisia.
Ushauri: ni kweli ukimwi unatisha lakini ni ugonjwa kama magonjwa mengine, kwa teknologia ya madawa ilipofikia unaweza ishi miaka mingi sana hadi uzee wako ukiwa na maambukizi ya virusi hivyo, na ndani ya hiyo miaka teknologia inaendelae kukua kwahiyo kuna uwezekano mkubwa ikapatikana tiba kabisa au dawa itayovifanya visiwe na madhara mwilini mwako. Hivyo usivunjike moyo na kudhani ndio mwisho wa maisha.
Kama ukikutwa hauna maambukizi (ni kitu kinacho wezekana) mtaalamu atakushauli jinsi ya kuishi na mkeo bila yeye kukuambukiza na mta mlea mtoto wenu salama kabisa na utaendela ku enjoy ndoa yako.
Wish you luck!!
Sent using Jamii Forums mobile app