Nimekutana na kitu cha ajabu sana

Nimekutana na kitu cha ajabu sana

Kama miaka ya 60 ulikuwa unamuita Mzee au kumwona Mzee mpaka mwaka huu ni zaidi ya miaka 60.

Sasa sijajua ulimkuta namkongojo au vipi.

Weka mambo yako sawa hasa kama utumii vilevi
 
nje ya maada.. kwanza heshima yako mkuu kama miaka ya sitini katikati ulikuwa unajitambua kiasi leo umkumbuke huyo mzee,. na bado tupo pamoja jukwaani.ninahofu utakuwa ni uzee tu mkuu hakuna lolote la ajabu .
 
Miaka ya sitini katikati kulikuwa na mzee mmoja anauza genge pahala,

alikuwa ni maarufu sana,

Hivi majuzi nimekutana nae na cha jabu alikuwa amevaa shati lile lile maarufu, nikadhani labda ninaota...nikamuita fulani?? akaitika naam....nikamuuliza siku hizi upo wapi, akanijuza yu sehemu inaitwa NOMBO, Wakati natafakari Nombo ni wapi, akawa kama anazungumza na mtu mwingine na wakati huo huo kuna meseji ilikuwa inaingia simuni mwangu, baada ya kumaliza kusoma ile meseji sikumuona tena yule mzee,

Hebu wataalam wa mambo tusaidieni kudadavua hii,

AU NI.

deja Vu?
Sijui kwa kitaalamu ndo wanaita time travel. Otherwise fatilia afya yako ya akili .
 
Shikamoo.

Jambo la kwanza ulikuwa unamahusiano gani na huyo Mzee.

Jambo la pili..Huyo aliekuwa anazungumza na huyo mzee naye alifutika.?
 
Kuvaa nguo ile ile ulomuona nayo miaka ya 80 ni jambo la kawaida.

Kuna watu wanavaa nguo flani kama utambulisho wao.

Ushamuona Rais Museveni,
kila siku shati jeupe long sleeve oversize, na cowboy pama!

Wadhani analo moja?
Maajabu ya ujumbe: jaribu kuwaong'oneza watu kumi ujumbe ule ule, halafu umtake kila mtu aseme kwa sauti amesikia nini? Utastaajabu tofauti baina yao! Sikujua kumbe katika kuandika pia! Huyu bwana anazungumzia mwaka wa 60 wewe unamnukuu mwaka wa 80!
 
Maajabu ya ujumbe: jaribu kuwaong'oneza watu kumi ujumbe ule ule, halafu umtake kila mtu aseme kwa sauti amesikia nini? Utastaajabu tofauti baina yao! Sikujua kumbe katika kuandika pia! Huyu bwana anazungumzia mwaka wa 60 wewe unamnukuu mwaka wa 80!
Me nimetoa mfano tu.
Ndiyo kama ulivyosema, uelewa binadamu tumetofautiana, upo sahihi mkuu.
 
Chai ya suturungi, inatumalizia bando tu. Nyanoko bhebhe.
 
Back
Top Bottom