Nimekata tamaa ya kuendelea kuishi

Nimekata tamaa ya kuendelea kuishi

Ndugu yangu kwa kifupi tu Ni kwamba watu wengi hawawezi kufunguka ila kiukweli wengi wanatamani wajifie tu, maana sio kwa shida hizi za dunia!!!

Km kweli Yesu nae atarudi bora angerudi Ili tujue moja kuliko kutuweka roho juu juu tu,

Mbaya zaid kuna wengine duniani wanapigika na bado Mbinguni au peponi hawaingii,Ndo ujue kwamba mwanadam anakabiliw na shida kila kona
Duniani unaishi kwa tabu afu na mbingu unaikosa yani shida juu ya shida
 
TX MOSHI WILLIAM anasema, "Wanaume tumeumbwa mateso, mateso kuhangaika."

Kadri kiza kinavyozidi ndivyo na alfajiri inavyokaribia.

Pambana JEMEDARI usikate tamaa, Ugumu unapitiwa na kila anayeitwa MWANAUME.

Watu wa ZIWA MAGHARIBI wanasema, "Huwakuta wanaume" yaani, "Bishaanga Abashaija".
 
Hata nashindwa nianzie wapi! kila nachojaribu naishia kuharibu,madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.
Pole sana mkuu. Mungu yupo.
 
Hata nashindwa nianzie wapi! kila nachojaribu naishia kuharibu,madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.
Dogo unafikri kila mtu angekuwa anaelewa shida zake hapa jukwaani wewe si cha mtoto? Pambana kiongozi usikate tamaa kirahisi hivyo! Wanaume tumeumbwa mateso!
 
Hata nashindwa nianzie wapi! kila nachojaribu naishia kuharibu,madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.
Pambana kufa utakufa tu ikifika mda
 
Waonee huruma watoto ukiondoka nani atawahudumia vipindi vigumu tunapitia lkn inatakiwa kuvumilia
 
Pole sana ndugu. Maisha ndivyo yalivyo. Kuna kupanda na kushuka. Vumilia na mwombe Mungu. Muda wako wa kupanda utafika siku moja. Tafadhali usifikirie kufa. Kujiua ni dhambi kwa Mungu. Mungu akubariki na kukutia nguvu.
Hata nashindwa nianzie wapi! Kila nachojaribu naishia kuharibu, madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.
 
Hata nashindwa nianzie wapi! Kila nachojaribu naishia kuharibu, madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.
Kama kuwa na Matatizo ya Kimaisha na Dhiki za Kimaisha ndiyo Kigezo cha Kukata Tamaa ya Maisha basi wengine hivi sasa tungeshajiua Kitambo tu na sasa kuwa Mavumbi kama si Mbolea za Mazao Shambani ila bado tunakomaa tu tukiamini kuwa kwa Mwenyezi Mungu hakuna Kuwahi wala Kuchelewa.
 
Kwanza nampa pole kwa hayo yanayomsibu mwenzetu. Lakini nawaomba kuacha mzaha wakati mtu anapokuwa muwazi na kueleza matatizo yake. Tumpe moyo na kumfariji ili apate nafuu moyoni mwake. Kuna wakati mwenzetu mmoja alileta ujumbe kama huo. Matokeo yake alibezwa na kupewa majibu kama hayo unayoyaona toka kwa wachangiaji hapo juu. Haukupita muda mrefu tukapata taarifa kwamba mwenzetu hatunaye tena. Hapo watu wakaanza kujilaumu kwa nini hawakutoa ushauri nasaha kuhusu tatizo lake. Mwenzetu anahitaji counselling/ ushauri nasaha na si wa kumbeza.
 

Mkuu msikilize huyo Mzee hapo naamini utaelewa Jambo ni marufuku kukata tamaa watu wanapitia magumu kuliko yako
 
Muda bado upo wa kutosha unaweza badilisha kila unayohis hayabadilishiki muda bado upo mkuu
 
Shukuru Mungu ,bado unanguvu na akili ya kupambana ,hivyo usiogope ni kwa kitambo tu . Alaf we ni baba unaweza kuwa "saidia fundi" kwa muda wakati unatuliza akili ili upate njia nyingine ya kuingiza kipato.
Ukifa utaumiza mke na wanao maana bado hujawataftia solution ya kuweza kulipa hayo madeni.

Pambana boss wangu kukata tamaa iwe mwiko
 
Ushauri wenu unanipa nguvu sana ndugu zangu.Angalau sasa nimepata faraja.ila ningepata kodi ya nyumba tu,ningeicha familia nikapige vibarua mashambani,hivyo kwa mwenye uwezo wa kunisaidia 120000 nitashukuru mno.
 
Mkuu plan A ikigoma remember Kuna herufi 25 nyingine mkuu.Hata Mimi Hali hio ilinikuta yaani graduate una mtoto alafu unaamka asubuhi unakuta sms mtoto hela ya Pampers, sabuni yaani acha tu pia hata kwa kuamka asubuhi kwenda Sina.

Ila Mungu si Athumani Kuna mahali nimepata japo haikuwa rahisi mkuu.
Ushauri wangu Usichague kazi pia marufuku kukata tamaa pia kukata tamaa ni dhambi kubwa mno.
Wazungu wanamsemo wao "It may rain today and tomorrow but day after tomorrow it will be sunshine"..Usikate tamaa jomba shida Kama Moto zinaunguza unaungua.
 
Kuna mdau kasema umpe namba akutumie 500k, ama alikuwa anatania.
Ushauri wenu unanipa nguvu sana ndugu zangu.Angalau sasa nimepata faraja.ila ningepata kodi ya nyumba tu,ningeicha familia nikapige vibarua mashambani,hivyo kwa mwenye uwezo wa kunisaidia 120000 nitashukuru mno.
 
Hata nashindwa nianzie wapi! Kila nachojaribu naishia kuharibu, madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.
Usifike huko ndugu!!

Mimi nilitamani kufa mwaka fulani kutokana na mlundikano wa stress usiokoma tangu nikiwa mdogo.

Nilifikia hatua ya kutoboa tundu kwenye dari kwa lengo la kufunga kamba ikiwa ni hatua ya kujiandaa kujitundika lakini baada ya kutafakari kwa kina na kugundua kwamba hakuna asiepitia changamoto duniani niliona ningemkosea Mungu kukatisha uhai wangu, nilijipa moyo na kuendeleza mapambano.

Huwezi amini kutoka kukata tamaa na kuwa tumaini hata kwa waliokata tamaa;- leo hii nina elimu, nina kazi, mke, watoto wawili na nimesaidia ndugu zangu wengi kufikia malengo yao.

Kinachonisumbua akilini ni pale tu ambapo huwa nikipita mtaa niliokataka kutekelezea tukio la kujiondoa uhai nikiiona ile nyumba huwa nakumbuka mbali sana.

Hata wewe unayo nafasi ya kuendelea kuishi na kufanya makubwa zaidi, usijiue Mungu bado ana jambo na wewe. Ipo siku utashuhudia humu.
 
Back
Top Bottom