Nimekata tamaa ya kuendelea kuishi

Nimekata tamaa ya kuendelea kuishi

Hata nashindwa nianzie wapi! kila nachojaribu naishia kuharibu,madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.0693074779 Nipo lwamgasa geita
We fala, hakikisha unakufa wakati watoto wako wameolewa na wana watoto.
Kumbuka ukifa huyo mrembo ataliwa na wengine...komaaa baba, hizo sio shida wala vikwazo ni changamoto ndogo sana.
Ikiwa vipi niletee mwanao mmoja nimlee mimi sitajali lakini awe wa kike;
1. Mtoto wa kike akiwa yatima huteswa sana
Na dunia
2. Sipendi kuona matatizo yanakuwa sababu
ya mtoto wa kike kuteseka.

Bro una nafasi ya kufanya vyema, piga kifua sema "Nitashinda"
 
Hata nashindwa nianzie wapi! kila nachojaribu naishia kuharibu,madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.0693074779 Nipo lwamgasa geita

Sasa kama wachina wamenunua si mkiachishwa mnapewa fungu? NSSF/PPF walikuwa hawapeleki? Hizo fedha za nssf/ppf ndio za kuanzia maisha(Biashara).
 
Hata nashindwa nianzie wapi! kila nachojaribu naishia kuharibu,madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.0693074779 Nipo lwamgasa geita
Katika karne 21 unaambiwa adui mkubwa kwako ni wewe mwennyewe
kwasababu unauwezekano mkubwa wa kujiua kuliko kuuliwa na mtu mwingine
Watu wanao jiua ni wengi kuliko wanaofia vitani.
 
 
Shida zooote nadhani zilianzia hapa.[emoji116]



Mshana Jr hebu tia neno hapa.
 
Hata nashindwa nianzie wapi! kila nachojaribu naishia kuharibu,madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.
Unadhani ukifa hali itakuwaje Kwa watoto wako?

Wewe siyo wa kwanza kuwa na madeni mkuu...
Pambana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu kwa kifupi tu Ni kwamba watu wengi hawawezi kufunguka ila kiukweli wengi wanatamani wajifie tu, maana sio kwa shida hizi za dunia!!!

Km kweli Yesu nae atarudi bora angerudi Ili tujue moja kuliko kutuweka roho juu juu tu,

Mbaya zaid kuna wengine duniani wanapigika na bado Mbinguni au peponi hawaingii,Ndo ujue kwamba mwanadam anakabiliw na shida kila kona
Umesema vema Mkuu,Hata enzi za Mtume Paulo Wakristo wa kipindi kile walikuwa wamekataa tamaa wanangojea tu Yesu aje kwa mara ya pili awachukue, Ndipo tunaona Mtume Paulo anawaandikia Barua Wakristo wa Thesolanike ili kuwatia Moyo na kwamba waendelee kuchapa kazi.
 
Pole mkuu ila nakushauri usiwaze hicho unachokiwaza,Kusema "nataka nife" ni jambo moja na "kukikabili kifo" ni habari nyingine kabisa...Acha na habari ya kifo mzee,huko sio kuzuri sana kama umeondoka duniani vibaya.
Unachotakiwa ukifanye jaribu sana kuomba Mungu akuondoshee hyo mitihani lakini pia huenda kwa mitihani hyo unayopitia Mungu anataka akufungulie neema,Hicho unachopitia ni kipindi cha mpito tu na kiza kinene na hapo kunakaribia kucha,Vumilia na pia tambua kuna mwenzio ana ana magumu kuliko yako.
Kuwashirikisha watu kwenye shida zako ndyo nafuu kwako usikae na majambo kifuani always huwa yanatafuta upenyo yalipuke...kuwa na roho ya kiume bro shida anazo kila mtu.
Kikubwa kinachokutesa wewe ni madeni,madeni kila mtu anadaiwa mkuu sema hutakiwi kuyakimbia unatakiwa wanaokudai uwe nao karibu ukiwakmbia na wewe presha ndo inazidi,kuwa nao karibu waambie ukweli kuhusu hali yako usiwafiche na waahidi utawalipa,huku ukiendelea kuomba Mungu sana.....Nakupa siku 10 utashangaa kila balaa limeyeyuka kwa njia ambayo hata wewe utashindwa kuhadithia......Yalinikuta mimi mkuu ndomana nakwambia hivyo.
Usiwaze kujiua huko ndo kubaya zaidi mkuu.
Barikiwa Sana Mkuu, ushauri huu asiupuuze.Sina cha kuongeza wala kupunguza.
 
Hata nashindwa nianzie wapi! kila nachojaribu naishia kuharibu,madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.
Msalimie JPM kama utaamua kwenda.......ila ukijiua utakua umeongeza tatizo mara mbili kwanza kumzika kabwela ni gharama michango lazima iwe mingi mingi, ama sivyo manispaa ilivalie njuga(imagine unazaliwa bila heshima na unazikwa bila heshima vile vile) pili familia ya kabwela itateseka mara mbili zaidi kwanza bila baba hivyo japo ni baba asiye na mbele wa nyuma lakini uwepo wake tu unatosha kufanya watu watabasamu na kupata nguvu ya kujituma, pili familia ya kabwela kama ukijiua itabaki bila chochote toka kwa baba mwendazake.

Kama unataka kujiua angalau basi iache familia ina pakujishikiza afu we ndo ujiwahishe usipokua na makazi.
 
Hata nashindwa nianzie wapi! kila nachojaribu naishia kuharibu,madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.
Hakuna binadamu hana shida, ila zinatofautiana tuu, hivyo hauko peke yako.Mwombe mungu afungue njia, huyu mungu ana miujiza yake.
 
mwenye shamba Kuna kipindi nilikuwa hovyo Sana Yan pakushika hamna mke hayupo watoto hawapo nikakomaa nikaenda kuwachukua kibishi, nikaanza kuishi nao kigheto gheto Kuna muda hata shilingi Mia mbili Ni tapu kuipata kwa wiki nikasema Sasa "HATA NIKIJIUA KAMA WAMESHINDWA KUNISAIDIA NIKIWA NAPUMUA JE NIKIJIUA HYO HELA YA JENEZA ITAPATIKANA AU NDO NTAZIKWA KAMA MBWA" je Hawa ninaowaacha Kama nipo hai wanapata msoto hvyo je nikiondoka sindio itakuwa too much.

Adui wa maisha yako Ni wewe mwenyewe pengine dunia inakusubiri ubadilike ili uende nayo sawa kweli nilibadilika kwa maana ya Imani nikakutana na watu wapya nikapata msaada muhimu na sasa maisha yanaenda nashukuru MUNGU Sana.
 
wewe hujakata tamaa ya kuishi ndio maana umekuja huku... unachohitaji wewe kutiwa moyo na kupewa matumaini tu, kitu ambacho ni rahisi sana kukipata katka nyumba za ibadaa... nenda huko
 
Mkuu una utani!! Kumbe una Hadi watoto na kazi pia halafu ujiue.......
Acha mzaha Tuliza akili usiwe na pupa watoto tu ni faraja tosha ndiyo maana ombaomba naye hakosi watoto.
 
Hata nashindwa nianzie wapi! kila nachojaribu naishia kuharibu,madeni kila kona. Linaisha hili linaibuka hili,huku watoto wagonjwa, kule mwenye nyumba hataki maelezo anadai pesa yake. Sehemu yangu ya kazi nayo wameuziwa wawekezaji wa kichina. Kwa kifupi sana nahitaji kufa.
Mkuu unachopitia ni somo muhimu katika maisha. Kaza buti kuna neema inakuja bahati ni pale fursa inapompata mtu aliyejiandaa vyema. Jizatiti kaka ili fursa yoyote itakayokuja uitendee haki. Bora upitie hali hii sasa,hivi imagine kama hii hali ungeipitia uzeeni ingekuwaje ? Utakuwa na nguvu ya kutafuta au kutokata tamaa ? Kaka kumbuka wewe ni mzima na u buheri wa afya na bado ni kijana na una nguvu mshukuru Mungu,jikaze kuna neema inakuja fungua akili na macho uione. Unapojaza mawazo hasi unaifunga akili, unaweza ukaiacha fursa au neema ikupite mchana kweupe.
 
Back
Top Bottom