Mnaonunua simu kariakoo, makumbusho mnaambiwa mpya wengi mnapigwa.
Sio kwamba ni feki bali zinajulikana kama refurbs.
Yaani simu original zilizokua na matatizo mbalimbali zikatengenezwa kwa kubadilishwa parts zenye shida.
Refurbs hazina ubaya ila tatizo ni kwamba refurbs zote au asilimia 99 zinatoka china.
Mchina anakusanya simu zilizoharibika ana repair na parts za hovyo, kuanzia vioo, camera, battery, na component nyinginezo lengo ni kutumia gharama ndogo kadri awezavyo kisha zinakuwa packed kwenye mabox yake pamoja na chargers, earphone manual, full sealed ukiikuta kariakoo unaambiwa mpya.
Ukitaka samsung, mpya isiyo na longolongo nenda kwa samsung stores au authorised dealers wale wanazo brand new, ila tu bei zimesimamia ukucha inabidi uvumilie kwenye bei.
Chukua hii.