Nimechoka kusubiri ajira za walimu

Nimechoka kusubiri ajira za walimu

Nimekata tamaa kabisa ubinafsi unawasumbua viongozi ndio maana hata leo bado wanatuambia tuvute subira hawajui wanatuumiza kwa kutotuambia ukweli
 
Nimekuwa kufarijiwa kwa muda mrefu kuwa nivumilie ajira za walimu zitatoka mapema. Ila sasa mpaka nimekata tamaa maana wanasiasa ni kawaida yao maneno mengi mwaka unaisha tunaingia mwaka mwingine mambo hayaelewiki.

Mtaani kunachosha yaani daah hata sijui
Pole sana
Ngoja Ngoja kidogo
Mpaka kesho tuone itakuaje.
 
usimuamini muongo hata kama akiwa anasema ukweli. Mwanasiasa ni muongo sana sio wa kumuamini. Muonee huruma mtu anayejiingiza kwenye siasa maana ndio mwanzo wa yeye kutengwa na jamii yake kwa kukosa uaminifu! Lakini wanasiasa hao hao mbona wengine waliweza? walifanyaje? kwa nini……… dah! inauma!
 
sitaki kuamini kama ukweli hawaujui kuwa ajira zinatoka lini. Kwanini wasiwe wawazi tu na kuitanabaisha jamii kuwa ajira zitatoka siku fulani! Jamani maisha magumu sana kwa kweli. Halikuwa kosa letu kusoma ualimu kwa kuwa tumeitikia wito. Kwa nini tunateseka hivi? Kila siku afadhali ya jana! wazazi na ndugu wanapoteza imani na sisi kuwa labda mambo hayakuwa vizuri chuo. Wengine wameshaanza kuweka vizingiti kabisa. Jamani ishi maisha yote lakin maisha ya kumtegemea ndugu ni magumu sana. Famili zetu za kiafrika zinajulikana. Ukikosa hela mambo hayaendi.
Rais wetu tafadhali baba kuwa na huruma tuajiri baba. Imetosha tumenyooka. Hakutakuwa na uhewa hewa wowote baba. Tunakuomba. Nasema kwa uchungu mchana maana hapa nilipo sina hata uhakika wa kula mchana huu nikaona bora tu nitoe maombi haya.
 
Hivi Mmeisha Jua Radha Ya Tango, Mkijua Ndo Mtaajiriwa Naona Mnafanya Uzembe Tu.
 
We mwalimu una uhakika wa kuajiriwa halafu unatupigia kelele humu, nimekasirishwa sana na hii tabia yako ya kulia bila sababu za msingi. By the way nikueleze wazi kuwa ni mwaka Wangu wa NNE tangu nimalize shahada ya WILDLIFE MANAGEMENT hata masikitiko sina.

don't bother!

Hahahah naona umempa jibu la kishujaa kabisa mkuu
 
Maajabu ni pale Serikali inapotamba kuondoa watumishi hewa zaidi ya 16,000 ili kuokoa matumizi na kusimamisha ajira mpya lakini malipo ya mishahara badala ya kupungua yameaongezeka kwa bilioni 50 kutoka bilioni 520 kwa mwezi September 2015 + watumishi hewa na kuibiwa. mpaka Kuwa bilioni 570 june 2016 kwa mwezi Bila watumishi hewa na wezi wote wamefukuzwa na waliokuwa wanaishi kama Malaika Sasa wanaishi kama mashetani.
Maajabu ya namna hii yanapatikana Tanzania tu.

Chanzo

Soma hapa angalia mishahara ya June 2016 http://www.bot.go.tz/Publications/MonthlyEconomicReviews/MER JULY 2016.pdf

Soma na hapa angalia mishahara ya Sept 2015 http://www.bot.go.tz/Publications/MonthlyEconomicReviews/MER SEP 2015.pdf

Zitto Kabwe
 
Kwasasa tunasubiri ajira baada ya uhakiki hewa wa watumishi hewa kukamilika. Oneni taarifa ya zitto hapo juu
 
Vumilia serikali imeanza kuajiri. Vumilia. RITA wametoa tangazo la ajira.
 
Dah! mapema mwaka huu? Hiv mhJafo anafaham maana ya mapema? Afu watu wengine wanapenda sifa eti mlitumia vibaya boom, hivi unajua watu wote wanapata asalimia mia? Je, unajua kuwa kuja kupata boom unakuwa una madeni lukuki, na baada ya boom la kwanza kwa linalofuatia hucheleweshwa sana hadi mipango ya bajeti kuvurugika? Unaposema mtu ajiajiri, mwalimu atajiajiri wapi? Serikali iache ukiritimba huu, mtu anakaa mtaani mwaka mzima ili hali kuna upungufu mkubwa wa walimu nchini pamoja na mrundikano wa wanafubnzi hasa baada ya elimu bure, visingizio vya hakuna pesa siyo vya msingi, serikali inakusanya mapato yake hadi kuvuka malengo kwa sasa, na ikumbukwa ajira za walimu mwaka huu ni kwa bajeti inayoisha muda wake yaani 2015/16 na si 2016/17 kama baadhi yetu tunavyopotosha. Hivi unahangaika na madawati wanafunzi wakakae tu darasani bila walimu? Mtu anayeleta dhihaka na kejeli asidhan anamkomoa mtoa mada bali halitakii mema taifa, mwalimu ndo anamuandaa mtaalam wa kufanya kazi viwandani hapo baadae, leo unategemea matokeo mazuri ili hali mwalimu 1 anafundisha wanafunzi 200 na kuendelea tofauti na idadi halisi ya wanafunzi 45, serikali inadai nchi haina walimu wa sayansi, leo unawakalisha mwaka mzima utadhani hjamna uhitaji. Where are we going as a nation?
 
Na mkurugenzi wa jiji la dsm, leo ametangaza nafasi ya kazi katika nafasi ya mwenyekiti wa bodi ya ajira ya jiji. Mwisho wa kutuma maombi ni 30 september 2016
 
Back
Top Bottom