Nimechoka kusubiri ajira za walimu

Nimechoka kusubiri ajira za walimu

Ee mtukufu raisi toa ajira vijana
wanateseka sana nipo huku kaliua
tabora hali ni mbaya vijana walio hitimu vyuo mbali mbali
wamekata tamaa na hawana imani tena na serikali achia ajira watakao pata wapate
na watakao kosa wakose.
Magu anataka hadi aitwe mungu siyo mtukufu......ila ipo siku nayeye atarudi uraiani tu....
 
Najilaumu kwa nini nilisoma kidato cha tano na sita pamoja na Elimu ya degree kwa sababu kwa alama nilizopata ningesomea ualimu wa msingi ningeajiriwa mwaka 2013 na ningechukua uuguzi ningeajiriwa tayari kwa utawala wa Mh .J.M.K .haya sasa nimateso ambayo sijawai yapitia .SIJAONA UMUHIMU WA WAKILISHI BUNGENI WAHOJI NI LINI AJIRA ZITATOLEWA.unayetuambia tujiajiri huku umeajiriwa na serikali au kampuni ni mnafiki.DENI la HESLB linaanza mwezi wa 12 .full stress hadi kichwa kinauma
Uko kama mimi nililazmishwa niendelee leo wenzangu walioishia four ni maafisa elimu
 
Wadogo zangu poleni sana kiukweli inauma mno maana kila MTU anasema lake mi naamin watazitowa hz ajira ingawaje mvumiliv muda mwengine hula mbovu..ishu za msingi km hiz naon hazichukuliwi serious
 
kilio cha ajira na maamuzi ya 25.10.2015 yananifanya niwachukie wote walio tia tiki kwa huyu mheshimiwa
Daaah mimi mmoja wao kwa vile nilijua yeye pia alikuwa Mwalimu angetusaidia ila sekta yetu ndo anasema inawatumishi hewa askari anapiga nao [HASHTAG]#selfie[/HASHTAG] na wakati ndo wanaongoza kwa vyeti feki...am sorry br...blame on me
 
Mtu anasema nijiajiri kwenye kilimo wakati sikusomea kilimo ikiwa mawazo yenyewe ndio hivi hakuna sababu ya watu kwenda chuo kikuu waishie kidato cha 4
 
Hiyo next week ndio mwezi wa tisa unaisha sasa kama hazitoki week hii mateso ya mtaani yatazidi kutuandama.Najuta kuharibu mali za wazazi kwa kusoma sana nimeuzidisha umasikini kisa shule na ajira hazisomeki. Mh John uliposimamia unazidi kututesa au unataka tuumwe B.P kwa stress za ajira
 
Ata mi huwa nashangaa mtu anasema ukalime angali hata formular za kilimo mashuleni
hujasoma mi naona bora serikali
waazishe masomo ya ujasiliamali
mashuleni ili watu wakitoka
vyuo wae na uwezo wa kujiajiri pindi ajira zinapo kosekana.
 
Nimekuwa kufarijiwa kwa muda mrefu kuwa nivumilie ajira za walimu zitatoka mapema. Ila sasa mpaka nimekata tamaa maana wanasiasa ni kawaida yao maneno mengi mwaka unaisha tunaingia mwaka mwingine mambo hayaelewiki.

Mtaani kunachosha yaani daah hata sijui
kiukweli serikali inakataisha tamaa sana, yan wanakera sana, maneno tu vitendo hamna
 
Kwani ajira ni ualimu tu? Kumbuka kuchoma mkaa ni ajira,kufuga kuku ni ajira,na pia kuchuma mchicha ni ajira.
 
Kwa kweli kama ni kuchoka, acha nifunguke ya moyoni.. Nimechoka kuteswa kisaikolojia kwa ajira za "kusadikika".. Nashindwa hata kufikiri kazi za kufanya kwa kuhofia unaweza kufanya mipango leo na kesho ajira zikatoka.

Hawaeleweki hawa watawala wa Tz..
 
Back
Top Bottom