Blackmamba
Member
- May 26, 2009
- 12
- 0
You know mpaka mtu ana fight kukutoa Africa ng'ambo ujue pana kipengele hapo, ukizingatia nchi hizo zinavyobana kuachia njia kwa urahisi kwa mweusi kupita. Sasa ninarudi kwenye hoja kwamba, huyo jamaa anampenda mke wake ndo maana alidiriki kumchukua mpaka kiwanja badala ya kuwaachia wavimba macho na wakaanga sumu mkewe. Hata hivyo weka wazi pande zote mbili za shilingi kuujua undani naona kama kuna jambo jingine limejificha hapa kwani sababu ya lugha si ya kumfanya mume aseme maneno haya kwa mke, kwani hata kimada (concubine) huwezi mwambia maneno machafu na ya kejeli kiasi hicho, ...kinorway ndo nini? Hajui kama kuna Air-Craft Engineers wa Kirusi, Professors wa Kichina na hata Marais wasiojua Lugha nyingine zaidi ya lugha zao? Kama ameshindwa kumlisha mke na kumlazimisha kutafuta vibarua ambavyo mpaka asome kwanza, ni vyema aseme kwamba 'JAMANI SHAMBA LIMENISHINDA, ILI WATU WA KULIMA WAJE, MAANA WAPO. GARI LIKIKUSHINDA , SISI WAPIGA MISELE TUPO......Hebu tupatie mawasiliano ili tumshauri vilivyo tafadhali maana mambo mazuri hayapo huko tu