Nimeamua kwa hiari yangu kusitisha...

Nimeamua kwa hiari yangu kusitisha...

Donpela

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2011
Posts
2,040
Reaction score
592
Habari wadau,
natumai wote wazima wa afya na mmerejea katika mambo yenu ya awali baada ya kusherekea vyema sikukuu za mwisho wa mwaka na kuanza mwaka mpya..
Binafsi nimeamua kuanza mwaka kwa kujizawadia zawadi ya kujipa likizo ya miezi 12 bila kunywa kileo cha aina yoyote
>najua itakua vigumu kutokana na marafiki na maisha niliyozoea awali ila wakati nasherekea mwaka mpya nilikua katika maombi na T.B JOSHUA kupitia luninga, na akasema kwamba mwaka "2014 is a bridge year, you will either fall or reach your destiny"
> nataka kujipa likizo niweze kuishi maisha bila kileo au kunywa yanaendaje ili nipime na mipango yangu

>>Napenda kuwaomba radhi sana TBL na SBL kwa hasara ntakayo isababishia..
>>naomba sana kutiwa moyo na nyie ndugu zangu humu jamvini...
>>KAMA KUNA MTU ANA MCHANGO WOWote ntashukuru sana na kama umekwazika //well chota dhambi tu..sio wakuku hukumu mie

...>>>>UPDATES<<<<<

HABARI WANA JAMVI...
Nachapa huu ujumbe kwa masikitiko kutokana jana baada ya vishawishi vya kadri siku 24 bila kusuuza koo....yalinishinda na kujikuta nikibwia fundo za castle baridi tatu chap...
MORAL OF THE STORY ; WE HAVE TO FAIL INORDER TO PASS
 
Mungu akusaidie ktk uamuzi wako. Napenda tu nikupongeze huo uamuzi uliochukua ni mzuri sana kwani familia nyingi zimekua wahanga wa hii kitu. Wengine walikosa kusomeshwa kisa baba chapombe hivyo ndoto zao ziliishia ndotoni.
 
Hongera sana ila vema ukajiwekea malengo ya kuacha kabisa maana kupumzika hakuna guarantee unaweza ukapiga tena huku ukijiliwaz kuwa umepumzika vya kutosha ngoja uonje
 
Hongera sana kwa uamuzi wako wa busara. Nakutakia kila la heri. Utakutana na vikwazo lakini usirudi nyuma. Wapo watakaokucheka wakisema umechanganyikiwa au umefulia, baadhi ya marafiki watakuacha, na mengine mengi ya kutaka urudi nyuma. Songa mbele - unaelekea kwenye mafanikio. Mungu na akutie nguvu ili uache kabisa.
 
Kuacha pombe ni uamuzi wako binafsi. Unaweza kuacha kunywd na una marafiki wanywaji kuliko kawaida. Niliacha kunywa pombe miaka minne iliyopita na marafiki zangu bado wanakunywa. Tulikuwa tukienda out na washkaji mi naagiza grand malt nakunywa mpaka navimbiwa. Ila kama huna msimamo we usikaribiane nao mazingira ya ulevi.
 
Hongera kama ni kweli. Ila vipi na kuhusu ile ...... Na yenyewe umesitisha au?
 
Hongera sana,sasa sio upumzike tu bali acha kabisa. Hiyo ni hatua mojawapo ya kumshinda yule mwovu...
 
Utayaweza maji?

Karibu kwenye club ya wanywaji wa maji.....it is refreshing and healthy....but only if you can stand the temptation...!

Babu DC!!
 
Habari wadau,
natumai wote wazima wa afya na mmerejea katika mambo yenu ya awali baada ya kusherekea vyema sikukuu za mwisho wa mwaka na kuanza mwaka mpya..
Binafsi nimeamua kuanza mwaka kwa kujizawadia zawadi ya kujipa likizo ya miezi 12 bila kunywa kileo cha aina yoyote
>najua itakua vigumu kutokana na marafiki na maisha niliyozoea awali ila wakati nasherekea mwaka mpya nilikua katika maombi na T.B JOSHUA kupitia luninga, na akasema kwamba mwaka "2014 is a bridge year, you will either fall or reach your destiny"
> nataka kujipa likizo niweze kuishi maisha bila kileo au kunywa yanaendaje ili nipime na mipango yangu

>>Napenda kuwaomba radhi sana TBL na SBL kwa hasara ntakayo isababishia..
>>naomba sana kutiwa moyo na nyie ndugu zangu humu jamvini...
>>KAMA KUNA MTU ANA MCHANGO WOWote ntashukuru sana na kama umekwazika //well chota dhambi tu..sio wakuku hukumu mie

Hongera sana, nakuombea iwe ni likizo ya maisha yako yote uwapo duniani.
"heri ya mwaka mpya"
 
Back
Top Bottom