(Hii ni thread yangu niliyoileta hapa JF tarehe 15 January 2016, kwa bahati mbaya sana mods wakaiondoa...sikutaarifiwa juu ya sababu zao za kufanya hivyo ila naamini yeyote aliyefanya hivyo aliteleza kibinadamu kama inavyotokea kwa wengine. Nimeileta tena leo hili niwajaze maarifa wanajamvi )
TUNDU ANTIPAS LISSU - Mpuuzi niliyeamua kumpuuza.
Tuanze kwa AMANI..
Bwana huyu ameshazoea kuwa kituko "A laughing doll" kwa watu hivyo mara nyingi anapotoa kauli zake "hafikirii" uthabiti na matokeo ya kauli hizo.
Hivi karibuni katika mahojiano yake ktk vyombo vya habari amenukuliwa akimkashifu Mhe Rais, Dkt John Pombe Magufuli kuwa ni mtu anayefanya kazi zake kwa kutaka "headlines" kwenye vyombo vya habari..
Lakini hakuishia hapo, akaeleza kuwa Mhe Magufuli ni mtu asiyefuata Sheria na kanuni za Utawala bora..akitaja kuwa hatua zinazochukuliwa "kusafisha" Serikali na Wezi Serikali ni kinyume na Sheria.
Ni Mpuuzi pekee, anayeweza kusema kuwa kufukuza wezi, wala Rushwa na wahujumu uchumi waliotengeneza mitandao ya wizi serikalini ni Kwenda kinyume na utawala bora...na kisha akadai kuwa CHAMA CHAKE, kinaendelea na mapambano dhidi ya rushwa na wezi Serikalini.
Sioni haya, wala sitaomba radhi, nitasema hili popote pale na SITAFUTA KAULI kuwa kwa ujinga na upofu wa fikra alionao Mhe TUNDU ktk hili yeye ni JIPU miongoni mwa majipu yanayosumbua nchi hii.
Kwa kuwa mimi siungi mkono na nimejitenga mbali na UPUUZI nasimama kumkemea TUNDU kama vile Injili ya Bwana inavyoelekeza wema kukemea UOVU.
Nawatakia Ijumaa njema.
Wenu.
JULIANA.