Nina zaidi ya mwezi hapa nilipo kanda ya ziwa sijaona taarifa ya habari ya saa mbili usiku. Kila siku umeme unashinda ila ikifika saa moja na robo wakati wa taarifa ya habari ya Channel 10 ambayo pia huchelewa kuonyesha habari za kampein wanakata umeme, kwa hiyo huwa nawahi kuangalia taarifa ya ITV saa 12 asubuhi.
Sasa wameanza mtindo wa kukata umeme wakati wa kusomwa taarifa hiyo na wanarudisha umeme mara taarifa inapokwisha .
Je, kwa ratiba hiyo TANESCO haitumiki kisiasa ?!
CCM kwa mtindo huu tegemeeni kukosa kura zaidi kuliko, kwani mnatia hasira sana.