Wasalaam Wadau wa JF na GT wote.
Ninapoandika Uzi huu kwasasa Hatuna Umeme hapa Tulipo, tatizo hili hapa kwetu
#Kilosa halijaanza wiki iliopita Tarehe 07/09/2015 wakati Tanesco wakitangaza Kujaribu mitambo ya Gesi.
Huku kwetu Tatizo la kukatika Umeme kwa Masaa 16 mpk 18 kwa siku limeanza Tangu mwezi wa Saba (07) Mwanzoni, ni takribani Miezi mitatu sasa hatuna umeme wa Uhakika na Bila Taarifa yeyote kutoka katika Shirika hili la Ugavi wa UMEME.
Wiki iliopita TANESCO walipotangaza mgao utakoma Tarehe 14/09/2015 tulijipa moyo basi nasi tumepona, UMEME uliendelea kukatika, Likaja Tangazo Umeme wa uhakika unapatikana sasa Ijumaa tarehe 18/09/2015 tukaisubiri Iyo jana umeme pia ukakatika kwa masaa 13.
Leo tena nnapoandika sasa Umeme umekatika saa 01:53 asubuhi hii na kurudi bila shaka ni mpk saa 4 usiku.
Sasa naomba TANESCO watuambie kuna nini kinaendelea mgao huu miezi mitatu mfululizo?
Najiuliza kwanini Mgao bila taarifa?
Hapa mimi kama mimi nimeshapata Hasara ya zaidi ya mil 4 tangu mgao Uanze Mkoa wa Morogoro, ikiwepo wilaya ya kilosa. Na kuna taarifa, sio hapa MOROGORO tu, maeneo mengi nchini YALIOPO PEMBEZONI yana mgao mkali sana wa masaa kati ya 16-24
Najiuliza Pia waandishi wa habari mpo wapi Kuutetea Umma ulioko pembezoni ya miji mikubwa kwa mateso haya?
Yan mnaandika tu mgao wa UMEME wakikosa umeme wakazi wa Dar es salaam. Kwann? Au hamjui haya?
Nadhan Tunahtaji kufikiri pamoja. TANESCO tangazeni mgao Tujue, tujipange tununue Majenereta. Mna turudisha nyuma kimaendelo na maisha yamekuwa ghali maradufu.
Mashine za unga zinasaga usiku wa manane, Wachoma mageti hawalali wanakesha kumalizia tenda za watu. Samaki wangu wa mil 3 waliozea kwenye freezer
😡 nikifika hapo. Huwa natamani kufanya lolote. (hasira sana). Maana nakaribia kufiliska.
Eeh Mungu Nisaidie!
NOTE: umeme huu una katika kila siku iendayo Kwa Mungu. Na hatujui hatima yetu
Tafadhali
Moderator msiunganishe uzi huu, unahtaji Majibu yakina sana, hasara tunayopata kwa mgao huu ni kubwa kuliko propaganda zinazofanya na Tanesco.