Nimeamini kweli mke ni ubavu wa pili

Lazima washangae, ngoja niweke ndani ya malengo yangu mwaka huu by december lazima ni post nimefikia wapi

Ila wanadai wanaume wanajua kupika zaidi ya wanawake, wako makini sana, sijajua kama kuna ukweli ndani yake
Ukweli kabisa, wakati wa kupika vile mnavopika kiaina mtu anaweza hisi unaboronga msosi

Ila baada ya kuiva na kutenga mezani huo utamu wake sasa unaishia kujiramba na kutamani upikiwe tena

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole na hongera.Ila ulichagua pishi gumu Sijui Kwanini.Umenikumbusha kuna siku nlikua naumwa mr.akaingia jikoni alinipikia mchemsho mzuri wa samaki.Ugali ndo alichemka alipika mkubwa Sana alishindwa kukadiria maji.Mwenyewe akasema tutakula mchana na usiku.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kweli Mungu ni mwema sana na Namshukuru kwa siku hii ya leo. Imekuwa na changamoto nyingi sana hii siku ya leo ila najua nimezishinda na usiku umeingia hapa ni kwenda kulala tu hakuna purukushani za ziada.

Kwanza kabisa wife kasafiri kaenda kwa wazazi wake, leo nimejikuta niko kwenye mitihani kidogo. Mke wangu amejaliwa kweli kwenye mapishi, huwa akiwepo nyumbani amepika; lazima niwahi nyumani nikapate maakuli. Napenda sana kula mimi na nafurahi sana kumpata mtu mwenye kujua kupika mapishi mengi sana.

Asubuhi imeanza nimeamka na njaa kali sana, imenibidi nikatafute sehemu nipate kifungua kinywa. Kwa kweli kila napoenda ukiangalia mazingira ya upishi na hata sehemu zenyewe kuna mainzi nimeshindwa kula ikabidi ninunue mkate nipike chai ninywe

Ile nimebandika chai nimeweka majani na sukari nikasubri ikachemka ili ninywe. Nilivyokunywa tu chai ilikuwa chungu sana kama mwarobaini. Ikanibidi nipige simu nimulize wife vipi mbona chai chungu majani leo mbona yamekuwa machungu. Akanijibu nitakuwa nimezidisha majani na yeye huwa anaweka vitu vingi zikiwemo mdalasini, iriki na vingine kanitajia sivijui. Kwa njaa ile nilimeza na ile mikate kama nyoka anavyomeza kuku.

Nilipomaliza nikaenda washa moto jiko la mkaa (Jiko Koa). Ule mkaa ulikuwa umelowa na maji. Niliuwasha sana kama saa nzima hivi ndo mkaa ukawaka. Niliwasha na karatasi wapi nikajikuta nimechana daftari la mtoto la shule lote kesho nina kazi ya kwenda kununua jingine. Nikaenda store kwenye makorokoro nitafute tu hata kimfuko cha plastiki, nilipokipata ndio kikawashia moto

Kazi ikaja bhana kuzisukuma, nilisukuma sukuma sukuma kila nikisukuma duara haliji naona linakuja ovyo ovyo. Huwezi amini nilisukuma ile chapati moja nusu saa. Nikasukuma sana mwisho nikaona nipike hivyo hivyo. Ile kuiweka jikoni tu na mafuta wacha niungue lile frampeni lilikuwa la moto sana. Mkono wangu nimeungua karibia vidole vyote, cha kusikitisha ile chapati ya kwanza ikatoka kama ina macho vile inanishangaa. Nimeshindwa kuila hii chapati hebu angalieni inavyonitizama kwa dharau kama hivi:

View attachment 1378190

Nikapika chapati ya pili nayo imeungua imekuwa kaukau. Kwa kweli nimemkumbuka sana mke wangu na vyakula anavyonipikia. Nimejua hata kama mwanamke ni mama wa nyumbani hapaswi kudharauliwa kazi ya moto si kazi nyepesi ina shughuli pevu. Ukila chakula cha mkeo ujue ni damu yake, jasho lake, nguvu zake, upendo wake, maumivu yake ya kuungua nk. Kubeza chakula kilichopikwa na mwenzio ni dhambi kubwa Mungu atusamehe tu.

Ila nashukuru chapati moja tu kati ya kumi na tano ndio iliyotoka vizuri nyingine nimeunguza sana. Sijui kama kesho zitafaa kula kiporo, ila kwa kweli kuna haja ya kujua kupika hata kama una mke. Nimekulia katika familia za mfumo dume mwanaume hakai jikoni, siwezi kujilaumu mwenyewe kwa kutojua kupika. Kwa kweli leo nimejua umuhimu wa mke wangu katika maisha yangu, Nakupenda sana Mke wangu, Mungu akujalie maisha marefu, ukiniacha mwenyewe nitakonda. .
View attachment 1378191

At least this one came out better compared to others: (Sadly, It is the only one)
View attachment 1378193

Kwa jinsi nilivyoungua Yesu tu ndio anajua, Nawasisitizia tu tuwaheshimu sana wake zetu. Hata kutofanikiwa ni kwa sababu tu ya kutoheshimu nafasi za wenza wetu katika maisha yetu. .

Its so funny eti mke kasafiri halafu eti mwanaume unaingia jikoni kupika mpaka unachukua na picha na ku-upload JF!

Whats this?

Niingie jikoni tuseme sina vitu vya kufanya?

Tuseme hoteli zote na baa zote,Chinese restaurants,KFC,Merry Brown and some shit like that vyoote hivyo nisiende agiza au hata kitimoto eti niingie jikoni napika mataputapu?

Aisee kuna watu wana muda wa kuchezea beyond measure!

Aisee wanadamu tunatofautiana sana!
 
Bora yako wewe unaweza kutengeneza irregular chapati, mimi najua kuzichoma tu zikiwa duara tayari. Ia ndizi, wali, ugali wetu wasukuma, samaki kukaanga, nyama, napika hatari.
 
Mwanaume lazima ujue kufanya vyote kama usafi, kupika na kadhalika. Ina maana mkeo akiumwa au kusafiri we utaishije? Au kabla hujaoa ulikuwa unaishije? Huwezi kula take away kila siku. Hakuna kitu kizuri kama siku moja moja kutenga kamuda na kuipikia familia hii ina raha yake sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah aise mazee asikuambie mtu hawa watu wanne Mama, Mke, Dada na Dada wa kazi ni wakuheshimu sana
Kuna siku nilibaki mwenyewe home nikasema wacha leo nipike ugali c naonaga jikoni ukipikwa fasta fasta 15min mzigo tayari, sitakaa nirudie kuingia jikoni kwa yalionikuta.
Nilieka maji fresh kwenye jiko pamoja na sufuria shida ilianza kwanza sijui unatakiwa ujue kukadiria maji ujue ni ugali wa watu wangapi, mi nilijiekea maji.
Yalivochemka nikaanza kueka unga na kukoroga, kila nikikoroga mzigo hauwi mgumu yani unakua mwepesi zaidi uji.
Nikaendelea kueka unga yakaja mabonge mabonge makubwa, kimoyo moyo nikajisemea haya yanaishaga ukiwa mgumu wakati wa kusonga. Mzigo nikaendelea kutia unga , weka unga na mimi.
Dah aise nakuja kusonga na mwiko umekua mgumu mwiko hausogei nikajaribu na nguvu zangu zote kusonga, huku nasema mbona yeye anasongaga tu hivi chap chap. Nikalazimisha ule mwiko ukavunjika huku unga umejaa karibia jikoni kote kila mahali ni unga.
Nikachukua lile sufuria na unga wake pamoja na ule mwiko uliovunjika nikatupa vyote. Dah aise wanawake wana nafasi yao kubwa sana.
 
Pole na hongera.Ila ulichagua pishi gumu Sijui Kwanini.Umenikumbusha kuna siku nlikua naumwa mr.akaingia jikoni alinipikia mchemsho mzuri wa samaki.Ugali ndo alichemka alipika mkubwa Sana alishindwa kukadiria maji.Mwenyewe akasema tutakula mchana na usiku.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hahah uliweza kula lakini???
 
Hata kama mwanaume huruhusiwi kuingia jikoni lakin mpaka huo umri hujui kupika chai!!??... Its so shameful!!! japo umesema hutaki dharau na maneno ila hapo umefeli sana..
 
Hata kama mwanaume huruhusiwi kuingia jikoni lakin mpaka huo umri hujui kupika chai!!??... Its so shameful!!! japo umesema hutaki dharau na maneno ila hapo umefeli sana..

Wengine wenye kebehi siwajibu ila wewe ngoja nipoteze mda kukujib

Umepata sh ngapi kunikebehi? Umepata faida gani? Usichukulie maisha yako ukafananisha na mie nilivyoishi. Usilazimishe 1 iwe mbili, hujui chochote kuhusu mimi alafu unakataka kuniponda.

Angalia maisha yako huna kasoro au wewe umekamilika
 
Wengine wenye kebehi siwajibu ila wewe ngoja nipoteze mda kukujib

Umepata sh ngapi kunikebehi? Umepata faida gani? Usichukulie maisha yako ukafananisha na mie nilivyoishi. Usilazimishe 1 iwe mbili, hujui chochote kuhusu mimi alafu unakataka kuniponda.

Angalia maisha yako huna kasoro au wewe umekamilika
Kasoro gan ww? Kupika chai kunaitaji elimu gan kuanzia unakuwa mpaka ulipofika sasa....!!
 
Halafu kuna watu wanasema "mwanamke ni chombo cha starehe".
Btw, hiyo chapati iliyotoka ya mwisho ni zuri sana hongera.
Huyu jamaa ni mtaalamu huwekuwa hujui kupika chapati itoke bomba vile alafu ametoa na idadi ya kilo moja.

God save us
 
Hongera kwa kutambua umuhimu wa mke!Ila mkuu ungeacha uzi upumue,acha na wengine waandike tusome uzoefu wao au maoni yao!Sasa ukijibu kila comment wengine inatuchosha kupitia!Ungeweza kujibu comment chache zenye uhitaji wa kufanya hivyo!
Yaani mimi comments zake sisomi na si kwa urefu ule. Comment ndefu utafikiri uzi

God save us
 
Dah aise mazee asikuambie mtu hawa watu wanne Mama, Mke, Dada na Dada wa kazi ni wakuheshimu sana
Kuna siku nilibaki mwenyewe home nikasema wacha leo nipike ugali c naonaga jikoni ukipikwa fasta fasta 15min mzigo tayari, sitakaa nirudie kuingia jikoni kwa yalionikuta.
Nilieka maji fresh kwenye jiko pamoja na sufuria shida ilianza kwanza sijui unatakiwa ujue kukadiria maji ujue ni ugali wa watu wangapi, mi nilijiekea maji.
Yalivochemka nikaanza kueka unga na kukoroga, kila nikikoroga mzigo hauwi mgumu yani unakua mwepesi zaidi uji.
Nikaendelea kueka unga yakaja mabonge mabonge makubwa, kimoyo moyo nikajisemea haya yanaishaga ukiwa mgumu wakati wa kusonga. Mzigo nikaendelea kutia unga , weka unga na mimi.
Dah aise nakuja kusonga na mwiko umekua mgumu mwiko hausogei nikajaribu na nguvu zangu zote kusonga, huku nasema mbona yeye anasongaga tu hivi chap chap. Nikalazimisha ule mwiko ukavunjika huku unga umejaa karibia jikoni kote kila mahali ni unga.
Nikachukua lile sufuria na unga wake pamoja na ule mwiko uliovunjika nikatupa vyote. Dah aise wanawake wana nafasi yao kubwa sana.
Nimecheka sana mkuu.
 
Back
Top Bottom