Niliyoyaona Mumbai(Bombay)

Niliyoyaona Mumbai(Bombay)

Kwa uchafu umelenga hata zile hoteli kubwa unaweza pishana na mtu anajisaidia haja kubwa kwenye lango la kuingilia...
Pia kuna maeneo yana ombaomba balaa, ombaomba anakuganda haswa yaani akikufuata usipompa chochote hakuachi ataenda na wewe kama unatembea hata kama ni km5 hadi umpe chochote...
Makazi kiukweli yanachangamoto huwezi jua makazi ya proffesor au ya mtu ambae hajaenda shule, kuna maeneo unaweza mkuta prof anaishi chumba ambacho store ina uhafadhali....
Vyakula vinapilipili sana, hadi pipi utakuta ina pilipili...
 
Wadau wikiiliyopita nilibahatika kwenda matembezi ya wiki moja nchini India Nilifikia katka jiji la Mumbai. kama ilivyo kawaida sehemu yeyote ukifika kwa mara ya kwanza lazima kuna mambo kadhaa kama si yote yatakuwa ni mageni kwako. Yafuatayo ni baadhi ya yale niliyo yashuhudia huko Mumbai. (1) Foleni ya magari na Pikipiki Sijawahi katika maisha yangu kudhani hata siku moja kama kuna sehemu kunawezakuwepo na msongamano wa magari na pikipiki kama ilivyo mumbai (2) Kelele za honi za magari na pikipiki nadhani kuna maeneo india kama chombo chako cha moto hakina honi huwezi kuendesha Ninaposema kelele za honi ni kelele kweli huwezi amini pikipiki imefungwa honi ya gari (3) Uchafu jamani ukweli ni kwamba hawa ndugu zetu ni wachafu Ukiingia kwenye mighahawa hii ya hali ya chini kwakweli kama una kinyaa huwezi kula. Nimambo mengi sana nimejionea mwenyewe huko kwa wenzetu lakini sio rahisi kuyaeleza yote hapa. Mwingine aliewahi fika huko kwa wadosi amwage hapa alichojifunza. Sikunyingine nitaelezea nilichofahamu kuhusu zile Hospitali maaarufu za Appolo Nawasilisha

Hospitali za Apollo sio za kitabibu bali ni kitengo maalum cha utalii, wanaendesha kitu kinaitwa "Medical tourism", kaa chonjo!!
 
Hizo honi hapa bongo naweza zipata dukani?? nataka nisumbuane na shemeji zangu wa kimakonde mahuta huku
Mkuu hamisj hivi basi la Mahuta kupitia Kisangara bado lipo??duuuh huko utawasumbua sana Wamakonde dadeki...hasa pale Newala mjini karibu na Posta kwa Braza Adam...Inapikwa sambusa moja tamu sana!Msimu wa mihogo kila mtu na kipisi cha muhogo mdomoni....Daaah Newala kuchereeeee
 
INDIA umetoka wiki iliyopita thread unaanzisha leo baada ya narendra modi kuhutubia mie nawaambia hivi.... mtaisoma namba na mikataba imeshasainiwa tufanye kazi, tujenge nchi chadema hamuwezi chukua nchi kwa thread zisizokuwa na kichwa wala miguu kama hizi
 
Vipi, uliweza kuonana na Amita Bachani na Misuni Chakalaboti...?
 
Ungeangalia vizuri ungegundua wako location wanaigiza muvi tu.
 
Uko sahihi.... kwa usafi sasa wanajitahidi... miaka ya 2008 nilienda kule ulikuwa ukitoka hotel kwenda nje kutembea hata kama ni 10mis ... ukirudi lazima uoge.... kulikuwa ni kuchafu kweli kweli.... kwa sasa naona kuna paving blocks na sehem nyingi za uchafu wanazisafisha....
 
Mwenye kujua kidogo kuhusu jiji la #Bangalore anidadavulie
 
Mkuu nakubaliana na wewe kwa namba 1 na 2. Uko sahihi kabisa. Ila kwa namba 3 sijui maana sijabahatika kuingia kwenye hiyo migahawa uliyosema. Mimi pia nilikuwa huko mwaka jana. Nitarudi hapa jukwaani kuongezea mkuu...good for memory!
 
Mie Nikiingiaga ndani ya daladala kuchefukwa... mashule yetu mengi wanafunzi hujisaidia vichakani....
Nikipita mitaa ya Congo hupataga kisunzi...........
Nikiingia uwanja wa maonyesho ya 77 nazuiga tumbo hadi baadae...
Nikipandaga mabasi ya mikoani na bana pua na kuziba masikio.........
Sijui eapoti maji hakuna Hospitali maji na umeme wa kusasua...........


WEWE mf bean. Mumbai ni jjiji lenye wakazi (24m) Zaidi nusu ya idadi ya waTZ.... halafu huduma za tiba zote hupatikana papo hapo!! na kila aina upasuaji na ubadilishaji viungo bila kucheleweshwa na mlolongo wa Siasa... ni pesa yako !!
Jijila Mumbai lina miaka Zaidi 3000 toka lijengwe.... Soko la kwanza la dhahabu duniani ni Mumbai... bandari kuu imeshemiri usafiri wa maji kuunganisha dunia.....

mara ingine anza na Ukweli na haki ya mazuri yenye faida!!
Mumbai ni kusafi ukilinganisha na Kolkata. Magari ni mengi lakini hukuti ajali kama kwetu. Heshima ya uhindini huwezi ipata popote, hebu fikiria mtoto anamwogopa baba utadhani ni malaika. Bikra uhindini ni jambo lenye tija. Ingawa uchafu, kutema mate ovyo, kukojoa barabarani hata kama Samora Avenue ni jambo la kawaida na watoto wa kiume kwenda kujifunza au kupunguza uhanga kwa machangu ni kawaida.
 
Mumbai ni kusafi ukilinganisha na Kolkata. Magari ni mengi lakini hukuti ajali kama kwetu. Heshima ya uhindini huwezi ipata popote, hebu fikiria mtoto anamwogopa baba utadhani ni malaika. Bikra uhindini ni jambo lenye tija. Ingawa uchafu, kutema mate ovyo, kukojoa barabarani hata kama Samora Avenue ni jambo la kawaida na watoto wa kiume kwenda kujifunza au kupunguza uhanga kwa machangu ni kawaida.
Uhanga ndo nini?
 
Sioni maana kuwadiscuss wahindi. Watu wajaabu sana wale. Nimetembea nchi nyingi na kukaa marekani kidogo lakni india naomba Mungu nisikanyage,ptuu!
 
Mumbai ni kusafi ukilinganisha na Kolkata. Magari ni mengi lakini hukuti ajali kama kwetu. Heshima ya uhindini huwezi ipata popote, hebu fikiria mtoto anamwogopa baba utadhani ni malaika. Bikra uhindini ni jambo lenye tija. Ingawa uchafu, kutema mate ovyo, kukojoa barabarani hata kama Samora Avenue ni jambo la kawaida na watoto wa kiume kwenda kujifunza au kupunguza uhanga kwa machangu ni kawaida.
Wanathamini sana bikra.?!
 
Back
Top Bottom