Niliyoyaona Jijini Mwanza

Niliyoyaona Jijini Mwanza

Wahindi wenyewe kuna wengine hawajui kuongea kihindi hata kidogo...wanaongea lugha za ukanda wao mfano watu toka tamil nadu lugha tofauti kabisa na hao wa Mumbai
Yeye amekariri kisa tu media zao huwa zinapanga Nini akisikie Basi. Nature ya binadamu Ni Ile Ile regardless of location sema labda hivi mabadiliko haya kuingiliana na elimu Yana displace values za watu
 
Wakuu wazima?

Nafikiri kuna kapost kangu niliwah post humu kuuliza sehem nzuri ya kupumzika kwa hapa Mwanza.
Sasa kwa kipindi hiki cha wiki 2 nilizokaa huku hay ndo niliyoyaona na kujifunza

1. Wanawake wanapiga kazi sana huku(wanajishughulisha) mida ya jioni barabarani utakutana nao sana wakiuza either matunda, dagaa, samaki, maharagwe yaliyochemshwa tu, nyanya na vikorombwezo vingine4, pia wanachoma mahindi na kuyauza.

2. Wengi wa wasichana huku ni waoga sana hasa kwa strangers.

3. Draft la huku wengi hucheza French( hawajui kuhusu British).

4. Kila wanapokaa hudhani wote ni wa huku hivyo huongea tu kilugha.

5. Hotels and Lodge za huku no bei rahis sana sana huanzia 30k.

6. Mwanza ni mji mzuri sana, una mandhari nzuri kuliko Arusha( kwa mtazamo wangu)

Asanteni wakuu
Jamani tuache huu ukoloni wa kuita kilugha? Lugha ni lugha zote tu na tuseme kama Kisukuma, Kinyakyusa au Kijerumani na Kama hatujui tunasema. Tukisema kilugha Km kukejeli na kuona ujinga
 
Mkuu hakuna mji ambao una watu wabaya tu, wapo ambao ni wazuri. Hata Gamboshi kunakosifika kwa uchawi wapo ambao hawapractice huo uchawi, lakini hii haiondoi kwamba Gamboshi kuna tabia fulani ambazo zinafahamika.

Labda nikutolee mfano mwingine; mimi nimesoma hapo High School, na pale shule machalii wa chuga walikuwa wanamakundi yao na wanajiona wao ndo wao (again, sio wote) sijui walikuwa wanajiona wanajua kuvuta bange vizuri au vipi. Hawa jamaa walikuwa wanatuchukia sana tuliotoka mikoani tena hasa hasa Dar, yani mtu umevaa zako smart umepiga pasi basi utaitwa bishoo mara mtoto wa mama na majina mengine mengi sababu tu wao labda wapo rough na milegezo yao. Kuna scenario moja ilitokea nikashangaa sana, kuna mchizi wetu wa Dar alikuwa akinata na mtoto mmoja mkali wa chuga, na huyo demu kuna jamaa wa chuga alikuwa akimpenda sana lakini demu akawa hamuelewi. Siku moja tupo dinner tunashangaa mchizi kabananishwa na machizi kama watano wa Arusha wanataka kumfanyia fujo. Sababu tu eti anatembea na demu wa Arusha yeye mtoto wa mama wa Dar aachane nae. Kilichosaidia na sisi wa Dar tulikuwa na jamaa mmoja ulikuwa unamtoka mkono kinoma, yule ndio alikuja kuokoa lile jahazi. Bila hivyo lazima jamaa wangemzuru!!

Sasa hiyo ni scenario moja tu, lakini tabia kama hizi ni kawaida sana hapo Arusha, ndio maana hata mimi nilivyorushiwa mawe wala sikupanic nikajiona kama ni mkosefu. Nalikuwa nikifahamu hizi tabia zao!!

Sabaya na Gambo ni typical mfano wa vijana wa Arusha na tabia zao. Ukiacha hawa ambao wana tabia za ovyo ovyo wapo washkaji wa Arusha ni watu poa sana. I can’t forget some memories at Club AQ enzi hizo, Masai Club, La Fiesta na Pool table na washkaji pale Sun-dip, swimming Arusha Hotel!! I had a very good time there na siwezi regret
Kila mkoa unawatu wa hovyo.

Au umesahau hapo Dar es Salaam kuna vijana wa hovyo wanajiita panya road?

Sasa watu wakianza kuandika uhalifu uliowakuta wakiwa miji mingine hapa Tanzania hatutafika mwisho?

Kingine. Mambo ya ubabe enzi za ujana ni kawaida tu. Tena vijana umri miaka 16 - 20?

Hiyo age vijana wengi wadogo wakiume ni kawaida kuonyeshana ubabe wa hapa na pale. Hasahasa shuleni.

Na mimi nasema hiyo ni sawa tu. Miaka hiyo ndiyo miaka ambayo vijana wadogo wanajifunza namna yakuwa wakakamavu lakini pia namna yakujilinda kama kundi.

Ni survival skills. Kama hutokei mtaa utashindwa kuelewa.

Mwisho hongera kwa kumbukumbu nzuri ulipokuwa A town.
 
Ila watu wanaosemaga Mwanza ni Mji mzuri Huwa wananishangaza sana
Kwa hiyo kama wewe unaona Mwanza siyo mji mzuri unataka kila mtu awe na mawazo kama yako? Au wewe kwa mtazamo wako kwamba Arusha ni mji mzuri unataka kila mtu akubaliane na wewe? This is the world of differences. Ukipendacho wewe mwingine hakipendi! Mimi mwenyewe nakushangaa kufananisha kamji ka Arusha na jiji la Mwanza!
 
Ngoja nikuambie kitu.

Wakazi wa A town wapo na strong personality kama vile walivyo Wakenya.

Hii inasababisha watu wanaotoka mikoa mingine kujiona inferior wanapokutana na watu kutoka A town.

Hii utagundua kwa urahisi sana mashuleni na hata makazini. Hasahasa kwa vijana chini ya 35 years.

Ni shida kubwa.
Hakuna kitu kama hicho...vijana wa Arusha Wana matatizo ya ushamba na too much ego inayowafanya washindwe kuishi vyema na watz wengine...
 
🤣🤣🤣Kwakweli nilikuwaga nawasikia ila kwa nayoona kwa ndg hawa,, Arusha ni mibange na wasela mavi,,, niko njiro mkuu njoo unipige
Hapa tunajadili mada na si vinginevyo.

Umeleta madai vijana wa Arusha wanavuta bangi. Nikasema sawa hilo ni dai lako.

Lakini unapaswa uthibitishe. Usipofanya hivyo basi wajumbe hawawezi kukuchukulia kwa uzito unaostahili.

Pia unazungumzia nije nikupige. Je, hiyo inatija yoyote katika mada tunayojadili?
 
Kujaribu nini kuvuta bangi?? Pombe yenyewe tu situmii, hiyo bangi labda ipikwe mboga
Usijaribu kuongea kilugha kwa simu ukija mjini kilugha ongea huku...

Hiyo bangi wala usijaribu hata kwenye mboga utawehuka na kutatembea uchi mjini watu wateseke kukusitiri
 
Hakuna kitu kama hicho...vijana wa Arusha Wana matatizo ya ushamba na too much ego inayowafanya washindwe kuishi vyema na watz wengine...
Vijana wengi wanaotoka mikoa mingine tofauti na A town wakiwa college/university hujiona dhaifu mbele ya wanafunzi wenzao kutoka Arusha.

Unafahamu kwanini?

Kwasababu vijana waliozaliwa Arusha wanapata advantage yakukutana na wageni wanaotoka mataifa ya Ulaya na Amerika na hii inawapatia nafasi yakufahamu mambo mapya tangu wakiwa wadogo.

Vijana hawa wakienda shule nakukutana na vijana kutoka mikoa mingine isiyo na utalii basi huona wanajidai au wakorofi.

Ni kama vile wewe ukirudi kijijini kwenu waskaji wa kijiji wanakuona wewe mtukutu na much know.

Uko na swali jingine nikufafanulie?
 
Usijaribu kuongea kilugha kwa simu ukija mjini kilugha ongea huku...

Hiyo bangi wala usijaribu hata kwenye mboga utawehuka na kutatembea uchi mjini watu wateseke kukusitiri
Huyu dada ana ushamba mwingi.

Au dishi limeyumba.

Hafahamu anachosimamia anadhani kuropoka ndiyo kushinda hoja.

Mara analaumu bangi mara anataka ajaribu kama mboga.

Nilimwambia hapo juu namna yake yakufikiria haipo sawasawa.
 
Usijaribu kuongea kilugha kwa simu ukija mjini kilugha ongea huku...

Hiyo bangi wala usijaribu hata kwenye mboga utawehuka na kutatembea uchi mjini watu wateseke kukusitiri
Mbona naongea na cha kunifanya hakipo, hata saiv nimetoka kuongea kilugha changu vizuri tu, bangi ni yenu mi hainihusu
 
Mbona naongea na cha kunifanya hakipo, hata saiv nimetoka kuongea kilugha changu vizuri tu, bangi ni yenu mi hainihusu
Wewe endelea tu ipo siku utajuta kuja mjini ukubwani😅
 
Vijana wengi wanaotoka mikoa mingine tofauti na A town wakiwa college/university hujiona dhaifu mbele ya wanafunzi wenzao kutoka Arusha.

Unafahamu kwanini?

Kwasababu vijana waliozaliwa Arusha wanapata advantage yakukutana na wageni wanaotoka mataifa ya Ulaya na Amerika na hii inawapatia nafasi yakufahamu mambo mapya tangu wakiwa wadogo.

Vijana hawa wakienda shule nakukutana na vijana kutoka mikoa mingine isiyo na utalii basi huona wanajidai au wakorofi.

Ni kama vile wewe ukirudi kijijini kwenu waskaji wa kijiji wanakuona wewe mtukutu na much know.

Uko na swali jingine nikufafanulie?
Yaan hata maneno yako yanaonesha haujiamini na kujikubali...kuna watu unaona ni Bora zaidi yako so unakuwa na shobo nao...

Trust yourselves bro...Haya mambo ya kuishi ukiwa unajistukia sio mazuri kwa maendeleo binafsi....na vijana wengi wa Arusha mna ili tatizo...ndo maana mnajiingiza kwenye bang, kuolewa na vibibi...kuiga umarekani ambao hata hao wamarekani wanajithidi kuusolve..nk nk
 
Kwenye kilugha ni uongo, Mwanza imejaza watu wa mikoa mbali mbali. Hasa mkoa wa Mara, lugha itumikayo ni kiswahili tu.
anaweza akawa sahihi licha ya wageni wengi kuvamia mwanza lakini wasukuma bado wapo wengi sana naupendelea xana kuongea kilugha, busweru,buhongwa namaeneo yapembeni mwa jiji bado kunawazawa wengi xana....
 
Back
Top Bottom