Nilivyomuona Mwana F.A Anafunguliwa Mlango wa VAT, Hakika Hakuna Ajuaye Kesho Yake

Nilivyomuona Mwana F.A Anafunguliwa Mlango wa VAT, Hakika Hakuna Ajuaye Kesho Yake

ERTUGRUL BEY

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
11,529
Reaction score
21,530


My people,

Hakika hakuna ajuaye kesho yake, hata wewe kamwe usije kujikatia tamaa katika maisha kwahakika siri ipo kwa Muumba wetu.

Haimaanishi kwamba nawe utakuja kutamba na VAT laa,namaanisha kwa safari yoyote ya maisha uliyokuwa nayo basi haijaisha mpaka iishe, kwa hiyo endelea kupambana bila kuchoka na amini ipo siku moja nawe utashaini tu

Back in the days, nikiwa ndani ya ukumbi wa Bilcanass pale posta mpya,wakati huo Mwana FA alikuwa anazindua album yake akiwa pamoja na East Coast Team kama kumbu kumbu zangu zipo sawa

Alikuwa amevaa jezi ya team ya mpira wa kikapu Maana Enzi hizo Basketball kama ilikuwa ina mwamko sana, kichwani akiwa amesuka msuko wa twende kilioni, yaani ile kinyamwezi sana, dah ilikuwa way back

Guess what? Today ni Naibu Waziri kitu ambacho hata yeye wakati huo huenda hakuwahi kabisa kufikiria au kuota ndoto hiyo japo kiutani utani, hiyo ndio siri ya maisha ilivyo

Endelea kufunua page za maisha yako huwezi jua page ya mwisho kabisa ikawa na matokeo bora kabisa

Kukata tamaa ni Sumu, endelea kupambana

Ni hayo tu!
 
Yaani unatumia exceptional case kama mhimili wa hoja yako ya jumla? Au nawe ni sawa na motivational speakers wanaokwambia elimu si kitu sana kwa vile eti Mark Zuckerberg aliacha chuo Harvard na kuanzisha Facebook?

Kuna akina Zuckerberg wangapi? Akina Mwanafa je? Zuckerberg angesoma YUDOMU angeanzisha hiyo fesibuku? Wanamuziki wangapi leo ni manaibu waziri kama Mwanafa?

Najua lengo lako ni kututia moyo lakini angalau basi tafuta mifano yenye uhalisia japo kidogo!
 
Washikaji sasa tupo hewani, leo, mwana FA utaoa lini? Hizi kwanja alizoimba mwana FA usingedhani mshua angekuja kuwa mheshimiwa.

Sasa washua wenzake kina AY, king crazy GK, O ten na wanakundi wenzake wengine, vipi hao members wa east coast wao hana interest na siasa ili nao wale shavu siasani?
 
Mwenzenu ni 'kitengo' kitambo tu halafu mnataka kudanganya watu bure tu hapa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom