Nilipomuamsha shetani wa mme wangu

Nilipomuamsha shetani wa mme wangu

SIMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU--- SEHEMU YA SITA

Mume wangu aliondoka, hakunitafuta tena na wala hakupokea simu zangu kabisa, kibaya zaidi hakumuambia mtu yoyote, kila kitu alifanya kimya kimya, nilaimua kutafuta chumba kwaajili ya kukaa kwa muda kwani gharama za hoteli zikukua kubwa. Baada ya kama wiki tatu hivi mume wangua linitafuta, alishaanza kulipa ule mkopo, kuna kiwanja kingine ambacho alikua ancho alikua ndiyo kaanza ujenzi, alikiuza na kupatakama milioni 22, alilipa yote, lakini mambo bado hayakua sawa, alinitafuta ili nimfungulie duka.

Kuna pesa nyingine ambayo aliipata kama milioni 12, sijui alikopa wapi lakini kuna rafiki yake alimsharu kuwa afungue duka langu, aanze kuuza vitu asimamie awe analipa mkopo kidogo kidogo. Kwelia lifanya hivyo, alifuingua na kila kitu tukabadilisha majina yakawa yake, akawa analisimamia yeye na kulipa mkopo yeye. Nilimuomba msamaha lakini hakutaka kusikia chochote, aliniambia nimuache kwani kichwa chake hakijatulia.

Mume wangu alipambana,m ndani ya miezi nene alifanikiwa kulipa ule mkopo, alimaliza deni, alirudishiwa hati yake, aliniita na kuniambia kuwa ile hati nibadilishe majina na niandike majina ya watoto wetu, sikua na namna nilibadilisha, lakini bado hakutaka kurudiana na mimi. Kwa mara ya kwanza nilienda kanisani, tuliitwa ili kusuluhishwa, mume wangu aliongea yake na mimi kuongea yake, wasiwasi wake ni kuwa nilikua nimemsaliti hivyo hawezi kukaa na mwanamke mzinifu,.

Niliapoa na kuapa kuwa sijawahi kumsaliti lakini hakunisikiliza, kanisani mambo yalishindikana, ikafikia hatua kuwa kila akiitwa anagoma kwenda. Katika kipindi nilipokua mbali na mume wangu dniyo niligundua kuwa nampenda sana mume wangu, niligundua kuwa siwezi kuishi vila yeye, maisha yalikua ni ya shida sana, sio kama sikua na pesa, hapana, nilikua napenda na nilikua na kila kitu lakini sikua na mapenzi, kila siku nilikua ni mtu wa mawazo, kulia na kusononeka.

Nilitamani sana kuwa karibu na mume wangu lakini ilishindikana, afya yangu ilizizi kuwa mbaya, nikawa ni mtu wa mawazo, kazini siendii tena bila taarifa, nilijikuta nakua mpeke wkani hata ndugu walikua kama wamenitanga hasa baadaya kusikia mambo niliyokua nimeyafanya. Mwaka mmoja baadaye mwanangu mdogo alianza kuumwa, ilitokea hgafla tu alikutwa na uvimbe shingoni na baada ya kwenda kupimwa aligundulika kuwa ana Kansa.

Kwasabbau ya mtoto nmume wangu aliniambia nirudi nyumbani, nilirudi nyumbani tukaanza kuhangaika katika kumtibu mtoto. Ile hali ilitududsiha karibu, nilijua kabisa mume wangu atakaua amenisamehe, maisha yaliendelea na yalikua mazuri, nilijikuta naanza kuwa na furaha tena, nilijikuta naona kama nimepata nafasi nyingine. Ingawa mume wangu hakuwahi kuniambia kuwa amenisamehe au kutaka kulala na mimi lakini nili0na kabisa kuwa upendo wake umerudi, niliona kuwa bado ananipenda na hasa namnaalivyokua ananisaidia kulea watoto wetu.

Kwa bahai mbaya baada ya miezi nane mtoto wetu alifariki dunia, ilikua ni huzuni kubwa sana kwangu, nilikua kama mtu aliyechanganyikiwa kwani alikua ni mtoto wangu pekee wa kiume, niliumia sana kila siku nikawa ni mtu wa kulialial mume wangu alikua karibu sana na mimi, alikua ananijali lakini hakuwahi hata siku moja kuongelea suala la mapenzi, kila wakati nilipotaka kugusia hayo mambo au kuonyesha dalili kuwa ninataka tukutane kimwili alinikwepa, mwanzo ilikua ni sababu ya mtoto anaumwa lakini baadaye alinikwepa tu na kunuiiambia kuwa hayuko sawa.

Nilikua naumia sana kwnai nilikua nampenda na kila siku nilikua naishi naye, kilichokua kinaniumiza zaidi nikuwa baada ya mazishi ya mtoto kumaliza 40 na kila kitu basi mume wangu alibadilika, hakua akininyanyasa lakini alihama chumba, alianza kubwa bize na kazi zake na mambo aliyokua anayafanya ni kama alitaka niondoke ila anaogopa kuniambia. Kwakua sikua na kazi yoyote nilikua mtu wa kukaa nyumbani, kila siku nina mawazo, nlikua mtu wa kujifungia ndani nalia mpaka basi.

Siku moja mume wangu alichelewa kurudi nyumbani, mpaka saa tano usiku napiga simu haipokelewi. Nilihangaika ktuma meseji lakini hazijibiwi, nilijikuta nahangika chumbani, kuna kitu kikaniambia nikague vitu vyake, sijui nilikua natafuta nini lakini mara nilijikuta kwenye mabegi yake na vitu vyake vya kazini. Wakati naangalia nilikutana na Document flani, mume wangu alionekana kukutana na mwanasheria kutaka talaka.

Kuna makaratasi niliyaona ya mwanasheria kuhusu mambo ya talaka lakini niliona kwenye diary yake kuwa tangu mtoto anaanza kuumwa alishapanga kunaicha lakinia lisitisha baada ya mtoto kuumwa, ila baada ya mtoto kufariki basi alitaka kuendelea na mchakato wa talaka. Niliumia sana, nilijihisi kuchanganyikiwa, baada ya kuona vile mume wangu kaandika wkenye diary yake kuwa hawezi kuendelea kuishi na mimi, hahisi kama ananipenda tena nilijua kuwa kila kitu kimeisha.

Nilijikuta naingia kabatini, kuna dawa za marehemu mwanangu alikua akizitumia kwaajili yya kumpunguzia maumivu kwani wakati wa mwisho wmisho alikua katika maumivu makali sana, analia mpaka wakati mwingine tunalazimika kumchoma sindano za usingizi kwani hali ilikua mbaya. Nilichukua kila dawa niliyokutana nayo hapo nabugia na maji. Haikuchukua muda nilidonoka na kupoteza fahamu.

****
Baada ya mtoto wangu mdogo kufariki tuliona kuwa haitakua busra kumuach adada yake bweni, alikua bado mdogoi na alikua akisoma na Kaka yake, walizoeana, kwanza tulimhamisha shule kwakua kule alikua na marafiki wengi ambao wangeweza kumuulizia kuhusu Kaka yake, lakini pili alikau akikaa kutwa. Nadhani pia hicho ndiyo kitu kilichokua kinamzuia mume wangu kuchelewa kuniacha, mara nyingi mume wangu alikua akiwahi kurudi kwaajili ya mtoto na ingawa alikua anajua kuwa mimi na Baba yeke tumetengana lakini hatukutaka kumchanganya.

Hata mume wangu aliponihama chumba hakufanya waziwazi, bado mtoto alijua kuwa tuko pamoja, nilijitahidi sana kuficha huzuni yangu kwani kila akiniona nipo kimya alikaua nadhani kuwa naumia kwasababu ya mdogo wake.
“Mama kwani mimi sitoshi au kwakua mimi ni mtoto wakike ndiyo maana huna furaha na mimi?” Nakumuka siku moja aliniuliza, nilikua nimekaa seuleni naangalia TV nakumbuka ilikua ni usiku, alinaimbia nimsaidie kufanya homework na nilimuambia nitaenda kumsaiodia, lakini kutokana na mawazo nilijikuta nasahau, wakati huo mume wangu alikua bado hjajarudi na akili yangu ilikua inawaza kuwa yupo na mwanamke mwingine anachepuka.

Wakati nimekaa nilijikuta nawaza mpaka machozi yanatoka mwenyewe, sikujua kama mwanangu alikua pembeni akiniangalia, kwa zaidi ya nusu saa alikua ananiangalia na yeye akaanza kulia ndiyo nilishatuka.
“K3wanini unasema hivyo mwanangu?” Niimuuliza huku nikimuita, alikuja nikaw anampakata.
“Kwasababu tangu Kaka afariki basi naona hakuna anayejali, wewe kila siku unalia na Baba kila siku anachelewa, mimi naona ni bora niende shule tu maana huku kama hamnitaki?” Manani yake yaliniumiza sana kwani yalionekana kuwa na ukweli, tangu mwanangu mdogo kufariki mapenzi ndnai ya nyumba yalipungua.

Mume wangu alikua bize na mambo ayake, kila wakati ni yeye na kazi bila kukumbuka kuwa ana mtoto mwingine huku mimi nikiwa mtu wakulia tu na huzuni kila saa.
“Hapana usiseme hivyo mwanangu, mimi na Baba yako tunakupenda tena sana, ni maisha tu ya kazi, tunakupenda.” Nilimuambia, alikubali lakini kishingo upande. Nakumbuka siku ambayo nagundua kuwa Baba yeke anataka kuniacha nilikua nahuzuni sana, alinifuata kutaka kuongea na mimi lakini nilimuambia kuwa ninaumwa hivyo asinisumbue, ndiyo niliingia chumbani na kuanza kupekua vitu na kujua kuwa mume wangu ana mwanamke mwingine.

Kumbe mwanangu naye hakulala, baada ya kumuambia kuwa asinisumbue alikaa sebuleni kuangalia TV, alikaa mpaka kwenye sa anane hivi za usiku, usingizi ulimpitia hivyo wakati Baba yake anarudi anagonga alishtuka, Binti wa kazi ndiyo alienda kumfungulia Baba yake mlango, alipofika sebuleni alimkuta ndiyo anaamka. Baba yake alishangaa kumuona palemkwani haikua kawaida yake, ilikua ni siku ya shule lakini alikua bado hajalala. Baba yake alimuambia kuwa aende akalale lakini kabla ya kwenda alimuambia.

“Baba mimi nataka mnirudishe bweni sitaki tena kuendelea kukaa hapa.” Alimuambia Baba yake, Baba yake alishangaa, alirudi na kukaa huku akimuuliza kuwa kwanini alikua hataki kukaa pale nyumbani.
“Nyie hamnipendi, mlishaachana na sisi tulikua tumekubali, hata Dan (sio jina lake halisi) alishakubali kuwa mmeachana lakini baada ya dn kuanza kuumwa nyie mlirudiana kwaajili yake, nikajua mmerudiana tukawa na furaha lakini sasa hivi dan kafa hamtaki tena kuonge. Nyie hamtutaki ndiyo maana tangu zamani mnatupeleka bweni tu bila kutuuliza kama tunapenda au la, mnakaa wenyewe, sasa hivi wewe ni kukaa tu huko kazini na Mama kila siku ni mtu wa kulia tu anamlilia Dani ambaye amekufa wakati mimi nipo.

Mimi hapa kila siku nakua kama niko mwenyewe, sina familia, familia yangu alikua ni Kaka yangu Dan, amekufa namimi nikikaa hapa nitakufa, nirudishe shule yangu ya zamani nikakae bweni kwani kule nina marafikia mbao wananipenda kweli.” Aliongea huku akilia, maneno yake yalimchoma sana mume wangu, ni kama alizinduka nakujua kuwa alikua anaishi maisha yake mpaka kusahau kuwa alikua na watoto.

Mume wangu alimbembeleza mtoto na kumuahidi kubadilika, lakini Rahel (sio jina lake kamili) hakumsikiliza, alimuambia kwua yeye ameshakua mkubwa na anajua kuwa hataiwi hivyo hataki kuishi pale hyumbani. Mume wangu alimuambia akalale na atabadilika,a likuja chumbani ili kuongea na mimi lakini dniyo alinikuta nimelala nimepoteza fahamu. Aliangalia kitandani na kuona diary yake pamoja na vidonge, alitoka na kuita watu, walininyanyua na kunipeleka hospitalinia mbapo nililazwa na kuja kuzinduka asubuhi yake.

Pembeni yangu kulikua na askari kwani nilitaka kujiua. Baada ya kuzinduka mume wangu alikuja, hakuongea chochote lakini alionekna kukasirika ingawa alikua analazimika kucheka, nilikaa hospitalini kwa siku tatu, hali yangu ilikua nzuri na niliruhusiwa, mume wangu alishafanya michakato na kumaliza ishu ya Polisi hivyo nilirudi nyumbani. Niliporudi ndiyo alinielezea maongezi yake na Rachel na kuniambia kuwa hataki tena mambo ya talaka, hataki tena mambo ya kdanganyana na kjama nipo tayari basi turudiane na kama inawezekana basi tutafute mtoto mwingine.

Kwangu ilikua ni kama sherehe, sikutaka hata kuwaza mara mbili kuhusiana na hicho kitu, nilitaka kumuomba msamaha lakini alikataa na kuniambia ni wakati sasa tusamehe na kuachana na hayo mambo, aliniambia kuwa tutengeneze familia isiyo na visasi kwani mambo tunayoyafanya yanaweza kumathiri hata na mtoto. Nilikubaliana naye na kweli niliamua kubadiika na kusahau kila kitu kwani kwangu ilikua ni kama kupewa nafasi ya kuzaliwa upya sikutaka kuharibu tena, niliapa kubadilika na kuacha kumchunga mume wangu pamoja na kuendelea kumfanyia vituko.

***
Maisha yalibadilika, kila kitu kilikua sawa, ile Biashara mume wangu alikua ahaisimamia mpaka ikawa kubwa, kwakua sikua na kazi ni Mama wa nyumbani na suala la ajira lilikua ngumu mume wangu aliniambia niende dukani niwe nasimamia. Nilienda kweli na kila kitu kilikua sawa, mume wangu aliniacha dukani lakini alikua haniamini tena, alikua ni mtu wa wasiwasi na kila wakati alikua anakuja kunikagua, kwakifupi nilikua ni kama mfanyakazi.

Ingawa alikua ananihudumia kwa kila kitu lakini kila pesa iliyokua inaingia ilikua jinagawanya mara tatu, kuna ambayo ilibaki dukani kuendeleza duka, nyingine aliweka kwenye akaunti ya mtoto na nyingine alibaki nayo yeye, mimi alikua akinipa kila kitu ila hakuniruhusu nisimamie pesa. Nilikubalianan na hiyo hali kwani nilijua kuwa itakua ngumu kwake kuniamini tena, niliendelea kujishusha ingawa hakuwahi kunizungumzia kuhusu mambo yaliyopita, mume wangu ni ile aina ya wanaume ambao akikusamehe anasahau.

Mungu alijaalia nilipata ujauzito, hapo mapenzi yaliongezeka, mipango ilikua nikajifungulie nyumbani kwetu lakini wakati nakaribia kujifungua dada yangu alipata ajli hivyo nilikosa mtu wa kunihudumia, nakwakua hjali yangu ilikua ni mbaya kwani mimba zangu zinasumbuasumbua ilimlazimu mume wangu kumuita Dada yake kuja kunihudumia, si yule ambaye alinifumania, hapana mwingine ambaye alikua si daa wa tumbo moja bali ni mtoto wa Mama yake mdogo.

Yeye alikua amemaliza chuo ila alikua hana kazi, mwanzo mambo yalikua mazuri, alikua ananihudumia vizuri, alinikanda na kujitahidi kuhakikisha kuwa niko sawa. Lakini mambo yalibadilika baada ya kama miezi miwili, nimeshamaliza uzani, nilianza kuona anakua karibu sana na mume wangu, kwakua alikua hana kazi basi aliendelea kubaki pale wakati mume wangu akimtafutia kazi.

Nilianza kupata wasiwasi kwani muda mwingi walikua wanatumia pamoja, mume wangu al8impenda sana kwani alikua na akili na mara nyingi alikua anampa mawazo makubwa makubwa, kuna ushauri alimpa mume wangu wa kufungua kampuni ya kutoa mizigo bandarini, wazo lilikuja kuwa mume wangu anafanya Biashara, anatumia makampuni mengine kutoa mizigo kwanini asifungue kampuni yake na kuanza kufanya kazi hivyo kuchukua tenda hata za rafiki zake.

Mume wangu alikubali lile wazo, lakini shida ilikua kwenye kuandika wakurugenzi, mimi aliniweka akanipa hasilimia 20, yeye 20, watoto watu wawili akawapa kumi kumi na yule dada yake akampa asilimia 40. Niliumia sana kwani niliona kama kampa kiasi kikubwa wakati haajchangia chochote, mume wangu aliniambia kuwa yule ni mdogo wake na alichompa ni kiudogo kwani sisi kama familia tumechukua asilimia 60.

Pamoja na kuambiwa lakini nilikasirika, nilijihisi kama nimesalitiwa, mume wangu alimnunulia gari nayeye anidyo akaw amkurugenzi wa kampuni kwani mimi nilibaki dukani na mume wangu alikua na kazi yake. Alihama pale nyumbani baad aya kuona kuwa tunagombana lakini muda mwingi alikua anakuja na wanatumia muda mwingi kwenye ofisi ndogo ya mume wangu, nilijiona kama vile wananizunguka, kuna wivu niliupata mpaka kuna wakati nilihisi kuwa anatembea na mume wangu.

Nilianza kumfuatilai mume wanngu, kila sikua kairudi kazini nashiak simu yake, nikiona meseji albda wanachat hata kama ni kusalimiana basi naanza kukasirika, namuuliza kwanini mdua wmingi anachat na dada yake wakati mimi hachat na mimi. Ukiangalai chart zao hazikua za mapenzi lakini kulikua na utani mwingi, walikua kama marafiki wanaambiana vitu, hata vitu vikitopkea kwenye mitandao wifi yangu anamtumia mume wangu na mume wangu naye anamtumia.

Nilikua naumia sana tunagombana na mume wangu, ilifikia hatua akawa nafutya kila kitu, hapo pia tukawa tunagombana, nilihisi kuwa lazima kuna kitu ndiyo maana anfuta ili kuficha, mume wangua lipoona imekua shida basi alibadilsiha password kwenye simuyake, hapo ndiyo nilijikuta nakosa amani kabisa, niliamini kuwa lazima wanachepuka, nilainza kufuatilia kila mahali lakini sikuona chochote. Kutokana na kule kusumbuana wifi yangu alianza kundiaharau, mwanzo alikua ni mtu wa kunsalimia, ananipigai simu tunaongea lakini baadaye aliacha na hata kuja nyumbani ikawa mara moja moja.

Uvumilivu ulinishinda, niliamua kumfuata ofisini kwake na kumuambia kuwa natakaa aachane na mume wangu kwani ndoa yetu haina amanmi. Kwanza alinishangaa, lakini aliniambia maneno ambayo yalinichoma na kuniaminisha kuwa anatembea na mume wako.
“Yule ni Kaka yangu nmheshimu hivyo huo ujinga wako sitaki kuusikia, lakini hata kama ningekua natembea naye inakuhusu nini? Pambana na hali yako usiniletee shombo lako hapa, nimekuvumilia muda mrefu lakini naona unadhani mimi ni kama hao, kwakua Broo umempanda kichwani unafikiri kila mtu utamfanay hivyo hivyo, mambo yako kila mtu anajua hivyo acha kujifanya malaika. Kaka anakuheshimu lakini badala ya kukaautulie na ndoa yako basi kila siku ni kuhangaika kukizungusha! Tuliza makalio chini!”

Nilijisikia vibaya sana kutukanwa na yule binti kwangu alikua ni kama mtoto mdopgo, nilirudi nyumbani na kumuambia mume wangu, cha ajabu badala ya kuwa upande wangu basi alinigeukia.
“Nataka unisikilize wewe mwanamke, ulishanidhalilisha mara moja, ulishataka kuvunja ndoa ya dada yangu na kuharibu mahusiano ya familia yangu, ulisema shemeji yangu kakutongoza wakati hakuna kitu sasa hivi unasema kuwa natembea na mdogo wangu, acha kunidhalilisha, narudia acha kunidhalilisha, sijui una nini kila tukiwa na amani unataka tu kuharibu, chunga, sitaki kukuacha lakini kamwe sitaruhusu uharibu familia yangu!” Aliniambia.

Aliongea sana lakini sikumsikiliza, jinsi alivyokua anazidi kuongea niliona kama anamtetea ndugu yake, ndiyo alizidi kuniaminisha kuwa kweli anachepuka na mdogo wake. Nilijikuta sina amani nakua na kisiraniambacho siwezi kujizuia, kibaya zaidi nikuwa yule binti alianza tabia ya kumpost Kaka yake, kila wakitoka labda kwa chakula basi alikua akipost na kuweka caption kuonyesha kuwa alikua anampenda Kaka yake na kumshukuru, hali hiyo iliniumiza sana, nilimuambia mume wangu lakini hakujali, aliniambia niache kufuatilia mambo ya kijinga.

Hali ile ilinipa upweke, kila siku nilikua nagombana na mume wangu, akawa ni mtu wa kuchelewa kurudi nyumbani, akawa anakua bize sana na simu. Baada ya kuona vile niliona kama vile naachwa, ilikua nidfanye kitu, nilianza kumfuatilia yule Binti na kugundua kuwa alikua na mwanaume mwingine ambaye ni mpenzi wake wa muda mrefu tangu akiwa chuo, nilimtafuta yule Kaka na kumuambia kila kitu, nilimuambia kuwa mpenzi wake anatembea na mume wangu ambaye ni Kaka yake.

Nilimuonyesha baadhi ya meseji ambazo wifi yangua linijibu akinitukana kila nilipokua namshutumu kuwa anatembea na Kaka yake, katika meseji hakukataa zaidi alikua ananijibu ongea na mume wako acha kunisumbua mimi. Yule Kaka alionekana kuumia sana, aliniambia kuwa wapo kwenye mahusiano kwa zaidi ya miaka 6 na walikua na mipango mengi, ikiwa ni pamoja nakwenda kujitambulisha lakinihaoni kama anaweza kumuoa.

“Hapana, usimuache, nianchotaka ni wewe kuhakikisha kuwa unamshawishi ili aachane na mume wangu, yule ni Kaka yake na sitaki avunje ndoa yangu.” Nilimsihi sana yule kijana kuongea na mpenzi wake, alionekana kunielewa tukaagana. Jioni nilikua na amani kidogo, mume wangu alichelewa kidogo, aliporudi nilianza kwa kumuuliza kama alikua kwa w3ifi yangu, aliniangalia kwa hasira bila kunijibu, aliingia chumbani na mimi kimfuata.

Ila nakaribia tu kuingia mlangoni, mume wangu aliushikilia mlango, akaufunga kwa nguvu ukanipiga kichwani, nilidondoka mpaka chini, hakuishia hapo, alinifuiata na kuanza kunipiga, alinipiga sana huku akinitukana.
“Wewe mwanamke ni mshenzi sana, yaani umeniharibia maisha yangu, nimeishi wka madani, naishi kwa shida kwasbabau yako na sas ahivi unaharibu maisha ya ndugu zangu! Nitakuua hapa ili uniondokee kwani naona kama unataka kuniua kwa presha.” Aliongea huku akiwa kanishikilia chini ananikaba.
 
SIMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU--- SEHEMU YA SABA!

Mume wangu alinipiga sana kisha akaondoka, hakurudi tena nyumbani kwa siku mbili, alirudi akiwa yuko kawaida kabisa, hakuonekana kukasirika, ilikua kama hakuna kitu kilichotokea, mimi niliumia niliona kama kaniddharau, nilimuambia kuwa nimechoka nataka kuondoka kurudi kwetu. Aliniangalia kwa dharau na kuniambia.
“Unataka nikupe talaka moja kwa moja au unaharaka talaka itakufuata kwenu?” Nilimuangalia mume wangu bila kummaliza, sikutegemea anaweza kuniambia hivyo.

Sikua na namna zaidi ya kunyamaza, mume wangu tangu hapo alibadilika sana, alikua ni mtu wa kuchelewa kurudi nyumbani, nikiongea kidogo basi atanipiga, wakati huo nilikua na mtoto mdogo lakini alikua hajali kabis. Mara nyingi akirudi nyumbani anacheza na mtoto wake kwani mtoto mkubwa alikua shuleni, alikua anafanya mambo yake kimya kimya hanishirikishi, pale dukani duka ambalo alinikabidhi mimi alileta kijana, ingawa mimi nilikua kama bosi lakini yule kijana alikua akifanya karibu kila kitu na mimi kuwa kama mtazamaji.

Maisha yaliendelea hivyo hivyo, kila siku tunagombana na nikiongea sana nakua naishia kupigwa, ilifikia hatua ikawa kama ni jambo la kawaida kwa mimi kupigwa, nikilalamika sana ananiambia kuwa kama nimechoka basi nimuache niondoke kwni nitakua nimempunguzia matatizo. Hali iliendelea hivyo mimi nikivumilia, kila siku nilikua nikiamini kuwa hizo ni hasira na ipo siku mume wangu atabadilika, atanipenda kama mwanzo.

Siku moja nilikua dukani, kuna dada mmoja alikuja na gari, hakushuka lakinia liposimama tu mfanyakazi wangu wa dukani alimfuata, yule dada alifungua kioo cha gari na mfanyakazi wangu alimpa pesa kisha akaondoka. Baada ya kuondoka nilimbana mfanyakazi kuniambia yule ni nani na ni kwanini alimpa pesa, mwanzo alikataa lakini baadaye aliniambia kuwa ni Mama mdogho.

“Mama mdogo, kipipi? Ni ndugu yako?” Nilimuuiliza, alitabasamu na kisha kuongea kwa dharau.
“Ni Mama mdogo mke wa Baba, inamaana hujui wakati ameshampeleka mpaka kwao na wazazi wake wanataka amuoe yeye.” Alianza kuniambia, kusema kweli nilishangaa lakini yule kijana aliniambia tena kama ananikooa kwakua alikua ananichukia sana, mume wangu alikua na mwanamke mwingine, amempa moja ya nyumba yetu, ameshampeleka kwao na amemtambulisha huyo dada ana mimba yake anataka kumuoa.

Nilishangaa kwani tulikua na ndoa ya kanisani na mume wangu inakuaje anapeleka mwanamke mwingine nyumbani kwao. Nilipaniki, nilitaka kuongea na mume wangu lakini asingenisikiliza, nilimpigia simu Mama yake na kumuambia kila kitu huku nikimuuliza ni kwanini anataka kuoa mwanamke mwingine wakati mimi bado nina ndoa naye tena ya kanisani.
“Inamaana bado hajakuacha, wewe utakua umemloga mwanangu, haiwezekani kila siku tunamuambia aachane na wewe lakini hataki, kweli hawezi kuoa wanawake wawili hivyo ni lazima akuache, asije kutuaibisha.”

Mama mkwe wangu aliniambia, kwa muda mrefu nikigombana na mume wangu mimi ndiyo nilikua mtu wa kusema, ktu kidogo tu nilikua nampigia Mama yake na ndugu zake kuwaambia, ingawa walikua hawaniamini lakini anagalau walikua wananisikiliza na hata kumuita mume wangu kuongea naye, Mama yake ni mtu wa dini na hana majibu ya namna hiyo.

Nilijikuta nakata simu bila kuongea kitu kingine, niliona aibu na kujua kuwa kumbe kila mtu ameshanichoka. Mume wangu aliporudi aliongea kama kawaida, nilitaka kumuuliza lakini nilihofia sana, nilijua kuwa anaweza kuishia kunipiga na kama Mama yake anamuambia aniache basi nikipiga kelele anaweza kuniacha mazima.
“Tatizo ni yule mwanamke, nilazima nifanye kitu?” Niliwaza, hasira zilinipanda nikijua kuwa kumbe kuna mwanamke mwingine ananiharibia ndoa yangu, sikuona tena makosayangu nilijua kabisa kuwa huyo mwanamke ndiyo ambaye anataka kuniharibia ndoa yangu lakini mume wangua takua ananipenda.

Kesho yake kama kawaida nilienda dukani, niliamua kuwa karibu na yule kijana kwani alionekana anajua kila kitu na mume wangu alikua anamuamini. Nlichukua laki tano katika droo na kumpa.
“Ni zanin?” Aliniulzia kwa mshangao kwani haikua kawaida yangu kumpa hata shilingi kumi.
“Si nakupa, kwani kuna ubaya gani au hutaki pesa, kama hutaki nipe pesa zangu.” Nilimuambia nikitaka kumnyang’anya lakini alizing’ang’ania, akazichukua na kubaki nazo.

“Nataka uniambie kila kitu kuhusu huyo Malaya, najua mume wangu anaamini sana na anakupa wewe pesa hivyo ninachotaka namimi nakua nakupa na nataka kujua kila kitu.” Kwanza lisia kidogo, lakini aliniangalia na kuniuliza.
“Kweli unataka kujua?”
“Ndiyo nataka kuijua, huyo mwanamke anakaribia kunivunjia ndoa yangu unafikiri nitamuacha.” Nilimuambia huku nikionyesha macho ya msisitizo, aliniangalia kwa huruma kama vile anataka kuniambia kitu lakini anasita, nilimsihi aniambie ndipo aliniambia mambo ambayo yalizidi kuniumiza.

Yule mwanamke alikua na ujauzito wa mume wangu, mume wangu alikua anatumia muda mwingi kule na kuna mara nyingi tu mume wangu humchukua mtoto wetu na kwenda kule, lakini pia wanaenda shulke kumtembelea mtoto na hata mtoto wangu mdogo alishampeleka. Kusemakweli nilikasirika sana kuona kuwa mumewangu pamoja na kunisaliti lakini anatumia wanangu kuniumiza, nilijua ana hasira na mimi lakini kwanini awapeleke wanangu kwa huyo Malaya wake, kweli niliumia sana.

Lakini pia nyumba aliyokua anaishi yule dada ambayo nilijenga na mume wangu na kiwanja tulinunua wote alishabadilisha jina na kumpa yule dada, hapo nilikasirika zaidi, nilijua kabisa kuwa mume wangu anakaribia kuniacha na kama asiponiacha basi atachukua kila kitu. Baada ya kujua nilikaa kimya kwa wiki mbili, siku nyingine yule dada alikuja dukanai kabisa, alishuka kwenye gari na kuja dukani, alikuja kama vile anaingia duka la jirani lakini nadhani alikua kuniangalia.

Kweli kwa kumuangalia alikua ni mjamzito na mimba ilikua ni kubwa, nilimuangalia na kupata hasira, nilitamani kumvamia na kumpiga lakini niliona kuwa nitaharibu, mume wangu alikua kuwa nimefanya vurugu basi ingekua shida. Bnilinyamza lakini nikipanga cha kufanya, nilishapata hasira, moto umeniwaka na nilishaamua kuwa hakuna namna ambavyo nitaruhusu huyo mwanamke kuniharibia ndoa yangu.

“Mume wangu ananipenda, yuko na huyu malaya kwakua anajua tu sijabadilika, akijua nimebadilika basi atanirudia.” Nilijiambia, wakati nawaza yule dada alikuja dukani kwangu, akasimama mbele yangu, hakua akinunua kitu alikuaakiangalia, kwa kumuangalia tu nilijua kuwa kaja kunichora, mimi nilimcgangamkia na kujifanya sijui chochote, alijiongeelsha sana alipoona simsemeshi basi aliondoka, hakurudi kwenye gari balia lizunguka mpaka kwenye duka la jirani.

Baada ya kama dakika kumi hivi alirudi na kumuulizia mume wangu, nilimjibu kistaarabu na kumuambia kuwa siku za kazi mume wangu haji pale labda amtafute wkenye namba yake.
“Kama huna namba yake nikupa umpigie?” Nilimuuliza kimitego, kusema kweli nilikua na hasira lakini nilijikaza, sikutaka kuonekana mkosaji, sikutaka kuharibu mambo nilikua sijajua kuwa nitafanya nini lakini kila nikimuangalia yule dada nilikua najiambia kuwa lazima nitafanya kitu kibaya, hawezi kuniharibia ndoa yake.
“Ninayo sema nilitaka kuona tu duka letu.” Aliniambia, nilimsikia alichokisema, nilijua kasema makusudi uka letu ili kuniumiza kichwa lakini niliamua kuwa mpole, sikutaka kuharibu mambo mapema.

Nilinyamaza kimya, sikusema chochote, niliacha mpaka akaondoka, mfanyakazi wangu wkaati wote huo alikua anatetemeka, alijua mambo yataharibika lakini wapi.
“Nilijua mtapigana?” Aliniuliza baada ya yule dada kuondoka.
“Mimi? Nipigane kwaajili ya kile kinyago? Hapana, sijafikia hatua hiyo, watu wa namna hii unawaacha tu wajiaminishe kuwa wataolewa. Amekuja amekuta mali kajua zimepatikanaje, labda kama mimi siajzaliwa, labda kama mimi sikuzichuma hizi mali, ndiyoa taolewa, ataishia kuandikwa tu majina lakini hatachukua chochote!”

Nilifoka kwa hasira, nilikua nimekasirika kiasi kwamba nilikua nang’aya meno kwa hasira.
“Utafanya nini?” Aliniuliza, nilimuangalia nikacheka kisha nikamuambia.
“Nitafanya nini nini? Mimi siwezi kufanya kitu, hiyo ni kazi ya Mungu kudili na mashetani, mimi kazi yangu ni kupiga goti tu lakini najua Mungu hataruhusu mtoto wa zinaa kuzaliwa. Kusema kweli mpaka wakati huo sikua najua kitu chochote, nilikua na hasira tu ila nilijua kuwa siwezi kuruhusu yule mwanamke kuzaa.

****
Pamoja na kwamba sikufanya chochote lakini mume wangu alirudi nyumbani akiwa na hasira sana, alilalamika kuwa nimemfanyia mke wake vurugu, yaani alimuita mke, alinipiga sana na kuniambia kama naona kuwa ni shida yeye kuoa mwanamke mwingine basi nimuache niondoke zangu. Kusema kweli sikua tayari kwa hilo, nilichofanya ni kuomba msamaha ingawa sikujua kosa langu, hapo ndipo nilifungulia malngo wa maateso.

Mume wangu alikua analala nnje na kamaa kirudi nyumbani ni kwaajili ya kubadilisha nguo na kuondoka, anaacha nguo chafu mimi nakua napata kazi ya kufua tu. Lakini hata pale anapokua nyumbani basi ni mtu wa hasira, kuongea tu na huyo mwanamke na nikiongea kidogo ananitukana, alibadilika sana kiasi kwmaba kuna wakati nilitamani kuondoka ila sikulifruhusu hilo, nilishachuma vitu vingi na mume wangu sikua tayari kuondoka.

Niliwaza nini cha kufanya nikakosa jibu, kuna siku nilikua tu dukani, nilikua peke yangu kijana aliondoka kwani mume wangu alimpigia simu, hakuniambia alikokua anaenda lakini nilijua kwa huyo mwanamke. Nilikua na mawazo sana juu ya nini cha kufanya, wazo lilinijia kuwa kama yule dada asipozaa basi mume wangu anaweza kumuacha, niliwaza kuwa mume wangu labda alichepuka bahati mbaya kwani ananipenda lakini alipopata mimba basi ndiyo mapenzi yakakolewa.

Niliwaza kuhusu kutoa ile mimba lakini sikua najua ni namna gani ninaweza kufanya hivyo. Wakati nikiwa nimekaa apapita dada mmoja, alikua amevaa nguo za nesi, hapohapo wazo lilinijia kuwa kama nikitaka kumtoa mimba basi nimtumie nesi, sehemua mabayo anaenda kiliniki ili ampe dawa za kuhariobu mimba na mimba itoke. Niliwaza ni namna gani nitatekeleza wazo langu lakini ilikua ngumu sana, kwana ilikua ngumu kwa mimi kumpata huyo nesi lakini pili ilikua ngumu kwa huyo nesi kukubali kwani ni kama angepoteza kazi yake.

Lakini nililipenda wazo langu kwani mimi nsiingehusika kwa chochote, nilianza kufuatilia sehemu ambayo anaenda kiliniki, kwa bahati nzuti ilikua ni ahanati tu ya kawaida si hospitali kubwa kama nilivyodhani, nilifuatilia mpaka nikajua nesi anayemhusumia, nikajua familia yake na nikajua mpaka anaposali. Nilianza kua rafiki naye, nikimlaalamikia kuhusu ndoa yangu na kumuomba ushauri, tuliongea mambo mengi, mpaka tukashibana ndani ya wiki mbili tu.

Sikutaka kupoteza muda nilimuambia nia yangu kuwa huyo mwanamke anataka kuniharibia ndoa yangu hivyo nataka amtoe mimba. Tofauti na nilivyodhani kuwa labda atakataa na kutaka hata kunishtaki aliniambia kama ni kuharibu mimba yake basi nimpe milioni 5. Kwangu hazikua pesa nyingi ila tulipunguziana mpaka milioni 3, aliniambia anataka keshi na hataki mambo ya kutumiana.

Nilikubali na kumpa pesa yake, aliniambia atampa vidonge lakini mimi sikuaka kujua, nilichotaka ni kuhakikisha mimba inaharibika bila kumdhuru huyo dada wala yeye kuonekana kuwa kahusika kwani mambo yakiharibika basi nitakamatwa mimi. Kweli tilikubaliana nikampa pesa yake akaondoka, sikutaka mawasiliano naye tena, akanmiambia kuwa mambo yakikamilika atanijulisha kanisani lakini hataki mambo ya simu.

Kweli haikupita siku mbili, nakumbuka ulikua ni usiku wa manane, mimi nimelala na mume wangu, simu ya mume wangu iliita, wakati huo huyo mwanamke alikua na ujauzito wa miezi saba, mume wangu alipigiwa simu na kunyanyuka harakaharaka. Alionekana kupaniki, niliamka na kumuuliza ni nini kimetokea.
“Mke wangu kalazwa hospitalini, mimba imetoka nayeye yupo mahututi!” Aliniambia, nilijaribu kumododosa lakini alikasirka na kunisukuma akaondoka.

Nilipaniki kwani sikujua kilichokua kinaendelea, ni kweli nilisikia mimba imetoka lakini sikutaka kumuua yule dada.
“Nimemaliza, umesikia mimba imetoka, nipo hospitalini hata yeye hali ni mbaya anaweza kufa wakati wowote.” Mesji iliingia kwenza niliogopa kujibu, namba nilikua naijua ni ya yule dada, ingawa nilishaifuta lakini nilishika namba ya mwisho, niliamua kumpigia akapokea lakinia alikua anaongea kwa sauti ya chini.
“Tuma meseji, nipo na watu ila kazi yako imeshaisha.” Aliniambia.

Niliana kutuma mesjei nyingi kumuuliza hali ya mgonjwa, nikimuambia kuwa mimi nimemuambia amtoe mimba si kumuua, alikua anajijibu kuwa imekua bahati mbaya dozi aliyompa ilikua kubwa na mambo mengine mengine. Tulichat sana baada ya muda aliacha kujibu meseji zangu na nilipompigia simu alikua hapatikani. Nilikua kwneye wakati mgumu sana nikitamani hata kwenda hospitalini kujua, mume wangu alikua hapokei simu zangu.

Nilimpigia kijana wadukani aliniambia kuwa hajui chochote, naye alijaribu kumpigia mume wangu lakini alikua hapokei. Kusema kwli nilishindwa kulala, nilijisikia vibaya na kuanza kuwaza nimefanya nini, nilijuta kwanini nsingemuacha azae. Asubuhi mume wangua likuja, alikua kaongozana na Dada yake, aliingia ndani, alionekana kuchoka sana, alikaa kwenye kochi na kuanza kulia, alilia sana, nilihisi kuna kitu kibaya, nilitamani kumfuata kumuuliza lakini miguu haikutembea, nilijihisi vibaya kwani mume wangu alionekana kuumia sana.
 
Mki'copy story za watu muwe mnaacknowledge. Acha na kataa igigisi kwani ukimtaja mtunzi na mwandishi wa kwanza kabla ya wewe kunakili ungemeguka???? Uzamani huo
 
Mki'copy story za watu muwe mnaacknowledge. Acha na kataa igigisi kwani ukimtaja mtunzi na mwandishi wa kwanza kabla ya wewe kunakili ungemeguka???? Uzamani huo

Tupe ushahidi ndugu au laa tukuone kuwa una majungu
 
Mki'copy story za watu muwe mnaacknowledge. Acha na kataa igigisi kwani ukimtaja mtunzi na mwandishi wa kwanza kabla ya wewe kunakili ungemeguka???? Uzamani huo
aisee kwanza samahani sana nimesahau hilo mara nyingi hua nawekaga na mtunzihii nimekopi tu japo mtunzi sjamueka tusameheane ungeeleza tukiutaratibu kuliko hivi kumeguka huko vipi? 🤨🤔
 
Back
Top Bottom