SIMULIZI; NILIPOMUAMSHA SHETANI WA MUME WANGU--- SEHEMU YA SITA
Mume wangu aliondoka, hakunitafuta tena na wala hakupokea simu zangu kabisa, kibaya zaidi hakumuambia mtu yoyote, kila kitu alifanya kimya kimya, nilaimua kutafuta chumba kwaajili ya kukaa kwa muda kwani gharama za hoteli zikukua kubwa. Baada ya kama wiki tatu hivi mume wangua linitafuta, alishaanza kulipa ule mkopo, kuna kiwanja kingine ambacho alikua ancho alikua ndiyo kaanza ujenzi, alikiuza na kupatakama milioni 22, alilipa yote, lakini mambo bado hayakua sawa, alinitafuta ili nimfungulie duka.
Kuna pesa nyingine ambayo aliipata kama milioni 12, sijui alikopa wapi lakini kuna rafiki yake alimsharu kuwa afungue duka langu, aanze kuuza vitu asimamie awe analipa mkopo kidogo kidogo. Kwelia lifanya hivyo, alifuingua na kila kitu tukabadilisha majina yakawa yake, akawa analisimamia yeye na kulipa mkopo yeye. Nilimuomba msamaha lakini hakutaka kusikia chochote, aliniambia nimuache kwani kichwa chake hakijatulia.
Mume wangu alipambana,m ndani ya miezi nene alifanikiwa kulipa ule mkopo, alimaliza deni, alirudishiwa hati yake, aliniita na kuniambia kuwa ile hati nibadilishe majina na niandike majina ya watoto wetu, sikua na namna nilibadilisha, lakini bado hakutaka kurudiana na mimi. Kwa mara ya kwanza nilienda kanisani, tuliitwa ili kusuluhishwa, mume wangu aliongea yake na mimi kuongea yake, wasiwasi wake ni kuwa nilikua nimemsaliti hivyo hawezi kukaa na mwanamke mzinifu,.
Niliapoa na kuapa kuwa sijawahi kumsaliti lakini hakunisikiliza, kanisani mambo yalishindikana, ikafikia hatua kuwa kila akiitwa anagoma kwenda. Katika kipindi nilipokua mbali na mume wangu dniyo niligundua kuwa nampenda sana mume wangu, niligundua kuwa siwezi kuishi vila yeye, maisha yalikua ni ya shida sana, sio kama sikua na pesa, hapana, nilikua napenda na nilikua na kila kitu lakini sikua na mapenzi, kila siku nilikua ni mtu wa mawazo, kulia na kusononeka.
Nilitamani sana kuwa karibu na mume wangu lakini ilishindikana, afya yangu ilizizi kuwa mbaya, nikawa ni mtu wa mawazo, kazini siendii tena bila taarifa, nilijikuta nakua mpeke wkani hata ndugu walikua kama wamenitanga hasa baadaya kusikia mambo niliyokua nimeyafanya. Mwaka mmoja baadaye mwanangu mdogo alianza kuumwa, ilitokea hgafla tu alikutwa na uvimbe shingoni na baada ya kwenda kupimwa aligundulika kuwa ana Kansa.
Kwasabbau ya mtoto nmume wangu aliniambia nirudi nyumbani, nilirudi nyumbani tukaanza kuhangaika katika kumtibu mtoto. Ile hali ilitududsiha karibu, nilijua kabisa mume wangu atakaua amenisamehe, maisha yaliendelea na yalikua mazuri, nilijikuta naanza kuwa na furaha tena, nilijikuta naona kama nimepata nafasi nyingine. Ingawa mume wangu hakuwahi kuniambia kuwa amenisamehe au kutaka kulala na mimi lakini nili0na kabisa kuwa upendo wake umerudi, niliona kuwa bado ananipenda na hasa namnaalivyokua ananisaidia kulea watoto wetu.
Kwa bahai mbaya baada ya miezi nane mtoto wetu alifariki dunia, ilikua ni huzuni kubwa sana kwangu, nilikua kama mtu aliyechanganyikiwa kwani alikua ni mtoto wangu pekee wa kiume, niliumia sana kila siku nikawa ni mtu wa kulialial mume wangu alikua karibu sana na mimi, alikua ananijali lakini hakuwahi hata siku moja kuongelea suala la mapenzi, kila wakati nilipotaka kugusia hayo mambo au kuonyesha dalili kuwa ninataka tukutane kimwili alinikwepa, mwanzo ilikua ni sababu ya mtoto anaumwa lakini baadaye alinikwepa tu na kunuiiambia kuwa hayuko sawa.
Nilikua naumia sana kwnai nilikua nampenda na kila siku nilikua naishi naye, kilichokua kinaniumiza zaidi nikuwa baada ya mazishi ya mtoto kumaliza 40 na kila kitu basi mume wangu alibadilika, hakua akininyanyasa lakini alihama chumba, alianza kubwa bize na kazi zake na mambo aliyokua anayafanya ni kama alitaka niondoke ila anaogopa kuniambia. Kwakua sikua na kazi yoyote nilikua mtu wa kukaa nyumbani, kila siku nina mawazo, nlikua mtu wa kujifungia ndani nalia mpaka basi.
Siku moja mume wangu alichelewa kurudi nyumbani, mpaka saa tano usiku napiga simu haipokelewi. Nilihangaika ktuma meseji lakini hazijibiwi, nilijikuta nahangika chumbani, kuna kitu kikaniambia nikague vitu vyake, sijui nilikua natafuta nini lakini mara nilijikuta kwenye mabegi yake na vitu vyake vya kazini. Wakati naangalia nilikutana na Document flani, mume wangu alionekana kukutana na mwanasheria kutaka talaka.
Kuna makaratasi niliyaona ya mwanasheria kuhusu mambo ya talaka lakini niliona kwenye diary yake kuwa tangu mtoto anaanza kuumwa alishapanga kunaicha lakinia lisitisha baada ya mtoto kuumwa, ila baada ya mtoto kufariki basi alitaka kuendelea na mchakato wa talaka. Niliumia sana, nilijihisi kuchanganyikiwa, baada ya kuona vile mume wangu kaandika wkenye diary yake kuwa hawezi kuendelea kuishi na mimi, hahisi kama ananipenda tena nilijua kuwa kila kitu kimeisha.
Nilijikuta naingia kabatini, kuna dawa za marehemu mwanangu alikua akizitumia kwaajili yya kumpunguzia maumivu kwani wakati wa mwisho wmisho alikua katika maumivu makali sana, analia mpaka wakati mwingine tunalazimika kumchoma sindano za usingizi kwani hali ilikua mbaya. Nilichukua kila dawa niliyokutana nayo hapo nabugia na maji. Haikuchukua muda nilidonoka na kupoteza fahamu.
****
Baada ya mtoto wangu mdogo kufariki tuliona kuwa haitakua busra kumuach adada yake bweni, alikua bado mdogoi na alikua akisoma na Kaka yake, walizoeana, kwanza tulimhamisha shule kwakua kule alikua na marafiki wengi ambao wangeweza kumuulizia kuhusu Kaka yake, lakini pili alikau akikaa kutwa. Nadhani pia hicho ndiyo kitu kilichokua kinamzuia mume wangu kuchelewa kuniacha, mara nyingi mume wangu alikua akiwahi kurudi kwaajili ya mtoto na ingawa alikua anajua kuwa mimi na Baba yeke tumetengana lakini hatukutaka kumchanganya.
Hata mume wangu aliponihama chumba hakufanya waziwazi, bado mtoto alijua kuwa tuko pamoja, nilijitahidi sana kuficha huzuni yangu kwani kila akiniona nipo kimya alikaua nadhani kuwa naumia kwasababu ya mdogo wake.
“Mama kwani mimi sitoshi au kwakua mimi ni mtoto wakike ndiyo maana huna furaha na mimi?” Nakumuka siku moja aliniuliza, nilikua nimekaa seuleni naangalia TV nakumbuka ilikua ni usiku, alinaimbia nimsaidie kufanya homework na nilimuambia nitaenda kumsaiodia, lakini kutokana na mawazo nilijikuta nasahau, wakati huo mume wangu alikua bado hjajarudi na akili yangu ilikua inawaza kuwa yupo na mwanamke mwingine anachepuka.
Wakati nimekaa nilijikuta nawaza mpaka machozi yanatoka mwenyewe, sikujua kama mwanangu alikua pembeni akiniangalia, kwa zaidi ya nusu saa alikua ananiangalia na yeye akaanza kulia ndiyo nilishatuka.
“K3wanini unasema hivyo mwanangu?” Niimuuliza huku nikimuita, alikuja nikaw anampakata.
“Kwasababu tangu Kaka afariki basi naona hakuna anayejali, wewe kila siku unalia na Baba kila siku anachelewa, mimi naona ni bora niende shule tu maana huku kama hamnitaki?” Manani yake yaliniumiza sana kwani yalionekana kuwa na ukweli, tangu mwanangu mdogo kufariki mapenzi ndnai ya nyumba yalipungua.
Mume wangu alikua bize na mambo ayake, kila wakati ni yeye na kazi bila kukumbuka kuwa ana mtoto mwingine huku mimi nikiwa mtu wakulia tu na huzuni kila saa.
“Hapana usiseme hivyo mwanangu, mimi na Baba yako tunakupenda tena sana, ni maisha tu ya kazi, tunakupenda.” Nilimuambia, alikubali lakini kishingo upande. Nakumbuka siku ambayo nagundua kuwa Baba yeke anataka kuniacha nilikua nahuzuni sana, alinifuata kutaka kuongea na mimi lakini nilimuambia kuwa ninaumwa hivyo asinisumbue, ndiyo niliingia chumbani na kuanza kupekua vitu na kujua kuwa mume wangu ana mwanamke mwingine.
Kumbe mwanangu naye hakulala, baada ya kumuambia kuwa asinisumbue alikaa sebuleni kuangalia TV, alikaa mpaka kwenye sa anane hivi za usiku, usingizi ulimpitia hivyo wakati Baba yake anarudi anagonga alishtuka, Binti wa kazi ndiyo alienda kumfungulia Baba yake mlango, alipofika sebuleni alimkuta ndiyo anaamka. Baba yake alishangaa kumuona palemkwani haikua kawaida yake, ilikua ni siku ya shule lakini alikua bado hajalala. Baba yake alimuambia kuwa aende akalale lakini kabla ya kwenda alimuambia.
“Baba mimi nataka mnirudishe bweni sitaki tena kuendelea kukaa hapa.” Alimuambia Baba yake, Baba yake alishangaa, alirudi na kukaa huku akimuuliza kuwa kwanini alikua hataki kukaa pale nyumbani.
“Nyie hamnipendi, mlishaachana na sisi tulikua tumekubali, hata Dan (sio jina lake halisi) alishakubali kuwa mmeachana lakini baada ya dn kuanza kuumwa nyie mlirudiana kwaajili yake, nikajua mmerudiana tukawa na furaha lakini sasa hivi dan kafa hamtaki tena kuonge. Nyie hamtutaki ndiyo maana tangu zamani mnatupeleka bweni tu bila kutuuliza kama tunapenda au la, mnakaa wenyewe, sasa hivi wewe ni kukaa tu huko kazini na Mama kila siku ni mtu wa kulia tu anamlilia Dani ambaye amekufa wakati mimi nipo.
Mimi hapa kila siku nakua kama niko mwenyewe, sina familia, familia yangu alikua ni Kaka yangu Dan, amekufa namimi nikikaa hapa nitakufa, nirudishe shule yangu ya zamani nikakae bweni kwani kule nina marafikia mbao wananipenda kweli.” Aliongea huku akilia, maneno yake yalimchoma sana mume wangu, ni kama alizinduka nakujua kuwa alikua anaishi maisha yake mpaka kusahau kuwa alikua na watoto.
Mume wangu alimbembeleza mtoto na kumuahidi kubadilika, lakini Rahel (sio jina lake kamili) hakumsikiliza, alimuambia kwua yeye ameshakua mkubwa na anajua kuwa hataiwi hivyo hataki kuishi pale hyumbani. Mume wangu alimuambia akalale na atabadilika,a likuja chumbani ili kuongea na mimi lakini dniyo alinikuta nimelala nimepoteza fahamu. Aliangalia kitandani na kuona diary yake pamoja na vidonge, alitoka na kuita watu, walininyanyua na kunipeleka hospitalinia mbapo nililazwa na kuja kuzinduka asubuhi yake.
Pembeni yangu kulikua na askari kwani nilitaka kujiua. Baada ya kuzinduka mume wangu alikuja, hakuongea chochote lakini alionekna kukasirika ingawa alikua analazimika kucheka, nilikaa hospitalini kwa siku tatu, hali yangu ilikua nzuri na niliruhusiwa, mume wangu alishafanya michakato na kumaliza ishu ya Polisi hivyo nilirudi nyumbani. Niliporudi ndiyo alinielezea maongezi yake na Rachel na kuniambia kuwa hataki tena mambo ya talaka, hataki tena mambo ya kdanganyana na kjama nipo tayari basi turudiane na kama inawezekana basi tutafute mtoto mwingine.
Kwangu ilikua ni kama sherehe, sikutaka hata kuwaza mara mbili kuhusiana na hicho kitu, nilitaka kumuomba msamaha lakini alikataa na kuniambia ni wakati sasa tusamehe na kuachana na hayo mambo, aliniambia kuwa tutengeneze familia isiyo na visasi kwani mambo tunayoyafanya yanaweza kumathiri hata na mtoto. Nilikubaliana naye na kweli niliamua kubadiika na kusahau kila kitu kwani kwangu ilikua ni kama kupewa nafasi ya kuzaliwa upya sikutaka kuharibu tena, niliapa kubadilika na kuacha kumchunga mume wangu pamoja na kuendelea kumfanyia vituko.
***
Maisha yalibadilika, kila kitu kilikua sawa, ile Biashara mume wangu alikua ahaisimamia mpaka ikawa kubwa, kwakua sikua na kazi ni Mama wa nyumbani na suala la ajira lilikua ngumu mume wangu aliniambia niende dukani niwe nasimamia. Nilienda kweli na kila kitu kilikua sawa, mume wangu aliniacha dukani lakini alikua haniamini tena, alikua ni mtu wa wasiwasi na kila wakati alikua anakuja kunikagua, kwakifupi nilikua ni kama mfanyakazi.
Ingawa alikua ananihudumia kwa kila kitu lakini kila pesa iliyokua inaingia ilikua jinagawanya mara tatu, kuna ambayo ilibaki dukani kuendeleza duka, nyingine aliweka kwenye akaunti ya mtoto na nyingine alibaki nayo yeye, mimi alikua akinipa kila kitu ila hakuniruhusu nisimamie pesa. Nilikubalianan na hiyo hali kwani nilijua kuwa itakua ngumu kwake kuniamini tena, niliendelea kujishusha ingawa hakuwahi kunizungumzia kuhusu mambo yaliyopita, mume wangu ni ile aina ya wanaume ambao akikusamehe anasahau.
Mungu alijaalia nilipata ujauzito, hapo mapenzi yaliongezeka, mipango ilikua nikajifungulie nyumbani kwetu lakini wakati nakaribia kujifungua dada yangu alipata ajli hivyo nilikosa mtu wa kunihudumia, nakwakua hjali yangu ilikua ni mbaya kwani mimba zangu zinasumbuasumbua ilimlazimu mume wangu kumuita Dada yake kuja kunihudumia, si yule ambaye alinifumania, hapana mwingine ambaye alikua si daa wa tumbo moja bali ni mtoto wa Mama yake mdogo.
Yeye alikua amemaliza chuo ila alikua hana kazi, mwanzo mambo yalikua mazuri, alikua ananihudumia vizuri, alinikanda na kujitahidi kuhakikisha kuwa niko sawa. Lakini mambo yalibadilika baada ya kama miezi miwili, nimeshamaliza uzani, nilianza kuona anakua karibu sana na mume wangu, kwakua alikua hana kazi basi aliendelea kubaki pale wakati mume wangu akimtafutia kazi.
Nilianza kupata wasiwasi kwani muda mwingi walikua wanatumia pamoja, mume wangu al8impenda sana kwani alikua na akili na mara nyingi alikua anampa mawazo makubwa makubwa, kuna ushauri alimpa mume wangu wa kufungua kampuni ya kutoa mizigo bandarini, wazo lilikuja kuwa mume wangu anafanya Biashara, anatumia makampuni mengine kutoa mizigo kwanini asifungue kampuni yake na kuanza kufanya kazi hivyo kuchukua tenda hata za rafiki zake.
Mume wangu alikubali lile wazo, lakini shida ilikua kwenye kuandika wakurugenzi, mimi aliniweka akanipa hasilimia 20, yeye 20, watoto watu wawili akawapa kumi kumi na yule dada yake akampa asilimia 40. Niliumia sana kwani niliona kama kampa kiasi kikubwa wakati haajchangia chochote, mume wangu aliniambia kuwa yule ni mdogo wake na alichompa ni kiudogo kwani sisi kama familia tumechukua asilimia 60.
Pamoja na kuambiwa lakini nilikasirika, nilijihisi kama nimesalitiwa, mume wangu alimnunulia gari nayeye anidyo akaw amkurugenzi wa kampuni kwani mimi nilibaki dukani na mume wangu alikua na kazi yake. Alihama pale nyumbani baad aya kuona kuwa tunagombana lakini muda mwingi alikua anakuja na wanatumia muda mwingi kwenye ofisi ndogo ya mume wangu, nilijiona kama vile wananizunguka, kuna wivu niliupata mpaka kuna wakati nilihisi kuwa anatembea na mume wangu.
Nilianza kumfuatilai mume wanngu, kila sikua kairudi kazini nashiak simu yake, nikiona meseji albda wanachat hata kama ni kusalimiana basi naanza kukasirika, namuuliza kwanini mdua wmingi anachat na dada yake wakati mimi hachat na mimi. Ukiangalai chart zao hazikua za mapenzi lakini kulikua na utani mwingi, walikua kama marafiki wanaambiana vitu, hata vitu vikitopkea kwenye mitandao wifi yangu anamtumia mume wangu na mume wangu naye anamtumia.
Nilikua naumia sana tunagombana na mume wangu, ilifikia hatua akawa nafutya kila kitu, hapo pia tukawa tunagombana, nilihisi kuwa lazima kuna kitu ndiyo maana anfuta ili kuficha, mume wangua lipoona imekua shida basi alibadilsiha password kwenye simuyake, hapo ndiyo nilijikuta nakosa amani kabisa, niliamini kuwa lazima wanachepuka, nilainza kufuatilia kila mahali lakini sikuona chochote. Kutokana na kule kusumbuana wifi yangu alianza kundiaharau, mwanzo alikua ni mtu wa kunsalimia, ananipigai simu tunaongea lakini baadaye aliacha na hata kuja nyumbani ikawa mara moja moja.
Uvumilivu ulinishinda, niliamua kumfuata ofisini kwake na kumuambia kuwa natakaa aachane na mume wangu kwani ndoa yetu haina amanmi. Kwanza alinishangaa, lakini aliniambia maneno ambayo yalinichoma na kuniaminisha kuwa anatembea na mume wako.
“Yule ni Kaka yangu nmheshimu hivyo huo ujinga wako sitaki kuusikia, lakini hata kama ningekua natembea naye inakuhusu nini? Pambana na hali yako usiniletee shombo lako hapa, nimekuvumilia muda mrefu lakini naona unadhani mimi ni kama hao, kwakua Broo umempanda kichwani unafikiri kila mtu utamfanay hivyo hivyo, mambo yako kila mtu anajua hivyo acha kujifanya malaika. Kaka anakuheshimu lakini badala ya kukaautulie na ndoa yako basi kila siku ni kuhangaika kukizungusha! Tuliza makalio chini!”
Nilijisikia vibaya sana kutukanwa na yule binti kwangu alikua ni kama mtoto mdopgo, nilirudi nyumbani na kumuambia mume wangu, cha ajabu badala ya kuwa upande wangu basi alinigeukia.
“Nataka unisikilize wewe mwanamke, ulishanidhalilisha mara moja, ulishataka kuvunja ndoa ya dada yangu na kuharibu mahusiano ya familia yangu, ulisema shemeji yangu kakutongoza wakati hakuna kitu sasa hivi unasema kuwa natembea na mdogo wangu, acha kunidhalilisha, narudia acha kunidhalilisha, sijui una nini kila tukiwa na amani unataka tu kuharibu, chunga, sitaki kukuacha lakini kamwe sitaruhusu uharibu familia yangu!” Aliniambia.
Aliongea sana lakini sikumsikiliza, jinsi alivyokua anazidi kuongea niliona kama anamtetea ndugu yake, ndiyo alizidi kuniaminisha kuwa kweli anachepuka na mdogo wake. Nilijikuta sina amani nakua na kisiraniambacho siwezi kujizuia, kibaya zaidi nikuwa yule binti alianza tabia ya kumpost Kaka yake, kila wakitoka labda kwa chakula basi alikua akipost na kuweka caption kuonyesha kuwa alikua anampenda Kaka yake na kumshukuru, hali hiyo iliniumiza sana, nilimuambia mume wangu lakini hakujali, aliniambia niache kufuatilia mambo ya kijinga.
Hali ile ilinipa upweke, kila siku nilikua nagombana na mume wangu, akawa ni mtu wa kuchelewa kurudi nyumbani, akawa anakua bize sana na simu. Baada ya kuona vile niliona kama vile naachwa, ilikua nidfanye kitu, nilianza kumfuatilia yule Binti na kugundua kuwa alikua na mwanaume mwingine ambaye ni mpenzi wake wa muda mrefu tangu akiwa chuo, nilimtafuta yule Kaka na kumuambia kila kitu, nilimuambia kuwa mpenzi wake anatembea na mume wangu ambaye ni Kaka yake.
Nilimuonyesha baadhi ya meseji ambazo wifi yangua linijibu akinitukana kila nilipokua namshutumu kuwa anatembea na Kaka yake, katika meseji hakukataa zaidi alikua ananijibu ongea na mume wako acha kunisumbua mimi. Yule Kaka alionekana kuumia sana, aliniambia kuwa wapo kwenye mahusiano kwa zaidi ya miaka 6 na walikua na mipango mengi, ikiwa ni pamoja nakwenda kujitambulisha lakinihaoni kama anaweza kumuoa.
“Hapana, usimuache, nianchotaka ni wewe kuhakikisha kuwa unamshawishi ili aachane na mume wangu, yule ni Kaka yake na sitaki avunje ndoa yangu.” Nilimsihi sana yule kijana kuongea na mpenzi wake, alionekana kunielewa tukaagana. Jioni nilikua na amani kidogo, mume wangu alichelewa kidogo, aliporudi nilianza kwa kumuuliza kama alikua kwa w3ifi yangu, aliniangalia kwa hasira bila kunijibu, aliingia chumbani na mimi kimfuata.
Ila nakaribia tu kuingia mlangoni, mume wangu aliushikilia mlango, akaufunga kwa nguvu ukanipiga kichwani, nilidondoka mpaka chini, hakuishia hapo, alinifuiata na kuanza kunipiga, alinipiga sana huku akinitukana.
“Wewe mwanamke ni mshenzi sana, yaani umeniharibia maisha yangu, nimeishi wka madani, naishi kwa shida kwasbabau yako na sas ahivi unaharibu maisha ya ndugu zangu! Nitakuua hapa ili uniondokee kwani naona kama unataka kuniua kwa presha.” Aliongea huku akiwa kanishikilia chini ananikaba.