Nilipokuwa mdogo nilikuwa na uwezo wa kufanya Miujiza

Nilipokuwa mdogo nilikuwa na uwezo wa kufanya Miujiza

Castle_Lite hapa kuna watu watajaa na utaanza kupiga mpunga😂😂😂😂

Sina huo uwezo sikuhizi 😂😂😂😂.

Kuna namna mwili ulikuwa una react kila nikinuia na nikiona umereact hivyo najua kabisa itatokea kweli.

Ila sasa kwa miaka mingi nikiwa naanza tu kunuia,
mwil unagoma sekund ile ile ya kwanza. Roho inakataa. Moyo unapoa na mind haifunguki.

kwahiyo kwa miaka ming sasa sijaweza fanikisha hata kunuia mazur juu yangu coz ya hiyo. Najikuta nikiomba Mungu naomba tu normal na sio kama kipind kile.

Ngoja ntarud kuwa msaf nikifika 40.
Kwa sasa dah! Bado kidogo 😎😎😎

Ntakuwa msaf ili nirudishe zile nguvu 😂😂😂🤣 au unanishaurije? win-one
 
Kilichotokea ukubwan ni kuwa mwili umeutia unajisi kwahy huo uwezo haiwezekan kukaa mahala pachafu

Mm nadhan hii Karama watu weng wanayo. Na ndio Hata waganga wa Kienyeji wamepewa.

Zile dawa wanazochanganya wananamna wanaziwazia mazur ili ziende kufanya kaz inayotakiwa.

Ndio maana kuna watu wanasema flan ana mkono wa Dawa na fulani hana.
Au yule mpaka akupe/akufanyie dawa na mkono wake ndio unapona.

Mfano babu wa Semunge/Loliondo
(Kikombe cha Babu).hakuwa mganga wa kienyeji . Aliwah kuwa Mchungaji KKKT, na akaja kuponyesha watu na Kikombe cha dawa za Kienyeji . Na anadai alioteshwa na Mungu .na Maelfu ya watu walipona.

Zingatia : Mchungaj na ameponyesha Maelfu ya watu na dawa za mizizi na sio Kuombea kwa Jina la Yesu.
 
kuanzia ulipo kua mdogo ?
Ndio
Nakumbuka wakati flani
Maeneo ya kwetu kule baridi kali kwa hiyo tunakulia jikoni
Si unajua mazingira ya jiko za vijijin
Nyumba na jiko vipo tofauti

So mama akawa na mgeni ndani na wadogo zangu ndani wanakula
Mi nikabaki jikoni na kulikua kuna baridi
Nikala kidogo tu nikapata hisia kali yaani kama mtu anakusimamisha nikabeba chakula na chai ile nafika mlangoni kuna mti wa mgunga ulikua nyuma ya jiko ulikua ushapekechwa na wadudu aisee ulishuka kwenye bati la jikon kama radi inavyolia ule mti ulilalia jiko na kuharibu vitu ndani sana

So sisahau lile tukio kwa kwel

Na mifano mingi midogo midogo
Naweza nikawa nimelala fofofo nikahisi kuna maji yamemwagika na labda sijayasikia yamemwagika ila najua tu yapo maji
Mimi nisipofua hiyo siku na wewe usifue maana lazima mvua inyeshe
Yaani napata hisia sana

Nilipata mdada mmoja...hakua hata na dalil mbaya
Ila moyo wangu ukaniambia huyu ni mchawi
Kumkagua aiseee ana hadi ungo
Kabla muheshimiwa flan ajapewa sumu niliota atapewa sumu
So nikamuadithia mama yangu
Hadi coment niliiweka kwenye ule uzi
Na alikuja kupewa
Vitu ni vingi ila huwa siweki record
 
Back
Top Bottom