Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,438
Kwa wale wanaosoma sana habari za wababe na watu waliokuwa na sifa zenye kuumiza miili na hisia wa hapa duniani, bila shaka wameshawahi kukutana na jina la Chico Marx. Huyu jamaa, ambaye alizaliwa mwaka 1891 na kufariki hapo mnamo mwaka 1961 alikuwa na makusudi mawili tu ya kuja kwake hapa duniani. Kwanza wanawake kwa fujo na pili, kamari kwa kufuru. Siku moja alifumaniwa na mkewe akimbusu mwanamke. Mkewe alipokuja juu, Marx alimwambia, "unapiga kelele bure, sikuwa ninambusu, nilikuwa namnong'oneza mdomoni……!"
I wasn't kissing her, I was whispering in her mouth
Ni utetezi mzuri eh…..!