Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
- Thread starter
- #21
yarabi toba! nshaambiwa nlichokula!
Ulichokula si pono,wala Nguruwe mnonoChakula nilichokula, nakisifia kitamu!
Nimekula bila hila, kimeniondoa hamu,
Cha jirani sitokula, changu chanitosha hamu,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Sikukipika kwa moto, kwani kimekwisha wiva,
Ndani kina jotojoto, chakula hicho si mbeva,
Si chakula cha watoto, si chakula cha mandava,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Nilijihisi nayeya, pale nikikirarua,
Pale nilipochoveya, kwenye mchuzi murua,
Nilihisi napepeya, utamu kunizingua,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Nilichokula si kuku, si ngombe wala si bata,
Msijeanza kushuku, majina mkaniita,
Wakijiji kala chuku, ametiliwa limbwata,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Nilichokula si embe, fenesi au nanasi,
Sio ugali wa sembe, au samaki mkisi,
Si tambi wala si pombe, msidhani nawatusi,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Nimekula kwa kuguna, nikala kikimya kimya,
Nkangata nkatafuna, na pia nikamungunya,
Mwenzenu nikajichana, miye ninawatambiya,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Chini nikabingirika, utamu kuninogeya,
Na jasho likanitoka, huku nikichekeleya,
Pumzi ikinitoka, kama ninaogeleya,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Sikitaki cha jirani, cha kwangu chatosheleza,
Kinanitosha shambani, na hata Uingereza,
Hata huko Marekani, changu tumbo chanijaza,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Nawauliza wenzangu, na wapishi majikoni,
Mmekula kama changu, chakula hiki ni nini,
Nawauliza Marangu, Kitete na Turiani,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Beti miye nazifunga, miye naondoka humu,
Meza yangu naipanga, nile chakula kitamu,
Komeo nimelifunga, sitaki katishwa hamu,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Chakula nilichokula, nakisifia kitamu!
Nimekula bila hila, kimeniondoa hamu,
Cha jirani sitokula, changu chanitosha hamu,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Sikukipika kwa moto, kwani kimekwisha wiva,
Ndani kina jotojoto, chakula hicho si mbeva,
Si chakula cha watoto, si chakula cha mandava,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Nilijihisi nayeya, pale nikikirarua,
Pale nilipochoveya, kwenye mchuzi murua,
Nilihisi napepeya, utamu kunizingua,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Nilichokula si kuku, si ngombe wala si bata,
Msijeanza kushuku, majina mkaniita,
Wakijiji kala chuku, ametiliwa limbwata,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Nilichokula si embe, fenesi au nanasi,
Sio ugali wa sembe, au samaki mkisi,
Si tambi wala si pombe, msidhani nawatusi,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Nimekula kwa kuguna, nikala kikimya kimya,
Nkangata nkatafuna, na pia nikamungunya,
Mwenzenu nikajichana, miye ninawatambiya,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Chini nikabingirika, utamu kuninogeya,
Na jasho likanitoka, huku nikichekeleya,
Pumzi ikinitoka, kama ninaogeleya,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Sikitaki cha jirani, cha kwangu chatosheleza,
Kinanitosha shambani, na hata Uingereza,
Hata huko Marekani, changu tumbo chanijaza,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Nawauliza wenzangu, na wapishi majikoni,
Mmekula kama changu, chakula hiki ni nini,
Nawauliza Marangu, Kitete na Turiani,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Beti miye nazifunga, miye naondoka humu,
Meza yangu naipanga, nile chakula kitamu,
Komeo nimelifunga, sitaki katishwa hamu,
Nilichokula kitamu, nilichokula nini?
Kaditama wa tamati, nimefika kiringeni
Tena nimevua shati, ninasubiri resheni
Ndugu nimejidhatiti, nikimege magegoni
Nataka msosi huo, nipe nami nifaidi.