davina
Kuondoka nyumbani SIO SULUHU, ni kuyakimbia matatizo.
Unachopaswa kufanya ni, kama wewe ni Mkristo, ninaamini ni hivyo, ni kwenda kwa Kiongozi wa Kanisa aliye karibu nawe. Mwite, aje nyumbani, awasikilize kila mmoja kwa wakati wake, kisha mkae kwa pamoja.
Mzungumzie matatizo yenu, muyakabili, mfanye maombi. Msameheane, muanze upya.
Kuna mambo ambayo mlipoanza maisha mlikuwa mnayafanya, lakini sasa hamyafanyi. Jiulize, kwa nini?
Mojawapo ya mambo ambayo hutokea kwenye familia nyingi - za Kikristo au Kiislam, au hata kwa wale walio katika imani tofauti - ni kuacha kumtumikia Mungu. Watu hawaendi kufanya Ibada, wanazembea, wanasema: Niko busy na maisha.
Kumbuka alivyoimba Bushoke: Hayo maisha yasije kukuchanganya, ukaabudu wengine ukamwacha Mola.
Nini maana yake? Kumwacha Mola ni nini?
Unapoacha kumtumikia Mungu, imani yako inashuka, Shetani anapata mwanya MKUBWA wa kukuingilia, kisha unapotoka. Unakosa woga mbele ya Mungu. Shetani anakupa imani ya uongo. Unajiona mwenye nguvu kumbe umeingia SHIMONI kwenye giza tororo! Hujijui. Unaanza kumdharau mumeo/mkeo. Unatamani wanawake/wanaume wasio wake/waume zako. Unazini. UMEKWISHA.
Lakini Mungu ni Mwema, kwani ni Mwingi wa Kusamehe. Kwa wale wote wenye imani au wasio na imani, wakiamua kutubu na kuungama kwa Mungu, husamehewa dhambi zao, ambazo hufutwa, nao huzaliwa upya.
Ukiondoka na kwenda nyumbani, Shetani ataukaza kabisa moyo wako. Huyo anayekuambia uondoke uende nyumbani HAMJUI MUNGU! Anakupotosha.
Kwani kuna binadam gani ASIYEKOSA? Jiulize: Unapokata tamaa kwa huyo mume wako, je, Mungu amekuvumilia wewe kwa makosa yako kwa muda gani?
Sikufahamu, lakini huu ndio naona kuwa ni ushauri bora kwako, kwani HAKUNA KINACHOSHINDIKANA kwa Mungu!
Ukae kwa amani, Mtumishi wa Mungu.
Nakutakia kila la heri kwenye ndoa yako. Mbarikiwe. Mumrejee Mungu na mdumu daima kwenye ndoa yenu takatifu.
Alichounganisha Mungu hapa duniani na mbinguni, asitengue binadamu!
Amina!