Kuna mdada mmoja nilikutana naye kwenye mgahawa Wa mama ntilie akiwa kama mpishi na muhudumu, alikua mrembo nikaona huyu akinikubali Na tukiendana, atanifaa for long term relationship even marriage if possible..na nlivomu-approach huyu dada sikujitutumua na kujifanya nina pesa.
Nikaanza kujifaragua kwake nkamshobokeea, nikaflirt naye, though sikumwambia nia yangu on the spot, na sikumwomba namba, ingawa yeye alijua Namaanisha nn, which brings me to third paragraph.
Siku iyo nimeenda kwenye mgahawa wake kula, mdada ananiuliza nafanya wapi kazi wakati sijawahi kukopa wala kumuomba chakula kwake, taa nyekundu Iliwaka kichwani kwangu, nikasema mapema hivi anauliza nafanya wapi kazi (kiuhalisia mm bodaboda), Kaniona danga au? Kwann asiniulize wazazi wangu, ukoo wangu, ndugu zangu, hobbies zangu, straight to the point akaniuliza nafanyia wapi kazi, nikamjibu kuwa ntamwambia siku nyingine.
Ghafla nilikata mazoea na huyo dada..Na mgahawani kwake sikwenda tena na plan ya mm kumtongoza niliihairisha maana nliona Hana hisia na mm, baadae atakuja nichuna pesa hlf asepe, sababu mapema yote anauliza nafanyia wapi kazi Ili aone atanipiga mizinga ya tshs ngapi.