Wana JF, niko njia panda juu ya mdada huyu

Jimmy De Lite

JF-Expert Member
Jun 10, 2019
635
2,305
Samahani wapendwa, Mimi siyo mwandishi mzuri Ila naomba mnielewe kwa chochote nitakacho kuwa nimeandika.

Kuna mwanadada nimekuwa na mahusiano naye toka mwezi wa kwanza,Naweza kusema mahusiano yetu yameanzia Facebook.

Huyu mdada mimi sikuwahi kumtongoza kwa sababu alikuwa akimpost mwanaume ambae alionekana ni kama mchumba/mpenzi wake.

Mara nyingi nilikuwa nacomment na kumsifia huyu Dada kutokana na uzuri wake huku rohoni nikiumia kila ninapoona akimpost yule jamaa wamekumbatiana wakiwa sehemu nzuri nzuri za starehe.

Kutokana na pigo na mwonekano wa huyu mwanadada nilikuwa najisemea kimoyo moyo kuwa Mimi siyo type yake kabisa, Hasa ukilinganisha na maisha yangu yalivyo.

Ikumbukwe huyu Dada toka kipindi tuwe marafiki fb hakuna aliyewahi kumtafuta mwenzie inbox (messenger), Mawasiliano yetu yalikuwa yanaishia kwenye comment pale. Naweza kusema huyu Dada hakuna siku niliwahi comment kwenye post zake akaacha kureply,kitu ambacho nilikuwa navutiwa naye.

Nakumbuka Mwez 1 alipost picha akiwa na jamaa yake, Kutokana na walivyokuwa wamependeza ilibidi tu nicomment hivi

''aah aisee wakubwa wenye hela wana faidi''

Isivyo kawaida yake hiyo comment hakujibu, nikaanza kuhisi ntakuwa nimemkera, nikataka nikaidelete ile comment ila nafsi ikagoma.

Kusema ukweli nilishinda siko sawa mana nilihisi atakuwa kakasirika sana, siku hiyo mida ya usiku nikiwa nimepumuzika nikapata wazo nikadelete ile comment

Kabla sijaenda kuifuta nikawa nimeona text imeingia messenger, kuchek hivi ni yule Dada,haikupita hata 2sec nikawa nimejibu ile text,Katika kuchat chat ndo akanambia kuwa hajapenda nilichocomment

Nikamwambia anisamehe,Akajibu usijali sisi binadamu wote ni Sawa,Pia haitoshi niko simple sana

Nakumbuka siku ile tulichat mpaka saa 6 usiku, akaniuliza nafanya kazi gani. Nikamjibu mishe ninazofanya, na yeye akanielezea vitu vyote vinavyomhusu mpaka familia yao yote na akawa ameniambia kuwa ana mchumba (yule anae mpost) na harusi yao ni mwez wa 10 mwaka huu.

Licha ya kuchat naye usiku huo lakini sikumwomba namba ya simu maana nilikuwa nishajiona kwake ni kama mbingu na Aridhi,In short Kwa huyu demu nilijiona sina thamani mbele yake,na kilichokuwa kinaniboa zaidi alikuwa ananiita mdogo wangu.

Ilibidi nimfanye kama rafiki tu basi.

Huyu Dada licha ya kuniambia kuwa ana mchumba wake Lakini alikuwa anapenda akiwa ana chat na mimi mara kwa mara,mara aingize masuala ya mapenzi mara hivi,Ikumbukwe muda wote huo tuna chat tu fb.

Nakumbuka mwezi wa pili mwaka huu ndo alinitumia namba yake ya simu,Alinambia amechoka kuchat fb so tuhamie offline,Nikamcheki tukawa tunachat sana,Mara aniite mpenz,nikawa nashangaa tu,akiwa amelala ananitumia sms tukalale wote mana anahisi baridi.

Baada ya kuona huyu demu anazidi kuniletea za kuleta ikabidi siku moja nijitoe fahamu,Nilimwomba tufanye game ya kirafiki siku moja,Daah huwez amini hiyo text aliisoma lakin hakujibu chochote mpaka inafika nusu saa haikujibiwa

Nikazima data nikalala,nilivyoamka asubuhi nikawasha data ili kucheki kama amejibu nikakuta holllaaa,nikasema potelea mbali siwez chat na demu ambaye sijui mwisho wake

Nikaingia kwenye contact list nikadelete namba yake,Haiwezekani asome text halafu aache kunijibu.

Zilipita kama siku mbili hivi ndio nikaona text yake cz namba yake nilikuwa naijua tarakimu mbili za mwisho,Ikabidi na mimi nimwoneshe jeuri

Alituma kama text tano za kulalamika why namchunia ndio kidume nikajibu nilikuwa busy,Hapo hapo demu yeye mwenyewe akaomba tukutane,Ikumbukwe muda wote huo mimi na yeye tulikuwa hatujawahi kukutana zaidi ya kutumiana picha na video call.

Mwezi wa 4 demu aliniomba niende kwao Singida,Nikamwambia labda tufanye mwezi 5 coz kuna mishe fulani nafanya mwezi wote wa 4,Akakubali japo kinyonge.

Hapa sasa naweza kusema tulikuwa ni kama wapenzi kabisa mpaka nakawa nahisi huyu Demu alinidang'anya yule siyo mchumba wake,Tulikuwa tunapigiana video call WhatsApp usiku akiwa uchi kabisa,Nikimwuliza,Hivi una mchumba Kweli? anakasirika,Ikabidi hayo ya yeye kuwa na mchumba nimwachie yeye, atajijua.

Bahati nzuri mwez 5 nikawa nimepata dili la kufuata gari la mzee mmoja Dar, Ieleweke mim hii pia ndio kazi yangu kusafirisha magari,Dar to Mwanza,Dar to Rwanda,Kongo,n,k

Nafanya hiyo kazi kama niko likizo lakini.

Tarehe 2 mwezi 5 mimi na yeye huyu demu ndio tulikutana naye kwa Mara ya kwanza uso kwa macho nikiwa nimetoka Dar na Harrier ya watu. Hakuwa na utofauti na picha zake wala video call zake,Ilibidi anipeleke mpaka kwao,kusema ukweli wana maisha mazuri sana hasa ukilinganisha na fala mimi. Pia ndo nikajua yeye ndo anasimamia biashara za mama yake hasa maduka ya vipodozi mawili na saloon pamoja na mgahawa mkubwa tu pale Singida.

Baada ya kumaliza kusalimia Ikabidi nimwambie nataka kuendelea na safari yangu kurudi Mwanza,akasema huwezi kwenda lazima ulale hapa,Daah kwa hiyo nilale hapa na haitoshi kanitambulisha kama rafiki,,nikajisemea kimoyomoyo hapa natoka kapa.

Ilivyofika mida ya saa moja kama na nusu demu akanambia twende ukapumuzike,nikamwuliza wapi,akasema wewe twende tu,Ikabidi tuingie kwenye gari akawa ananielekeza njia ya kupita mpaka tukafika lodge moj. Nikapaki gari tukaingia mpaka mapokezi then tukapewa funguo,Tumefika room sikutaka mambo mengi nilimvaa kama short ya umeme,Ikawa ndo Mara yetu ya kwanza kukutana kimwili (sex). Mida kama saa 6 Usiku akanambia nimpeleke nyumban kabla ya mama yake hajarudi. Ilibidi nifanye hvo then mim nikanyoosha moja kwa moja mpaka mwanza.

Huyu demu naweza sema toka tuanze kukutana mwezi wa 5 nimeshakutana naye zaid ya Mara 6 mana kila weekend lazima aje Mwanza,na kinachonishangaza zaidi amekuwa ni mtu wa wivu sana

Juzi kuna demu kacomment kwangu fb kuwa amenimiss,kamtukana sana,Ikabidi nimwambie yule ni classmate wangu na saivi yuko pale UDSM ni dent,nikamwomba asifikirie vingine,tukawa tumeelewana vizuri,Cha kushangaza tena zaidi amekuwa akiniambia kuwa nisije kumuacha

Mara ya kwanza nilikuwa nahisi hana mchumba labda ananiongopea tu, lakini huo ndo ukweli mwezi wa 10 ni harusi na vikao vishaanza,Pia akimpost mchumba wake kule fb unakuta pia marafiki na ndugu wana comment kuwa wameisubiri harusi yao kwa hamu mwezi wa kumi.

Tangu mimi na yeye tuanze mahusiano amewahi kunipost mara mbili kwa kusema mim ni rafiki yake,Hiyo mimi siyo mbaya ila huwa nabaki njia panda anaposema kuwa nisije kumsaliti na wakati anajua kabisa yeye anaolewa!!

Na anasema lazima tuzae Mtoto,Ukimwuliza tutazaaje Mtoto na wakati unaolewa,ananuna na kubadilika kabisa.

Ikumbukwe Huyu Demu kamaliza UDOM mwaka juzi.

Nimeanza kuwa na wasi wasi na huyu Demu ndio mana nimeamua kuja kuomba ushauri huku.
 
Ndoa za siku hizi. Ni bora unazaa na wanawake halafu unachukua watoto unalea. Usimsaliti kwani yeye hakusaliti? Tafuta wako ujipigie huyo manzi atakuingiza kwenye majaribu. Piga chini.
Msubiri mpaka atakapoolewa kisha punguza mawasiliano taratibu.

Nampa pole sana jamaa anayemuoa. Utakuta jamaa naye sishiki simu ya mke wangu. Matokeo yake unafikisha watoto 5 na wote wa jamaa. Umefikisha miaka 70 mwanamke anakuambia hawa watoto siyo wako. KIfo hicho ni bora ujue mapema kabisa mkeo ni mtu wa namna gani
 
Wanaume mnapenda kujipa stress jaman, hapo unajua kamtu kanamchumba nawewe umeingia soon utazama kabisa, halafu siku kakiolewa unaanza kulialia .

Huyo bibi ana uhuru na wewe kwasababu hayupo ndoani subir mwez Wa kumi utaleta mrejesho .Achana nae utaambulia maumivu.
 
Back
Top Bottom