Niijuavyo Freemasonry

Niijuavyo Freemasonry

Eiyer,

Mkuu, Asante sana,

Japo napata shida, sina hakika hadithi hii ni tafauti na niijuayo mm, ama ni sawa.

Nimrod alikuwa ni mpiganaji, aliekuwa na ambition za kuipanua empire yake, yy alikuwa ni mu ethiopia, katika harakat zake za kivita, ndipo alikutana na semiramis, mwanamke huyu alikuwa ni mwenyeji wa Urech, ambayo sasa inaitwa Uru wa kaldayo, Mwanamke huyu alikuwa ni malaya aliekuwa anamiliki danguro, na alikuwa anafanya kazi ya kuwapoza wanaume walokuja kujipumzisha hapo ktk huo mji.

Hapa ndipo semiramis alikutana na Nimrod, na moja ya masharti aliompa Nimrod ni kuwa ilikuwa ni lazima amuoe' na kwa kipindi kile ilikuwa haikubaliki kutawaliwa na Malaya.

Hapo ndipo uongo ukatungwa, kuwa semiramis alikuwa ni bikra, alietokea baharini, kuja kukutana na Nimrod ambaye ni Mungu jua. Hapo ndipo ikaibuka imani ya Unajimu na utabiri wa Nyota.

Imani hii ilijikita katika madai kuwa Shetani ndie mtawala wa haki, na muumba wa dunia, na Mungu alikuwa amemchakachua nafasi yake. Na ikatabiriwa kuwa atazaliwa mtoto ambae atakuja kuurudisha Utawala wa shetani kwa kumnyang'anya Mungu madaraka yote.

Hadithi hii ni ndefu kila napojaribu kuisamarise naacha mambo Muhimu.

Lakini nakumbuka, semiramis alikuja kuuliwa na mwanae kwa Upanga, tena ukatungwa uongo kwamba amepaa kwenda kwa Mume wake kumsaidia kutawala.

Habari hata google kuipata ni shida, kuna mambo mengi hapa yananichanganya, anaeifahamu hadithi hii vyema atukumbushe.

Nimrod ndie anaesemekana alisimika rasmi imani ya ki freemason duniani.
 
Last edited by a moderator:
Ishmael,

I have answered this Question thousand times,.In short ist like this ,yes we have failed then tell us where is the Plane ?.If U CANT THEN ALLOW ME TO CALL YOUR god AS ""THE GOD OF GAPS"",

Who appears only,when scientists fail to solve the problems.
 
Umeyajuaje yote hayo na wakati umesema wanafanya shughuli zao kwa siri sana, na most of their members ni watu matajiri na watu maarufu, so na wewe ni tajiri au maarufu?? maana tajiri hawezi kuwa na rafiki maskini.
by the way you have prove your poor thinking capacity by saying issues that u dont know.
hujaongelea kwa habari ya viapo wanavyoapishana huko au hilo haulijui tukufungue akili wewe pooir mind.
 
Umeyajuaje yote hayo na wakati umesema wanafanya shughuli zao kwa siri sana, na most of their members ni watu matajiri na watu maarufu, so na wewe ni tajiri au maarufu?? maana tajiri hawezi kuwa na rafiki maskini.
by the way you have prove your poor thinking capacity by saying issues that u dont know.
hujaongelea kwa habari ya viapo wanavyoapishana huko au hilo haulijui tukufungue akili wewe pooir mind.

Matusi na lugha za kejel havisaidii.Hapo ndo akili yako ilipofikia?
 
Noel 2014,

Nakujibu hapa chini kama ifuatavyo..
1.,kwa nn tunakufa?.
-Ili ujue kwa nn tunakufa lazima ujue maana ya neno kifo kwanza!.Sina shaka unajua ndo mana uko jukwaa hili.
-,.Kifo ni Natural,hakitegemea amri yoyote ile,na (kifo cha uzeeni)hakizuiliki kwa kuomba ama kwa miujiza yoyote ile,ispokuwa (kifo cha ghafla,mfano ajali,ugonjwa n.k) kinaepukika kwa njia mbali mbali! Kama vile matibabu(sayansi),ama tahadhali(ajali .nk).
Hakuna ushahidi wowote wa mtu ama watu aliomwomba mungu wasife na hawakufa.Kwa hiyo kifo ni Natural kama vile kuzaliwa.

-Kwa hiyo kwa jibu rahisi ,tunkufa sababu ni asili.Ndo hadithi yenu ile ya kwamba kifo ni moja ya adhabu baada ya Adam kula tunda haina Mashiko kwa maana inajichanganya.Maana anayejua mambo yote hata yajayo hawezi shindwa kujua kiumbe chake kitakula tunda,tofauti na Hpo kubaliana na mm kwamba Hata mungu hakujua kama watakula tunda.

2.Who set this Formula ?
-Hakuna kitu/mtu/Nguvu iliyoseti formula ya kifo/kufa.Ni asili kama nilivokujibu hapo juu(1).

3.Hivi kifo kisingekuwepo dunia ingekuwa vipi?
-Ndo mana nikakwambia mungu wako hausiki kabisa katika kupanga vifo.Kwa hiyo hilo swali mulize mungu wako je ingekuwaje kama Adam na hawa wasingekula tunda,hii dunia ingetosha population yote?.Hapo ndo ujue Bible ni . Hadithi za kutunga zilizopitwa na wakati.Kifo ni asili kwamba viumbe hai watazaliwa na baada ya muda watakufa hii ni formula na ipo tu wala haihitaji mwongozaji.

4.Wewe ungekuwa vipi?

-Hata sijui.
5.ukipishana na kichaa huwa unafanya nn?.
-Ukichaa ni hali tu ya akili kutokuwa katika hali sahihi.Cha kushangaza nyie huwa mnasema kazi ya mungu.Yaan mungu anayefurahia watu kuwa vichaa?aiseee !..Mtu akifanikiwa mnasema mungu kamjaalia,akiharibikiwa mnakaa kimya,naomb pia muwe mnasema mungu kamfilisi ama kamuadhibu.

6.Angalia unavoutumia ufaham wako vibaya!.
-Thibitisha kwamba mimi nautumia ufaham wangu vibaya!,bali wewe unautumia ufaham wako vizur.
Tofaut yangu mi na wewe ni kwamba we umejazwa uoga wa kisichokuwepo,na wewe ni small minded,mimi sio muoga na sikubali kuburuzwa kwa imani za kimapokea kama nyie.

Koran imejaa habar za maisha ya waarabu na sheria zao,Biblia imejaa masimulizi ya waizrael na yamaduni zao .nyie kitabu chenu kiko wapi?.Kitabu kinaitwa walaka kwa Wagaratia mtu kakikomalia utadhani kinasomeka walaka kwa wazaramo.,Mbona wao hawasomi vyetu mfano cha shaban Robert tu.?
 
Eiyer,

Mkuu Eiyer

Umewezaje kufanya utafiti na kujua mambo yote haya, lakini umeshindwa kutafuta ni namna gani watu wa Roma waliweza kukubaliana na Ukristo haraharaka baada ya kuelezwa kwamba habari za Yesu na Mama yake Maria ndio zile zile za Nimrodi na Mama yake na ukiongezea na Mungu Jua ndio Uungu wa hao watatu unakuwa umekamirika kama ulivyokamilika Uungu wa Utatu Mtakatifu????
 
mie kwa kunambia kuwa alikusanya mwili nakubali c ilibaki mifupa but viungo vya uzaz ndo nashndwa kukuelewa hapo how?
hv hakuelewa kama hv viungo huoza na kupotea kwa kujichanganya na udongo post vt vinavyo fikirika bhana unatuchanganya Eiyer
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Eiyer

Umewezaje kufanya utafiti na kujua mambo yote haya, lakini umeshindwa kutafuta ni namna gani watu wa Roma waliweza kukubaliana na Ukristo haraharaka baada ya kuelezwa kwamba habari za Yesu na Mama yake Maria ndio zile zile za Nimrodi na Mama yake na ukiongezea na Mungu Jua ndio Uungu wa hao watatu unakuwa umekamirika kama ulivyokamilika Uungu wa Utatu Mtakatifu????

Mkuu hapo kwa RED unamaanisha Utatu Mtakatifu wa Yesu, Maria na Mungu Baba? Hebu finyanga upya hoja hapo ili urudi kwenye tunachoamini yaani Baba,Mwana na Roho Mtakatifu.......

Kuna vitu ni kweli Kanisa lilikubali kuvifanya ambavyo sioni tatizo lake ambavyo vilikuwa vya kipagani lakini Kanisa likavigeuza ili kwa mfano ile siku ya jua iliyokuwa sikukuu kubwa sana kwa wapagani baada ya wao kuong'oka huwezi kuifuta tu siku iliyosheherekewa karne nyingi zaidi ya Kanisa kuifanya siku hiyo iwe siku ya kuzaliwa Yesu (Christmass) badala ya siku ya jua............

Siku hizi tunaita utamadunisho yaani kutumia utamaduni ule ule waliozoea watu wa jamii fulani kabla ya kumjiua Yesu na kuvifanya vitu vile vile (vinavyokubalika na Kanisa) katika ibada za Kanisa kwa mfano kupokea sadaka za mifugo au mazao badala ya fedha tu kama ilivyozoeleka..............
 
Mkuu Eiyer

Umewezaje kufanya utafiti na kujua mambo yote haya, lakini umeshindwa kutafuta ni namna gani watu wa Roma waliweza kukubaliana na Ukristo haraharaka baada ya kuelezwa kwamba habari za Yesu na Mama yake Maria ndio zile zile za Nimrodi na Mama yake
Una maana gani unaposema kuwa "ni zile zile"?

Zile zile zipi?
na ukiongezea na Mungu Jua ndio Uungu wa hao watatu unakuwa umekamirika kama ulivyokamilika Uungu wa Utatu Mtakatifu????
Unaonaje kuwa habari za Utatu wa Mungu na utatu wa kipagani kuwa zinafanana?

Hata kama zinafanana kwanini unadhani kuwa Utatu wa kwenye Ukristo ndio umetokea kwenye Upagani na sio kinyume chake?

Hivi ukitengeneza gari halafu nikaja kuiga nitakuwa nimetengeneza kopi au ni ile ile?

Niliwahi kukuambia kuwa niliwahi kupata makala moja tatizo nimeisahau website,nikiikumbuka nitakuwekea link,jamaa wanasema kuwa kuliwahi kuwepo na "mtu" aliyekuwa anadaiwa kuwa ni mwokozi wa watu na alikuwa na wafuasi 12 na alizaliwa na bikira,stori hii ni ya zamani kama miaka 10,000 iliyopita

Sasa sijui utasema kuwa na dhana nzima ya mwokozi nayo imetokea kwa wapagani au vipi

Ninachoweza kukushauri ni kuwa unatakiwa uiumize akili yako zaidi ya hapo ulipofikia ili uweze kuzijua mbinu za Shetani

Ni mjanja sana!
 
MTAZAMO,

Mkuu
Haya mambo ya utamadunisho ni kosa kubwa sana mbele ya neno la Mungu na Mungu Mwenyewe, Mark 7:7. Niko tight kidogo ama sivyo ningekuwekea Historical account kwa undani,Alichokiweka hapa Eiyer ni undisputed Historical Account ndio maana namshangaa with all this understanding ni kipi humfanya aendelee kukubaliana na Hoax ya Baba,Mwana na Roho Mtakatifu?

Yes. Utatu Mtakatifu ni Utamadunisho Pia Mkuu.
 
Last edited by a moderator:
mie kwa kunambia kuwa alikusanya mwili nakubali c ilibaki mifupa but viungo vya uzaz ndo nashndwa kukuelewa hapo how?
hv hakuelewa kama hv viungo huoza na kupotea kwa kujichanganya na udongo post vt vinavyo fikirika bhana unatuchanganya Eiyer

Sikuchanganyi bali unajichanganya mwenyewe

Hiyo stori niliyoiweka hapo,ukitakja kuitafakari kwa maendeleo yaliyopo sasa utaina kama ya kijinga hivi [and yes it's absurd] lakini unatakiwa ufikirie ni wakati gani haya yalikuwa yanatokea,jambo la kijinga kwenye hiyo story sio hilo la kukusanya viungo tu ni mengi

Lakini pia ujinga huu upo hadi leo na watu wanaendelea kufanywa wajinga tu!
 
Mkuu
Haya mambo ya utamadunisho ni kosa kubwa sana mbele ya neno la Mungu na Mungu Mwenyewe, Mark 7:7. Niko tight kidogo ama sivyo ningekuwekea Historical account kwa undani,Alichokiweka hapa Eiyer ni undisputed Historical Account ndio maana namshangaa with all this understanding ni kipi humfanya aendelee kukubaliana na Hoax ya Baba,Mwana na Roho Mtakatifu?

Yes. Utatu Mtakatifu ni Utamadunisho Pia Mkuu.

Don't worry,someday you will understand why .......
 
Eiyer,

Haya mambo tumeishayaongea sana hapa.
Nadhani kuna tatizo kubwa la kuchukulia kila issue independently, ni ngumu sana kuzungumzia kila kitu upya kila wakati kinapo resurface.

Ukiristo uliopelekwa Roma ulikuwa unazunguzia Mungu in duality, Converts wakawa wengi kiasi cha kutishia Ufalme kupinduka sababu ya kukosa fedha, ndio haraka sana habari za Maria na Yesu zikawa Spinned, BOOM, mungu akatengenezwa haraka haraka akawa ni yule yule wao ufalme ukaendelea.

Ntakuwapo jioni kwa mjadala zaidi, wakati huo niletee fungu linaloelezea utatu mtakatifu kabla ya kufa kwa Yesu na Kabla Injiri haijaubiliwa Roma.
 
Sikuchanganyi bali unajichanganya mwenyewe

Hiyo stori niliyoiweka hapo,ukitakja kuitafakari kwa maendeleo yaliyopo sasa utaina kama ya kijinga hivi [and yes it's absurd] lakini unatakiwa ufikirie ni wakati gani haya yalikuwa yanatokea,jambo la kijinga kwenye hiyo story sio hilo la kukusanya viungo tu ni mengi

Lakini pia ujinga huu upo hadi leo na watu wanaendelea kufanywa wajinga tu!

Alaa!!!!!
 
Noel 2014,

Nimrod sio muasisi wa imani ya imani ya Freemason kama unamaana kuwa imani ya Freemason ni imani ya kishetani au kipagani

Muasisi wa Uasi au upagani ni Shetani mwenyewe pale alipoendesha kampeni mbinguni ya kumuasi Mungu,hawa wengine ni waendelezaji tu,kampeni hiyo Shetani aliiendeleza Eden na baadae binadamu wa kwanza kuiendeleza ni Kain ambae inasemekana ndipo neno Freemason ililipopatinaka

Neno Freemason linamaana ya wajenzi huru,Kain na nduguye Abel waliagizwa na Mungu wajenge madhabahu kwaajili ya kumtolea Mungu sadaka,Mungu aliwaagiza namna ya kuijenga madhabahu hiyo,Abel alifanya kama Mungu alivyomuagiza lakini Kain yeye alijenga vile ambavyo yeye alitaka,yaani alitaka kuwa "free" au kwa lugha nyingine alitaka kuwa "mjenzi huru" na baada ya kufanya hivyo sadaka ya Abel ilikubaliwa na ya Kain ilikataliwa

Inadaiwa kuwa Freemason wanamuona Kain kama nabii au mtume wao kwakuwa ndio muasisi wa Wajenzi huru au Freemason kwa lugha ya Kiingereza,hawa wanaendeleza uasi uliofanyika kule mbinguni na ndio maana namba 13 ni namba takatifu sana kwao kwakuwa ni namba ya uasi

Ni namba ya uasi kwasababu zifuatazo

1;Namba 13 inawakilishwa na watu waliokuwa kwenye chumba ilipofanyika karamu ya mwisho kabla ya Yesu kusalitiwa,kulikuwa na Yesu pamoja na wafuasi wake 12 hivyo kufanya wawe 13,baada ya Yuda kuondoka na kwenda kufanya shauri na Mafarisayo,mule mdami aliwaacha wakiwa 12 na yeye ndie alikuwa wa 13,hii inamaana kuwa ayeye Yuda ndie alikuwa ameibeba namba 13

2;Namba kumi na tatu inakuja kuonekana tena kwenye uasi mwingine wa Shetani mbinguni baada ya kuwashawishi 1/3 ya malaika waliokuwa mbinguni,hiyo 1/3 ukiondoa alama ya / inakuwa imebaki 13,hawa watu wanaitazama kama namba muhimu sana kwao kwani ule uasi ulioanzia mbinguni bado wanaueneleza

3;Kuna wafalme ambao walipigana vita nyakati za mwano kabisa za historia ya binadamu hapa duniani na inaelezwa kwenye biblia kuwa ulipofika kwaka wa 13 waliasi [Mwanzo 14:4] haya matukio na mengine yanawafanya hawa watu waichukulie namba hii kuwa ya muhimu sana kwao,kuna namba nyingine lakini hii ina umuhimu wa kipekee

Kutokana na hayo unaweza tu kuona vile uasi ulikoanzia na wala Nimrod sio mwanzilishi wa hawa ndugu bali ni muendelezaji,ambae anaweza kuwa mwanzilishi kwa maana ya binadamu wa kwanza kufanya uasi mbele za Mungu ni Kain na ndi maana wanamuona kama mtume wao

Hata Yuda anakubalika sana kwa hawa watu pamoja na Albert Pike pamoja na Adam Weishapt,hawa wote ni watu maalum sana kwa hawa watu!
 
Sangarara,

Mkuu tuutendee haki huu uzi wa Free ideas

Tutakapoanza kujadili haya tutakuwa tunakwenda nje ya mada

Unaweza kuanzisha mada ambayo inazungumzia haya na tutajadili pamoja na tutawaalika na wengine na tutajifunza pamoja!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu tuutendee haki huu uzi wa Free ideas

Tutakapoanza kujadili haya tutakuwa tunakwenda nje ya mada

Unaweza kuanzisha mada ambayo inazungumzia haya na tutajadili pamoja na tutawaalika na wengine na tutajifunza pamoja!

Hivi unategemea nipate opportunity ya kumdeclare Mungu wa Kweli alafu niache sababu ntakuwa natoka nje ya Mada, wakati najua kabisa hata hii mada inapata nguvu kwa binaadamu kwa sababu ya kutomuabudu Mungu wa Kweli?
 
Back
Top Bottom