Kutokana na vyanzo mbali mbali vya habari inasemekana kuwa Semiramis alikuwa mama yake Nimrod na baadae walikuja kuishi kama mke na mume
Nimrod alikuwa ni mfalme wa Babeli na ufalme wake ulikuwa na utamnaduni tofauti na falme zingine,yeye ndie aliyeamua kujenga mnara mrefu sana ambao ulikuwa na malengo mawili
1;Kuzuia watu wa ufalme wake kufa na mafuriko au gharika kama itakuja kutokea tena
2;Kwenda kumfuata Mungu na kumhoji sababu ya kuleta gharika na kuuwa watu
Nimrodi alianzisha imani ya kuabudu sayari na nyota,umani hiyo ilikuwa sana wakati huo na ikafikia hadi kuwa kama imani ya ulimwengu kwa wakati huo
Babu yake Nimrod ambae ni mtoto wa Nuhu aliyeitwa Shem alikuja kumkamata na kumuua Nimrod na kuukatakata mwili wake vipande vipande na kuvisambaza maeneo yote ambayo kulikuwa na imani aliyoianzisha Nimrod na Shem aliagiza kuwa kama kutakuwa na mtu mwingine aliyekuwa anaifuata imani hiyo nae atafanywa kama Nimrod
Muda ulipita na Shem alikuja kufariki Dunia,baada ya kufariki Dunia mke wa Nimrod au mama yake kwa upande mwingine alikusanya mabaki ya mwili wa mumewe au mwanae ili akayazike upya,alifanikiwa kupata mwili wake wote lakini alishindwa kupata mabaki ya kiungo cha uzazi cha mumewe au mwanae
Baada ya kukikosa aliwaambia wafuasi wa imani hiyo kuwa Nimrod alkuwa amekwenda kwenye jua na ndiko alikokuwa anaishi na amekwenda na kiungo chake cha uzazi na alikuwa ametoa maagizo kuwa kuanzia wakati huo hicho kiungo kitakuwa ni alama ya imani yao,haikufahamika hasa mawazo hayo aliyatoa wapi lakini ndivyo alivyowaambia wafuasi wa Nimrod na kuanzia wakati huo kiungo hicho kikawa ni alama kubwa sana ya imani hiyo
Baadae walikuja kui design alama hiyo na kuwa na muonekano tofauti ili unsiweze kuonekana kiurahisi na kugunduliwa na watu
Leo kiungo au alama hiyo inaitwa Obelisk,unaweza kuona picha yake hapa chini
Hiyo ni obelisk iliyoko Washington
Baadae mabaki ya mwili wa Nimrod ulizikwa kwa taratibu zote za kiimani na baada ya muda kupita uliota mti kwenye kaburi la Nimrod na mama yake au mkewe alisema kuwa hiyo ilikuwa ni ishara ya Nimrod kuzaliwa upya na mama yake au mkewe aliagiza kuanzia siku hiyo mti huo utakuwa ni alama ya kuzaliwa upya Nimrod
Lakini pia mkewe aliagiza kuwa Nimrod amekuwa mungu na kuanzia wakati huo alitakiwa aabudiwe na ndivyo ilivyokuwa na alipewa jina na Baal,hivyo mti huo ambao umekuja kujulikana kama "christmass tree" leo hii ndio inasemekana uliota kwenye kaburi la Nimrod na ni ishara ya kuzaliwa upya
Mti wa Christmass
Semiramis alipotoa hayo maagizo alipotea kwa muda na kurudi akiwa mjamzito,alipoulizwa alikokuwa alisema kuwa alikuwa amemfuata mwanae au mumewe na ujauzito aliokuwa nao alikuwa amepewa na mumewe na alikuwa anakuja kumzaa mtoto ambae atakuwa mwokozi wa kizazi kile kutoka kwa watu waliokuwa wanawanyanyasa lakini zaidi atakuja kuwaokoa na wanyama wakali waliokuwa wanatishia uhai wa jamii ile ya Babeli
Kweli baada ya muda Semiramis alijifungua mtoto aliyepewa jina Tamuz na alipokua alikuja kuwa na tabia kama ya "baba" yake kwa kuwa muwindaji bora
Mtoto huyu alikuja kupata ajali mbaya iliyokuja kuyaondoa maisha yake pale alipokuja kujeruhiwa vibaya na nguruwe pori na kusababishiwa majeraha ambayo hakupona na alikuja kufariki,ile siku ambayo aliuwawa na nguruwe pori iliamriwa kutokuliwa nyama na ilisemwa kuwa nyama ya nguruwe pori na nguruwe yoyote yule kuwa haifai baada ya mnyama huyo kumuua aliyetarajiwa kuja kuwa kiongozi wa watu wa Babeli
Muda ulipita na Semiramis alikuja kuwaambia kuwa mwanae hakuwa amekufa bali alikuwa amemfuata baba yake huko alikokuwa na akawaambia wafuasi wake kuwa tangu siku hiyo atahesabika kuwa ni mtoto wa mungu wao na atakuwa akiabudiwa,aliagiza ia kuwa alama itakayokuwa inamuwakilisha mungu wao ambao ni Nimrod itakuwa ni jua
Baadae aliwaagiza kuwa alikuwa ameagizwa kumfuata mumewe siku sio nyingi na aliagiza kuwa atakapomfuata alama yake itakuwa ni mwezi,ulipita muda na alikuja kufariki na kuanzia hapo alikuwa akiabudiwa
Na hapo dipo ilipopatikana imani ya kopagani yenye utatu wa Nimrod,Semiramis na Tamuz,utatu huu ulikuwa una majina tofauti tofauti kila imani hiyo ilipokuwa inakwenda na kuota mizizi,mfano Misri walikuwa wanafahamika kama Isis,Horus na Osiris
Hiyo ndio historia fupi ya Nimrod na imani yake pamoja na Babeli
Historia hiyo ndio inaaminika kuwa ya kweli japokuwa kumekuwepo na historia zingine tfauti na hiyo,ili uweze kupata ukweli ni bora ukatafiti mwenyewe ili uujue ukweli
CC:
juve2002
Mkuu wa chuo Ntuzu Sangarara charminglady Kaunga Ablessed Kongosho King'ast Mtambuzi Ishmael MTAZAMO RGforever .......