Nifanyeje kuhusu ili?

Nifanyeje kuhusu ili?

Naamini mpo wazima wakubwa na wenzangu

Mie nina mpenzi wangu nipo nae kama mwaka sasa
Kilichonifanya niandike hapa mie sina usafiri so analazimika kila siku anipitie home anipeleke kazini na jioni hivyo hivyo anirudishe hom

Ukifika muda wa kurudi daily mpaka nimpigie simu ndipo atoke ofisini kwake aje anifate
Nisipopiga anaweza akanifata hata saa moja usiku.

Nakwazika nahisi sijui ananionaje labda bila yeye hom sirudi nimefikiria jioni niwe najijulia usafiri bila kumpigia kimya kimya tu akijashtuka namwambia mie nipo om,apa nitakuwa nakosea kweli?

Sasa unataka aje hapo akusubiri ndio uone raha? Elewa inachukua muda gani kwa wastani hadi afike hapo then mpigie muda kabla kidogo. Hata mimi sipendelei nifike then nianze kusubiri hadi mtu atoke. Ni kujipanga tu
 
Lol wacha tu basi nideke nikiwekwa ndan nayasahau hayaaaaaa

Kwa kudeka huko na lawama za kishamba nani aweke zigo ndani! Eti mpaka nimpigie simu, dah!

Hivi ulishawahi kuwa na zoezi la kuwa unamsubiria mtu kila siku mpaka amalize kazi zake wewe kweli? Ngoja tu.
 
nyie wadudu kazi kweli.......na yeye c yupo job....sasa unaona shida gani kumjuza umemaliza,,,, na umempata kweli huyo....bembeleza ndoa kabisa.....
 
bidada unless kama mida hyo unamsubiria unakuwa bado na kazi za kufanya subiri mana walau utaonekana mchapakazi au mnalipwa overtime sawa...otherwise kukaa kazi zishaisha hadi usiku mhhh, si upande usafiri mwingine..?
Ila ndo vile lifti za watu sheeda,..mi zishanishinda kusubiria ratiba ya mtu

Smtmz kazi zimeisha basi napiga miayo hadi aje aaagggr
 
Oaneni ikibidi muwe mnabadilishana nani ampitie mwenzie....siku ingine una drive wewe kumpitia yeye...mnarudi home

Daah Mungu akipenda smtmz unaambiwa naja masaa 2duu hili ni tatzo mkuu
 
  1. Kwani huyo ni mkeo/mmeo wa ndoa?
  2. hebu tenga dk 5 tu halafu fikiria maisha yako huko nyuma miaka 10 iliyopita uliendeshaje.
  3. yawezekana anatumia gia ya kukuchukua na kukurudisha ili akuchunge vizuri au afanye mambo yake vizuri. wewe akikumindi kwa sababu umeamua kurudi home mwambie wewe umenjichunga vizuri ndiyo maana kakukuta upo vizuri.

Na ndo kuchungwa kwenyewe huku,,
Mwanaume bila yy kuja om sijafika inabore sana
 
nyie wadudu kazi kweli.......na yeye c yupo job....sasa unaona shida gani kumjuza umemaliza,,,, na umempata kweli huyo....bembeleza ndoa kabisa.....

huna adabu hata ya kubipu kidogo hakuna mdudu anaeongea hata Kama ana Kosa hupaswi mwita mdudu mwenzio
 
Labda tungesikia na upande wa pili unasemaje ingekua jambo bora sana!
 
Tamthiliya za kifilipino zimewaharibu wengi,wale wanaigiza tu mama.Bora huyo mumeo mtarajiwa anakuja kukubeba wengine wakiwapigia wenziwao wanaambiwa mimi nimeshifika nyumbni panda daladala.
 
Duh! Inavyoonekana Mpenzi wako sio rafiki yako.

Anyways,usiwe na kijiba cha moyo bibie juu ya umiliki wake wa gari,hicho ndio kinakufanya uone kama ana kunyanyasa.Shemeji yetu anajikalisha mjini mpaka usiku yote kukusubiri wewe lakini bado unaona haitoshi.

Ni jukumu lako kumtaarifa ukisha maliza kazi,sio yeye aanze kukupigia kukuuliza kama upo tayari caz atakuwa anakupigia simu kila baada ya nusu saa after working hours halafu utaona kero.
 
Mimi binafsi Sijaona tatizo hapo!
Ungempigia mara kadhaa akawa anaacha kukufuata, ningeshawishika kuwa upande wako.
Huyo anakujari sana.
 
Back
Top Bottom