Nifanye nini tena labda mnishauri

Nifanye nini tena labda mnishauri

Status
Not open for further replies.
Achana nae na usimtafute wala kuhangaika nae. Usiogope kuingia kwenye uhusiano mpya ila safari hii kuwa mwangalifu zaidi na umpatie hisia zako mtu mwenye malengo uliyokusudia ambae ameonyesha kuyatimiza kwa vitendo na si kwa ahadi.
Ukitaka mwanaume akupende,hata kama umempatia mambo ya kikubwa,bado umwonyeshe kuwa unajithamini na si wa kutetereka au kushoboka sana. Onyesha kujielewa na kuwa na msimamo na sio kubehave kama mtu wa bei rahisi. Usimwonyeshe kumtegemea kupita kiasi,zingatia ratiba ya shughuli zako bila kumtengea muda yeye isipokuwa kama mmepanga muda wa kuwa pamoja.
Mtake ushauri katika shughuli unazofanya na akikupatia ushauri,onyesha kuufuata na umpatie matokeo.
Onyesha bidii katika kazi zako na ayaone matunda ya kile unachokifanya na kumwonyesha kuwa unathamini shughuli zako na malengo uliyojiwekea.
Punguza marafiki wa kiume ila usisite kupokea simu au kusalimia wanaume wanaokupigia au kukusalimia huku akiwapo.
Usijionyeshe kuwa mtu mwenye dharau au kumlinganisha na watu waliomzidi kipato au waliomzidi kwa namna yoyote kwa lengo la kumuumiza. Maana unaweza ukadhani ukimfanyia hivyo atakuona bab kubwa na kukuhonga sana ili usimkimbie. Ukweli ni kuwa wanaofanya hivyo ni wanaume wachache ambao ni wageni wa mapenzi au wenye nia ya kukutumia haraka na kuachana na wewe na wale wasiojiamini.
Akikuita mahali mwonane au akikutoa out, vaa na upendeze kwa namna inayoendana na tukio. Kama amekuita mwende beach,vaa nguo za casual lakini zenye heshima ambazo hazikufanyi uonekane kama mlupo au demu,bali uonekane ni msichana au mwanamke wake. Kama ni kwenye harusi,pigilia nguo smart sana na nywele uziset vyema na ikiwezekana tafiti hata rangi za ukumbi au sare ili usiwe out of place. Kama ni msibani, usivae suruali ya jeans au mini skirt yenye mpasuo. Vaa nguo ya heshima na uwe na angalau ka khanga na mtandio wa kufunika kichwa. Mfanye ajisikie vizuri umiwa nae.

Usiwe mtu wa kulalamikalalamika au kunung'unika kila mara au kususasusa bila sababu za msingi.
Jifunze kutabasamu ukiwa nae bila hata sababu. Mwonyeshe kuwa una furaha inayotoka ndani yako na siyo kununa na kuwa serious muda wote labda kuwe na jambo la msingi la kukufanya kuwa hivyo.
Kuwa na marafiki wanaojielewa na sio wale waluwalu au ambao wanaonekana dhahiri kuwa wamekata tamaa.
Onyesha ukomavu katika kutatua mambo na usipende kuhusisha watu wengine katika migogoro yenu. Sio mnagombana kidogo,tayari umewapigia marafiki zako au mmepanga kitu,tayari umeomba ushauri kwa mashosti zako.
Punguza mazoea na marafiki wa mwanaume ulienae. Usijenge maziea ya kuwapigia simu au kuwatafutatafuta, mwanaume wako atakutafsiri kuwa uko easy na pia hao marafiki zake ndio wanaokutathmini na kumshauri kama unafaa au lah.
Ukigundua anakucheat,tafuta ushahidi taratibu na ukithibitisha, mweleze na asipoonyesha dalili za kubadilika,mpige chini bila kujihoji mara mbili.
Wapende ndugu zake na wasiliana nao bila yeye kujua mradi alikutambulisha kwao labda kama halipendi hilo. Panga nao ratiba za kwenda sehemu kutembelea n.k bila kumhusisha. Hilo litakusaidia kumjua na pia wewe kujisogeza karibu na familia yake.
Mfanyie surprise kwa kumnunulia kitu ambacho hakutarajia bila kumjulisha kuwa unakusudia kufanya hivyo. Ambatanisha zawadi hiyo na ujumbe mzuri unaoelezea namna unavyompenda n.k
Usimfiche maswala kama ya kuwa na watoto au watu angalau wawili uliowahi kutoka nao kabla yake.
Jaribu kuzingatia haya na mahusiano yako yanaweza kukomaa na kuwa ya kudumu au ndoa maana wanaume wengi wasiooa wanaogopa mtu mwenye dalili za kuwaelemea kuanzia mwanzoni tu mwa uhusiano huku wao wakiwa hawako tayari kwa majukumu.
Pia ukimfanya mwanaume auone uhusiano wako na yeye kuwa burudani na kitu chenye kumfanya ajisikie vizuri, ni lazima atatafuta namna ya kukufanya uwe patna wake wa kudumu tofauti na pale unapokuwa chanzo cha yeye kukasirika,kuhuzunika, kukereka kila mara na kuchoka akili, ni lazima akukwepe au kukwambia live kuwa hakutaki.
Nimekueleza haya maana wengi wenu wanawake,huwa hamjui makosa mnayofanya na mnadhani watu wanawaacha bila sababu na kushangaa wanaoa watu mnaodhani mmewazidi.
Hata hivyo, wanaume wana preferences tofauti,wengine watachangia.
Ahsnte saaaaaaanaaaaaa.......
 
Usimpe mtu haraka haraka tu Wiki mbili kuwa muangalifu inaonekana pia ulimuonyesha uko desperate sana jiamini binti 23yrs ushakuwa mdada mkubwa tu usilie lie tena
Sawa
 
Nilikuwa single kwa muda mrefu sikuwa na imani na wakaka hata kidogo. Mwez jana nikakutana na mkaka mstaarabu na mwenye akili ya maisha alinivutia sana kwa maana alikuwa anahitaji mwanamke wa maisha halikadhalika mimi.

Nikajikuta nimezama kwa kipindi kifupi ndani ya wiki 2 nilijikuta nimemuamini

Ghafla tu akaacha kupokea simu zangu na kutojibu ujumbe
Sikukata tamaa nilimtafuta tena kwa upole sana maana sikujua kosa langu na hatukugombana

Duuuuh sikuamini text yake ya mwisho ilinihuzunisha saaaaanaaa "Its over..kwasasa siko tayari kuwa katika mahusiano"
Nawaza sijui nini nimemfanyia nakosa amani na naogopa kumsumbua zaid nahisi atanichukia.

Waswahili wanasema, "Penda mahali unapopendwa, mahali usipopendwa achana napo." Mimi nakushauri kubali hali halisi ya yote yaliyotokea na uendelee na maisha yako. Chukulia hilo tukio kama sehemu ya funzo ya mahusiano. Wakati ukiwa single jipe muda wa kutafakari na kujua wapi ulipokosea ili uweze kujirekebisha. Na zaidi ya yote sali sana na umuombe Mungu akuonyeshe mwanaume ambaye anakufaa, mwanaume ambaye atakupenda na kukuheshimu na sio mwanaume wa kukutumia na kukuacha pale anapomaliza haja zake kama toilet paper.
 
Waswahili wanasema, "Penda mahali unapopendwa, mahali usipopendwa achana napo." Mimi nakushauri kubali hali halisi ya yote yaliyotokea na uendelee na maisha yako. Chukulia hilo tukio kama sehemu ya funzo ya mahusiano. Wakati ukiwa single jipe muda wa kutafakari na kujua wapi ulipokosea ili uweze kujirekebisha. Na zaidi ya yote sali sana na umuombe Mungu akuonyeshe mwanaume ambaye anakufaa, mwanaume ambaye atakupenda na kukuheshimu na sio mwanaume wa kukutumia na kukuacha pale anapomaliza haja zake kama toilet paper.
Ahsante sana kwa ushaur kaka yangu......nitaufanyia kaz
 
...Mwez jana nikakutana na
mkaka mstaarabu na
mwenye akili ya
maisha...

ulikosea kujaji mapema na bado unaendelea kujaji makosa kama mwanzo. futa kabisa kichwani hayo maneno hapo juu kwenye blue! utakua umepiga hatua sana katika kulishinda hili jambo.
 
...Mwez jana nikakutana na
mkaka mstaarabu na
mwenye akili ya
maisha...

ulikosea kujaji mapema na bado unaendelea kujaji makosa kama mwanzo. futa kabisa kichwani hayo maneno hapo juu kwenye blue! utakua umepiga hatua sana katika kulishinda hili jambo.
Ni kweli.....Thank you
 
Duh ukisema mkaka mstaraabu naona ka unanisema mimi anyway turudi kwenye mada hapo mapenzi hamna tena manake wanaume huwa wananamaanishaga wanachosema, utapata mtu wako wa ukweli iko siku.
 
Duh ukisema mkaka mstaraabu naona ka unanisema mimi anyway turudi kwenye mada hapo mapenzi hamna tena manake wanaume huwa wananamaanishaga wanachosema, utapata mtu wako wa ukweli iko siku.
Ameeeeen
 
Nilikuwa single kwa muda mrefu sikuwa na imani na wakaka hata kidogo. Mwez jana nikakutana na mkaka mstaarabu na mwenye akili ya maisha alinivutia sana kwa maana alikuwa anahitaji mwanamke wa maisha halikadhalika mimi.

Nikajikuta nimezama kwa kipindi kifupi ndani ya wiki 2 nilijikuta nimemuamini

Ghafla tu akaacha kupokea simu zangu na kutojibu ujumbe
Sikukata tamaa nilimtafuta tena kwa upole sana maana sikujua kosa langu na hatukugombana

Duuuuh sikuamini text yake ya mwisho ilinihuzunisha saaaaanaaa "Its over..kwasasa siko tayari kuwa katika mahusiano"
Nawaza sijui nini nimemfanyia nakosa amani na naogopa kumsumbua zaid nahisi atanichukia.
Kwanza nikupe pole kwa mkasa uliokukuta / kukutokea.
Kwa ushauri wangu na mtazamo wangu.
Kuna kitu ambacho nataka nitambue toka kwako, kipindi mpo katika uhusiano wenu wiki 2.
1. Umewahi kuongea nae kitu chochote kuhusu wewe kwa undani.
2. Umewahi kuonesha hisia za karibu sana kipindi upo nae.

Kama ulimuonesha hisia zako mapema mno kuwa unahitaji kuwa nae katika uhusiano, basi hapa umefanya kosa kubwa,
Hata kama umependa mwanaume kiasi gani, kamwe usioneshe hisia zako mapema kuwa umempenda kwa dhati.

Mkiwa katika uhusiano kamwe usimueleze kila kitu kuhusu wewe, na jaribu asijue kila kitu kuhusu wewe,
Mpe muda zaidi ya miezi sita hata mwaka mzima, hiki ni kipindi ambacho wapenzi huanza kufahamiana baadhi ya mambo kwa kiasi Fulani,

Labda huenda huyu mwanaume alikutambua kila kitu chako na baadhi ya mambo yako na jinsi ulivyo mpa mchezo,
Amekuona mwanamke dhaifu,
Na huenda akafikiria kuwa unafanya umalaya, au akitokea mwanaume mwingine utashindwa kuwa na msimamo dhabiti, hicho alicho kifikiria.

Hapo ungetakiwa uanzishe mahusiano nae lakini usingeonesha hisia zako kwa ukaribu,
Halafu ungejaribu kuonesha umakini, msimamo, na mwelekeo katika mambo yako, hata angekuomba mchezo ungemkatalia na kusubiri baada ya miezi 6 hata mwaka ndio umpe hii ingesaidia kumfanya aamini kuwa upo makini hata kama umependa kwa kiasi gani?

CHA KUFANYA / JINSI YA KUMRUDISHA
mvumilie kwa muda kidogo takribani wiki 2 au hata mwezi 1.
Mfuate tena mweleze kuwa huna kosa na unahitaji uwepo wake, unahitaji ukaribu wake, mmbeleze mwambie ukweli atakuelewa,
Na usifanye makosa kwa kumnyenyekea sana na kumwendea kila wakati unamuomba mrudiane.
Mshawishi kwa kila neno na kila namna ikiwa na sababu / maelezo ya kujitosheleza akakuelewa na mkarudiana.

Endapo atakubali mrudiane.
Kamwe usirudie makosa uliyofanya,
Na pia jaribu kumchunguza pia Hutu mwanaume kama ana familia, ama uhusiano na mtu mwingine,

( pia unaweza kumchunguza hata kabla hujarudiana nae, kama ana mpenzi mwingine ama familia, ni chanzo kipi kilimfanya achukue uamuzi wa kusitisha mahusiano yenu )

Akikataa kurudiana nawe / ukiona hana muelekeo wa penzi lenu kurudi,
Usiogope wala usiumie sana,
Maana hizi ni moja ya changamoto katika mahusiano, kabla ya ndoa.

Cha msingi, mwambie ukweli na hujapendezwa na maamuzi aliyochukua,
Na kama ameamua iwe wewe kubaliana na matokeo cha msingi Fanya mambo mengine ya muhimu,
Ambayo yatakuweka bize,
Huku ukijaribu kusahau maumivu ya kuachwa na mtu umpendaye.

Kumbuka malipo ni duniani, lazima yatamkuta tu huyu mwanaume.

Usiwaze sana jaribu kusahau mahusiano kwa muda mfupi.
 
Nyie ndio waumiza miyoyo ya watu kabisaa nyinyi wanafki ampendeki pia na mchekea mtu ila u dont say that u dont love someone.... U pple ur hell
 
Kwanza nikupe pole kwa mkasa uliokukuta / kukutokea.
Kwa ushauri wangu na mtazamo wangu.
Kuna kitu ambacho nataka nitambue toka kwako, kipindi mpo katika uhusiano wenu wiki 2.
1. Umewahi kuongea nae kitu chochote kuhusu wewe kwa undani.
2. Umewahi kuonesha hisia za karibu sana kipindi upo nae.

Kama ulimuonesha hisia zako mapema mno kuwa unahitaji kuwa nae katika uhusiano, basi hapa umefanya kosa kubwa,
Hata kama umependa mwanaume kiasi gani, kamwe usioneshe hisia zako mapema kuwa umempenda kwa dhati.

Mkiwa katika uhusiano kamwe usimueleze kila kitu kuhusu wewe, na jaribu asijue kila kitu kuhusu wewe,
Mpe muda zaidi ya miezi sita hata mwaka mzima, hiki ni kipindi ambacho wapenzi huanza kufahamiana baadhi ya mambo kwa kiasi Fulani,

Labda huenda huyu mwanaume alikutambua kila kitu chako na baadhi ya mambo yako na jinsi ulivyo mpa mchezo,
Amekuona mwanamke dhaifu,
Na huenda akafikiria kuwa unafanya umalaya, au akitokea mwanaume mwingine utashindwa kuwa na msimamo dhabiti, hicho alicho kifikiria.

Hapo ungetakiwa uanzishe mahusiano nae lakini usingeonesha hisia zako kwa ukaribu,
Halafu ungejaribu kuonesha umakini, msimamo, na mwelekeo katika mambo yako, hata angekuomba mchezo ungemkatalia na kusubiri baada ya miezi 6 hata mwaka ndio umpe hii ingesaidia kumfanya aamini kuwa upo makini hata kama umependa kwa kiasi gani?

CHA KUFANYA / JINSI YA KUMRUDISHA
mvumilie kwa muda kidogo takribani wiki 2 au hata mwezi 1.
Mfuate tena mweleze kuwa huna kosa na unahitaji uwepo wake, unahitaji ukaribu wake, mmbeleze mwambie ukweli atakuelewa,
Na usifanye makosa kwa kumnyenyekea sana na kumwendea kila wakati unamuomba mrudiane.
Mshawishi kwa kila neno na kila namna ikiwa na sababu / maelezo ya kujitosheleza akakuelewa na mkarudiana.

Endapo atakubali mrudiane.
Kamwe usirudie makosa uliyofanya,
Na pia jaribu kumchunguza pia Hutu mwanaume kama ana familia, ama uhusiano na mtu mwingine,

( pia unaweza kumchunguza hata kabla hujarudiana nae, kama ana mpenzi mwingine ama familia, ni chanzo kipi kilimfanya achukue uamuzi wa kusitisha mahusiano yenu )

Akikataa kurudiana nawe / ukiona hana muelekeo wa penzi lenu kurudi,
Usiogope wala usiumie sana,
Maana hizi ni moja ya changamoto katika mahusiano, kabla ya ndoa.

Cha msingi, mwambie ukweli na hujapendezwa na maamuzi aliyochukua,
Na kama ameamua iwe wewe kubaliana na matokeo cha msingi Fanya mambo mengine ya muhimu,
Ambayo yatakuweka bize,
Huku ukijaribu kusahau maumivu ya kuachwa na mtu umpendaye.

Kumbuka malipo ni duniani, lazima yatamkuta tu huyu mwanaume.

Usiwaze sana jaribu kusahau mahusiano kwa muda mfupi.
Ahsnt sanaaa

Nimekuelew hakuna mfano
And I wil take ur words
 
Ahsnt sanaaa

Nimekuelew hakuna mfano
And I wil take it words
Usijali ni wajibu wa kila mwanadamu kumsaidia binadamu mwenzake kwa matatizo mbali mbali kulinda na uwezo wao na wa mwenyezi mungu pia........

Nakutakia maisha mema ya uhusiano huko utakapoenda, but kuwa makini tena sana.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom