Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

Seif anawaingiza kwenye mkenge, matatizo yake hayataonekana sasa hivi, as long as wako ndani ya Muungano! Wakitoka tu watajua kwamba wao si wamoja tena! Historia itawatafuna kisawasawa!

Haya maneno ya nyerere mnayapenda sana, hakuna kitachowatafuna, na kama ni hivyo si wabara mvunje muungano mbona mnang'agania nini?
 
Topical, hatujawazuia kujitawala, ila sisi bara hatuamui kimdadimdadi mambo makubwa kama kuwa nchi, kumbuka maalim seif hajamaliza mwaka tangu avue kanga na baibui la kike alilokuwa anavaa kujificha, hata hamjui kukaa? mnahaha tu? mmeungana basi fanyeni kazi ya maendeleo sio kuchokonoa kwengine kabla hamjawapatanisha vizuri wazanzibari na kuisafisha serikali iliyojaa wezi.
 
topical, hatujawazuia kujitawala, ila sisi bara hatuamui kimdadimdadi mambo makubwa kama kuwa nchi, kumbuka maalim seif hajamaliza mwaka tangu avue kanga na baibui la kike alilokuwa anavaa kujificha, hata hamjui kukaa? Mnahaha tu? Mmeungana basi fanyeni kazi ya maendeleo sio kuchokonoa kwengine kabla hamjawapatanisha vizuri wazanzibari na kuisafisha serikali iliyojaa wezi.

kuna akili hapa watu milioni 40 hatuwezi kujiendesha kwa kuunda nchi yetu ya tanganyika ??? Kwa nini tuendelee kuwalazimisha wazanzibari na mambo yao ??? Jinchi hili la tanganyika haliendi ila kwa kuwa zanzibar katika muungano huu ni uwenda wazimu ???? Labuda kuna ajenda nyengine ya kanisa
 
Wazanzibari huwa hatusemi kwa maneno tukiamuwa, sisi wanaume bwana, tukisema "yes" ndiyo inakuwa hivyo, tukisema "No" ndiyo hivyo hivyo haiwi, zanzibar ipi tunayoitaka, ikifika wakati wake, si mda mrefu tangu sasa, tutasema kwa vitendo, nadhani mnatutambuwa.
 
..upande mmoja unaweza kujitoa ktk muungano bila majadiliano au kuushirikisha upande wa pili.

..Zanzibar wana serikali,baraza la wawakilishi,vyombo vyake vya ulinzi na usalama, wanasubiri nini kujitoa ktk muungano?
 
..upande mmoja unaweza kujitoa ktk muungano bila majadiliano au kuushirikisha upande wa pili.

..Zanzibar wana serikali,baraza la wawakilishi,vyombo vyake vya ulinzi na usalama, wanasubiri nini kujitoa ktk muungano?

Usemayo ni kweli lakini mara nyingi hupelekea civil war....kuna njia ya kistaarabu ya majadiliano na kura ya maoni....hii ndio njia nzuri na nyepesi ya kupita...au tunapendelea damu imwagike kwanza kama Sudan halafu ndio ije referendum?
 
Wanaitaka nchi "yao" ya Zanzibar; Wanataka kurudia "utukufu wa Zanzibar" kwa kuwa hapa walipo sasa hawaoni manufaa "yoyote" kwa Zanzibar. Wanasema wanaitaka nchi yao waliyonyang'anywa na Wadanganyika (ati Watanganyika). Wanataka warudishiwe nchi yao waliyonyang'anywa na Nyerere na watu wa bara.

Ni Zanzibar ipi hiyo wanayoitaka?


  • Zanzibar ya historia ya kale (Zenj - nchi ya weusi?) ambayo ni zaidi ya visiwa vya Unguja na Pemba bali na mwambao wa Afrika ya Mashariki
  • Zanzibar ya Sultani(ambaye naye utawala wake ulizidi mipaka ya Unguja na Pemba)
  • Zanzibar ya Sultani chini ya Mwingereza
  • Zanzibar ya baada ya Uhuru na Sultani akiwa bado ni Mkuu wa Nchi na serikali ya Mseto
  • Zanzibar ya Mapinduzi kabla ya Muungano
  • Zanzibar "mpya" ambayo haijawahi kuwepo yaani ya baada ya muungano
Ni ipi hasa wanayoitaka? Ni ipi hasa Zanzibar "proper". Isije kuwa ni kama nchi ya ahadi ambayo iko katika fikra za watu tu lakini haijawahi kuwepo; yaani ile nchi imiminikayo maziwa na asali na kwamba watu wa bara na dunia nzima wanataka kuwanyang'anya Wazanzibari. Na labda hapa itabidi tulijibu swali pia kuwa Mzanzibari ni nani hasa?

Hapa panatakiwa Tanganyika tu. Mambo yote poa.:frusty:
 
Nonda said:
Usemayo ni kweli lakini mara nyingi hupelekea civil war....kuna njia ya kistaarabu ya majadiliano na kura ya maoni....hii ndio njia nzuri na nyepesi ya kupita...au tunapendelea damu imwagike kwanza kama Sudan halafu ndio ije referendum?

Nonda,

..u keep on invoking Southern Sudan time and again.

..kwa mtizamo wangu the case and the plight of former Southern Sudanese is quite different frm what is going on in Zanzibar.

..lini ulimuona msudani kusini akiongoza serikali ya Khartoum?

..ile serikali ya mpito ya Southern Sudan ilipatikana baada ya miaka 30++ ya mapigano na umwagaji damu.

..Zanzibar wana serikali yao tangu kuasisiwa kwa muungano wake na Tanganyika.

..Southern Sudan haikuwa dola/nchi iliyoungana na Sudan, bali ilikuwa sehemu ya Sudan.

..kama Zanzibar waliweza kuitisha kura ya maoni kuhusu suala la serikali ya umoja wa kitaifa, basi wanaweza kuitisha kura ya maoni kuhusu suala la muungano.

..hata suala la kujitoa kwenye muungano wanaweza kufanya hivyo kwasababu wao walikuwa ni nchi/dola kamili inayojitegemea.

..taasisi na vyombo vya kuiwezesha Zanzibar kujiondoa ktk muungano and allow for a smooth and peaceful transition zipo. sijui kwanini wa-Zanzibar wanakuwa na kigugumizi ktk hilo.

..naomba uondokane kabisa na masuala ya kuzungumzia damu-damu.

NB:

..majadiliano ya nini wakati wa-Zanzibar are convinced kwamba muungano unawarudisha nyuma?
 
Tuanze na Umeme Zanzibar wananunua umeme mara mbili ya bei uuzwao T.bara fuatilia utajua hilo.

Unajua kua TRA wanaenda na boti ya mwanzo zanzibar nakukusanya kodi na jioni hurudi na boti ya mwisho wakiwa na sanduku la pesa za ushuru wakiskotiwa na ulinzi mkali, sasa kuna ubaya gani zanzibar wakitozwa ushuru mara moja wakati pesa haibakii znz? Hii ni mbinu za kuiuwa bandari ya Znz na tayari wamefanikiwa.

Na kuhusu pesa wanazopewa Zanzibar unapeswa kujua kua hawakaiwi bure,zanzibar wanashea 12% ndani ya bank kuu,na pia munakusanya ushuru,sasa kuwalipa wanajeshi wenu kunashida gani hasa ukizingatia kua kua wanajeshi wote wazanzibar ni kutoka bra idadi yao inashinda idadi ya wananchi wa visiwani, sasa si mumejipatia ajira wenyewe tu na pia munalinda koloni lenu.

tunawalinda na nyie pia msije mkachapana. lakin znz ni ardhhi ndogo sana, na nina sababu ya kuamini kwamba pato lake ni insignificant ktk muungano. tuwaache wakafe njaa
 
Takashi,
Usiseme sera za CCM ni kutoka serikali mbili kuwa moja ila ni matamanio ya viongozi wengi wa CCM Zanzibar (ASP) laa sivyo sioni sababu kabisa ya CCM na CUF kuungana kuunda chombo kimoja chini ya ilani za CCM. Na Wazanzibar mlipiga kura kuupa baraka Muafaka ambao unawaunganisha zaidi na CCM kutawaliwa. Leo hii Zanzibar hakuna chama cha Upinzani hivyo kulazimu sauti ya wananchi inapitia misikitini na vijiweni. Tatizo lenu kubwa hamtaki kuamini kwamba hao kina Seif wapo kwa maslahi yao binafsi zaidi ya kuitaka Zanzibar huru kama mnavyodai.

Na kuhusu malalamiko ya mabadiliko ndani ya katiba ya muungano pasipo ridhaa ya Wazanzibar sijui kama umewahi kufikiria sababu kubwa ya mabadiliko haya badala ya kuwasingizia bara..Unaweza sema hayo hayakuwa makubaliano baina ya Tanganyika na Zanzibar lakini ikumbukwe tu kwamba sheria ya vyama vingi ilikataliwa na wananchi zaidi ya asilimia 80 lakini ikapitishwa kinyume cha matakwa ya wananchi na rais akiwa mh. Mwinyi Mzanzibar na hakika mabadiliko yote ndani ya katiba ya Muungano yametokana na kuwepo vyama vingi...

Itawezekana vipi leo hii uchaguzi umtafute rais wa Muungano kutoka CCM lakini makamu wake awe ni rais wa Zanzibar hata kama CUF imeshinda hapa hawa watu watakuwa wanatekeleza sera na ilani za chama gani.. Huyo Seif kama makamu wa rais akiwa bara atazungumza kwa niaba ya Wazanzibar au makamu wa rais na kwa sera za CUF au CCM...

Na hata hivyo inakuwaje leo makamu wa rais uchaguzi uliopita Mh.Dr Shein asiwe na nguvu wakati ule au leo kama rais wa Zanzibar ila ingekuwa vizuri kama wakati ule angekuwa Karume na leo hii Dr.Shein, hawa watu si badio ni Wazanzibar na wanashika kiti cha makamu au wanaweza kuwa rais wa Jamhuri. mimi sioni mantiki kabisa ktk hili yaani leo Dr.Shein akiwa makamu wa raiis ndio itabadilisha kitu gani badala ya kuwepo Bilal na alishindwa vipi kuwawezesha alipokuwa makamu wa rais.

Kifupi mkuu wangu jaribu hata wewe kufikiria kitu hii na utagundua kwamba haiwezekani kabisa kuwa na rais na makamu kwa kufuata nchi wanazotoka bali uwezo wao na mrengo wa chama chao, isipokuwa rais wa Zanzibar anatakiwa utoka chama kilichoshinda uchaguzi wa Zanzibar lakini sii lazima huyo huyo awe makamu wa rais. Kufanya hivyo ni kuingia tena muafaka wa CCM na CUF hivyo kuondoa kabisa utawala wa vyama vingi.

Swala la mkakati wa kuondoa jina la Zanzibar nadhani ndilo wazo la CCM na kwa bahati mbaya CUF imejiunga na mtazamo huo ingawa kisiasa wanaendelea kudai wanataka serikali tatu. sasa iweje chama kiwe na muafaka wa makubaliano kushare madaraka na chama kinachotaka kuua Zanzibar maana ndio agenda ya ASP au niseme CCM visiwani.

Baraza la Mapinduzi limefanikiwa kuwameza CUF ktk huu muafaka, hivyo leo tunautawala wa chama kimoja Zanzibar chenye malengo ya KiCCM na haitakuwa rahisi kuunda serikali tatu pasipo vyama hivi kuanza mgogoro baina yao. Kumbuka tu ni Mwinyi aliyepiga vita kauli ya Malecela kuundwa kwa serikali tatu akihofia matakwa ya uwakilishi wake na ASP..na knachowashinda CUF ni nguvu ya dola ya CCM bara baada ya Mwinyi na Maalim Seif kufikisha malalamishi haya haya kwa Nyerere wakati wa Malecela na Aboud Jumbe, hofu kubwa ilitoka Zanzibar kwa Wazanzibar na sii bara(The record shows).. Kumbuka tu mkuu wangu wakiondoka tu CCM bara, ule uadui wa Hizbu na ASP utarudi kwani CCM Zanzibar ni ASP kwa uhalisia wake na CUF ni Hizbu kiasili - picha haziivi..Muafaka huu ni kwa faida ya CCM na hadaa kwa viongozi wa CUF.

Mwisho umezungumzia mambo ya Muungano ni lazima yazungumziwe na theruthi mbili za wabunge toka bara na visiwani, hii haina maana yoyote zaidi ya katiba ya kwanza kufikiria kwamba wajumbe wote watatoka chama kimoja CCM, lakini maadam leo hii wabunge wa bunge la Muungano wanatoka CUF na CCM inakuwa sii rahisi kugusia maswala ya muungano pasipo kuwa ni agenda ya chama kimoja. zanmani yalihusu maslahi ya nchi lakini maadam sasa hivi tunawakilishwa na wabunge toka vyama tofauti, agenda za Muungano zinagawika kwa sera za vyama kwa maslahi ya Zanzibar kitu ambacho CCM na CUF hawakubaliani na ndio maana wakawa vyama pinzani. Hivyo bara tunaweza kusimamisha theruthi tatu ya wabunge wetu lakini Zanzibar tutakuja na swala la wabunge watoke chama gani zaidi maana haikuwepo ktk katiba.

Mimi nachoweza kusema ni kwamba tunahitaji katiba mpya na all parties ktk jamii zetu wahusishwe ipaswavyo kuhakikisha haki za bande zote zinatazamwa kwa mara nyingine kulingana na mfumo wa kisiasa uliopo leo na sii maswala ya Wazanzibar au Wabara unless haki na desturi za Wananchi wa upande wowote zinakiukwa.

Laa sivyo nitakwambia tu kwamba Wapishi wengi huharibu mchuzi na ndicho nachokiona kwa Zanzibar kwani maswala muhimu ya kukiwezesha kisiwa hiki yanakiukwa na ulalamishi wa Zanzibar ni kwa Wazanzibar hali nusu ya Wazanzibar wamehamia bara na karibu the population ni watu wa kuja mnatafuta mengine makubwa zaidi. Leo imefikia hata Mhindi mkimbizi wa kiismaliia kuhoji uzawa na uraia wa Karume hali yeye mwenyewe rangi yake inamtema. Nachelea kusema kwamba tabia hii ya kibaguzi wanayo sana wahindi na waarabu ambao siku zote hujiona wao wabora zaidi ya mtu mweusi, huu upepo wa kuitaka Zanzibar kwa nguvu zote usiwe ni sauti ya hao wabaguzi ambao asili yao ni HATE.. yaani roho mbaya kwa watu wa mataifa na mila tofauti na zao..
 
Nonda,

..u keep on invoking Southern Sudan time and again.

..kwa mtizamo wangu the case and the plight of former Southern Sudanese is quite different frm what is going on in Zanzibar.

..lini ulimuona msudani kusini akiongoza serikali ya Khartoum?

..naomba uondokane kabisa na masuala ya kuzungumzia damu-damu.

NB:
..majadiliano ya nini wakati wa-Zanzibar are convinced kwamba muungano unawarudisha nyuma?

JokaKuu.
Umeshasahau hii damu damu kwa haraka?
Serikali aliyoongoza Mkapa ilifanya nini huko Zanzibar? ilizalisha wakimbizi na vifo kadhaa.... Arusha kilitokea nini? Damu tayari imeshamwagika na itamwagika TZ kama hatutapatia dawa matatizo tuliyonayo.

Katika kadhia ya kuitaja Sudan ya kusini ni kuwa referendum imekuja baada ya hiyo damu kumwagika kwa muda mrefu...lakini katika serikali ya bashir baada ya majadiliano msudan kusini amekuwa makamo wa rais au sio mmoja wa viongozi wa serikali huyu ?na ndie anayemtia joto Bashir juu ya mambo ya Sudan ya kusini!

Umeshasahau kuwa suala la kura ya maoni lilikuwa ni wazo la CCM ili ku-delay na ku-derail mapatano Zanzibar? Ndio CUF walilipinga mwanzoni lakini baada ya Seif na Amani kukutana waliona ni njia ya kuiadabisha CCM.Na walifanya kampeni ya kura ya "ndio"....again hapa suala la kura ya maoni lilikuja kupitia majadiliano ya vyama na baadae kwenda kwenye baraza la wawakilishi...sasa ni vyema yakipatikana majadiliano ya pande za muungano na kama itakuja referendum basi itafuatia kwa bunge na baraza la wawakilishi kufanya kile kinachohitajika.
 
Baraza la Mapinduzi limefanikiwa kuwameza CUF ktk huu muafaka, hivyo leo tunautawala wa chama kimoja Zanzibar chenye malengo ya KiCCM na haitakuwa rahisi kuunda serikali tatu pasipo vyama hivi kuanza mgogoro baina yao. Kumbuka tu ni Mwinyi aliyepiga vita kauli ya Malecela kuundwa kwa serikali tatu akihofia matakwa ya uwakilishi wake na ASP..na knachowashinda CUF ni nguvu ya dola ya CCM bara baada ya Mwinyi na Maalim Seif kufikisha malalamishi haya haya kwa Nyerere wakati wa Malecela na Aboud Jumbe, hofu kubwa ilitoka Zanzibar kwa Wazanzibar na sii bara(The record shows)....

Ilipobainika mwaka 1992 kwamba Zanzibar ilikuwa na mipango ya kujiunga na jumuiya hiyo ya kiislamu kulizuka mvutano mkubwa ambao ulizaa hoja ya Wabunge wa Tanzania Bara kudai "Tanganyika yao." Waziri Mkuu wa wakati huo John Malecela na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM Marehemu Horace Kolimba walipoteza nafasi zao, kwa shinikizo la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyedai kwamba wakuu hao walikuwa wamemshauri vibaya Rais wa wakati huo Ali Hassan Mwinyi.



Wakati Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilipojiunga na jumuiya hiyo mwaka 1992 kulizuka mvutano mkubwa hata miongoni mwa viongozi wa juu wa Serikali ya Tanzania hata ikafikia mahali ambapo ilidaiwa kwamba Waziri Mkuu wa wakati huo Bw. John Malecela na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM marehemu Horace Kolimba walichukizwa na jambo hilo na hivyo kubariki wazo la kikundi cha Wabunge 55 wa CCM (G 55) kilichotaka iundwe Serikali ya Tanganyika.
Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa CCM walijiwa juu na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa kuruhusu wazo la kudai Serikali ya Tanganyika lijadiliwe Bungeni wakati sera ya CCM iko wazi kwamba ni Serikali moja. Mwalimu Nyerere aliwataka wale wote wanaotaka kujadili suala hilo wajiuzulu kwanza uanachama wao wa CCM
Tanzania sasa kujiunga na OIC.

Mkuu.
umeandika mengi lakini haya yanathibitisha kuwa aina ya muungano tulionao ni bomu. mazingaombwe...nililofarajika ni kuona umetaja umuhimu wa katiba mpya..je katiba mpya bila ya kuujadili muungano ndio tutaweza kutatua matatizo sugu ya muungano na muundo wake?

Mambo ya muungano wa nchi ni ya kiserekali , kwa maana ya nchi wanachama,wananchi wa nchi wananchama,wabia..si ya vyama vya siasa. Hili linazidi kuukoroga muungano na ndio sababu CCM wanaona muungano ni mali yao na wanataka kuulinda vyovyote iwavyo! Our Muungano is out-dated! zinahitajika serikali za tanganyika na serikali ya Zanzibar kuujadili tena

...Iko wapi serikali ya Tanganyika? sasa niambie utakishika vipi kivuli hiki? Utatatua vipi utata wa muungano hapo? Mtoto(Muungano) kaua mzazi wake mmoja na sasa anamyemelea kummaliza wa pili.

Anyway, nani anauwelewa, anaufahamu muungano wa Tanganyika na zanzibar?...Tuseme tu..haueleweki...it is a ghost!
 
Mkandara, Ahsante kwa maoni yako. Kwa ridhaa yako naomba nishadidie yangu senti moja.
Mkandara;
Leo hii Zanzibar hakuna chama cha Upinzani hivyo kulazimu sauti ya wananchi inapitia misikitini na vijiweni. Tatizo lenu kubwa hamtaki kuamini kwamba hao kina Seif wapo kwa maslahi yao binafsi zaidi ya kuitaka Zanzibar huru kama mnavyodai
Madhara ya sauti za vijiweni yanaonekana kwasababu watu wanasadiki kile wanachosikia bila tafakuri. Kwa mznz wakawaida anayeishi kigamboni au ilala hili la muungano halielewi, angependa watu waishi kama walivyo. Hoja za kundi la kuuvunja muungano nyingi zimejikita katika madaraka, tunataka mawaziri sawa JMT, tunataka wabunge idadi sawa, tunataka IGP au CDF kwa zamu n.k yote hayamgusi mznz wa kawaida.
Na kuhusu malalamiko ya mabadiliko ndani ya katiba ya muungano pasipo ridhaa ya Wazanzibar sijui kama umewahi kufikiria sababu kubwa ya mabadiliko haya badala ya kuwasingizia bara
Ridhaa ipi zaidi ya ile ya wabunge wao ndani ya JMT? Na wala hajajitokeza kiongozi kulisema hadharani, yote haya yapo vijiweni, maskani na misikitini.
Itawezekana vipi leo hii uchaguzi umtafute rais wa Muungano kutoka CCM lakini makamu wake awe ni rais wa Zanzibar hata kama CUF imeshinda hapa hawa watu watakuwa wanatekeleza sera na ilani za chama gani.. Huyo Seif kama makamu wa rais akiwa bara atazungumza kwa niaba ya Wazanzibar au makamu wa rais na kwa sera za CUF au CCM
Na ikitokea vinginevyo Rais wa znz akashindwa kutekeleza majukumu kwa sababu za kibinadamu, makamu ambaye ni Seif wa CUF ndiye atakuwa Rais kwa muda huo, sasa akiwa ndani ya JMT, si hili ni kuleta GUN bara hata kama Tanzania bara!
Pili, Rais wa znz akiwa makamu wa Rais, siku Rais wa JMT akishindwa majukumu kwasababu za kibinadamu, Rais wa znz atakuwa na authority gani ndani ya JMT? hakuchaguliwa na Tanzania bara!
Dr.Shein akiwa makamu wa raiis ndio itabadilisha kitu gani badala ya kuwepo Bilal na alishindwa vipi kuwawezesha alipokuwa makamu wa rais
Ni kutafuta tu sababu hata kama haipo. Husikii wanasema IGP na CDF wawekwe kwa kupokezana, sijui ina mantiki gani hii!!! Ni matokeo ya hadithi za vijiweni
Haiwezekani kabisa kuwa na rais na makamu kwa kufuata nchi wanazotoka bali uwezo wao na mrengo wa chama chao, isipokuwa rais wa Zanzibar anatakiwa utoka chama kilichoshinda uchaguzi wa Zanzibar lakini si awe makamu wa rais. Kufanya hivyo ni kuingia tena muafaka wa CCM na CUF hivyo kuondoa kabisa utawala wa vyama vingi
Wakati wanajadiliana Seif na Karume hawakushirikisha mtu kutoka JMT, jambo jema. BLW likafanya marekebisho yaliyogusa katiba ya JMT bila kushirikisha JMT. Leo hakuna waziri kiongozi znz, katiba ya JMT inamtambua na haimtabui makamu wa Rais. Kwahiyo hakuna sababu kuleta mambo ya GNU ndani ya JMT.
Baraza la Mapinduzi limefanikiwa kuwameza CUF ktk huu muafaka, hivyo leo tunautawala wa chama kimoja Zanzibar chenye malengo ya KiCCM na haitakuwa rahisi kuunda serikali tatu pasipo vyama hivi kuanza mgogoro baina yao
Serikali ya tatu ishughulikie nini? mbona hakuna mznz anayenijibu, maana ukitaka kitu lazima kuwe na sababu. Serikali ya tatu itaendeshwaje na kwa utaratibu gani?
Rais wa serikali ya tatu atakuwa na mamlaka gani ikiwa znz wanadai kiti UN, EA n.k
Kumbuka tu mkuu wangu wakiondoka tu CCM bara, ule uadui wa Hizbu na ASP utarudi kwani CCM Zanzibar ni ASP kwa uhalisia wake na CUF ni Hizbu kiasili - picha haziivi..Muafaka huu ni kwa faida ya CCM na hadaa kwa viongozi wa CUF
Wapo wanaosema mapinduzi daima, na wengine wanasema mapinduzi ni ya Nyerere na Okello. Angalia mkanganyiko huu! ndio chanzo cha manung'uniko ya muungano, yaani muungano ni 'bangusilo' the place to vent out frustration as a result of underground family feud.
Ulalamishi wa Zanzibar ni kwa Wazanzibar hali nusu ya Wazanzibar wamehamia bara na karibu the population ni watu wa kuja. Mhindi mkimbizi wa kiismaliia kuhoji uzawa na uraia wa Karume hali yeye mwenyewe rangi yake inamtema. Tabia hii ya kibaguzi wanayo wahindi na waarabu,siku zote hujiona wao wabora zaidi ya mtu mweusi, huu upepo wa kuitaka Zanzibar kwa nguvu zote usiwe ni sauti ya hao wabaguzi ambao asili yao ni HATE.. yaani roho mbaya kwa watu wa mataifa na mila tofauti na zao
Siku zote nasema wznz wengi wanaimba nyimbo wasizojua maana ya tungo zake. Unaposikia watu wanasema vunja muungano ili tufutiwe visa za Oman, inasikitisha sana na inafikirisha. Hivi muuza pweza pale feri au mpiga matofali pale kigamboni tatizo lake ni kwenda Oman kweli!! yaani muungano hauna maana zaidi ya kufutiwa visa ya Oman, so sad!
Nguvu unayoisema mkandara ipo nyuma ni kweli kabisa, nasema Znz ni yao wavunje muungano na kurejea katika nchi ya amani, mizambaru, jasmini na asali.
 
Mimi nachoweza kusema ni kwamba tunahitaji katiba mpya na all parties ktk jamii zetu wahusishwe ipaswavyo kuhakikisha haki za bande
zote zinatazamwa kwa mara nyingine kulingana na mfumo wa kisiasa uliopo leo na sii maswala ya Wazanzibar au Wabara unless haki na desturi za Wananchi wa upande wowote zinakiukwa.

Laa sivyo nitakwambia tu kwamba Wapishi wengi huharibu mchuzi na ndicho nachokiona kwa Zanzibar kwani maswala muhimu ya kukiwezesha kisiwa hiki yanakiukwa na ulalamishi wa Zanzibar ni kwa Wazanzibar hali nusu ya Wazanzibar wamehamia bara na karibu the population ni watu wa kuja mnatafuta mengine makubwa zaidi. Leo imefikia hata Mhindi mkimbizi wa kiismaliia kuhoji uzawa na uraia wa Karume hali yeye mwenyewe rangi yake inamtema. Nachelea kusema kwamba tabia hii ya kibaguzi wanayo sana wahindi na waarabu ambao siku zote hujiona wao wabora zaidi ya mtu mweusi, huu upepo wa kuitaka Zanzibar kwa nguvu zote usiwe ni sauti ya hao wabaguzi ambao asili yao ni HATE.. yaani roho mbaya kwa watu wa mataifa na mila tofauti na zao..
Last edited by Mkandara; Today at 08:58 PM.

Mkuu vizuri kama unaamini Demokrasia. Na Demekarasia ambayo inakua huru na ya uwazi. Mimi nitakua na machache sasa hivi. Nimeona hata Mkuu Nonda amechanjia kujibu makala yako vizuri tu. Hata mimi vile vile nimeiunga mkono...Tatizo nililoliona kuwa tuna mtazamo tofauti kuhusu hali ya siasa za Tanganyika na Zanzibar. Ni kama muisilamu na mkristo anavyo amini Mungu.

Ninacho amini mimi ni kuwa kuna kasoro nyingi sana Katika Muungano na nathubutu kusema hata hao viongozi hawana uwezo wa kutafuta ufumbuzi wa kasoro zilizopo. Kuna wale wanao amini tu Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika ,pamoja na kwamba hawatamki wazi wazi. Mimi sitegemei kama kuna mtu anaweza kubadilisha mtazamo wa wazanzibari kuhusu muungano. Njia pekee na ambayo itakuwa fair ni kuwa na muungano wa serikali tatu. Lakini kuendelea kutafuta chanzo cha kuku, jubu utalipa kwa imani yako.

Katika mjadala wa rasimu ya katiba Mzee, H.N. MOYO alimwabia Mh, SITTA Kama wakati wao umekwisha. Sasa vijana wana mtazamo mpya kuhusu Muungano. Wewe anataka muungano uwe vipi? serekali mbili kama ulivyo ? serikali tatu? au serikali moja? Kuendelea kuwaingiza Nyerere ,Karume , Jumbe Kawawa hakutasaidia lolote. Hawa wakati wao umekwisha.

Kuhusu watu wa upande mmoja kuishi sehemu ya pili ya muungano isiwe kigezo kama hao watu wanaukubali muungano kama ulivyo. Mimi vile vile nimepata bahati kuishi nje ya Africa kwa miaka mingi tu, na sehemu niliyoishi haikua na uhusiano wakaribu na Tanganyika wala Zanzibar. Taratibu za uhamiaji ziko wazi, unaomba kibali cha kuishi hio sehemu. Kuna malipo mienzi mitatu ,sita mwaka na kuendela.

Hii vile vile inapunguza uhamiaji wa ovyo ovyo. Hii inwezekana alimradi kuwe na sheria za uwazi." HATE " hakuna mtu anazaliwa nayo ni mazingira yanasabaisha hiyo.
 
Wana Jf, ifike mahali mjadala ukidhi na kujibu haja na hoja kama zinavyotolewa. Inashangaza wengine kujenga hoja ambazo ima hawawezi kuzitetea au pengine wameagizwa na hawana majibu. Suala la kuwa wanataka znz ni la wazanzibar, sidhani limekuja tu kichwani bila kuwa na sababu za msingi. Ndio maana MMKJ ameuliza kama raia, je wenzetu ni ipi hiyo mnaitaka? Hakuna jibu zaidi ya kejeli . Tukajua hili ni swali gumu tuliache kama lilivyo. Huku mjadala ukiendelea maswali yanazidi kuzuka na hakuna majibu, sidhani kama hii ni sawa.

Znz inataka kuwa huru kama inavyodai, ili ipate kiti UN, EA, SADC, na mahusiano kama nchi pekee katika mashirika ya kimataifa na kidini. Znz tayari ina Rais, makamu wawili, wimbo wa taifa, bendera, mamlaka zake za kiuchumi na hata kimechezo.

Popote duniani, iwe Union, Confederation au Federation kuna mambo ya msingi ya pamoja yanayoliunganisha taifa.
Mfano, Canada ni Confederation na kila jimbo lina sheria na zake, lakini ipo bendera moja ya Canada, wimbo mmoja wa Taifa na shughuli zenye sera katika sura ya utaifa. Tofauti za sheria kati ya jimbo na jimbo inatokana na mazingira. Kila jimbo lina bajeti yake, Gavana na Waziri mkuu(premier), lakini waziri mkuu (Prime minister)wa Canada ni mmoja ndani ya bunge la taifa (House of Common). Sera za canada za nje, ulinzi, mahusiano na vyombo vingine ni moja. Kila jimbo pamoja na kuwa na bendera yake inachangia katika serikali kuu.

Marekani ni Federation, nayo kama Canada kila state ina mipango yake na mchango wake kuendesha Federal govern. Lakini marekani ni moja kwenye mambo ya kimataifa, kuanzia UN, sera za nje, mambo ya ndani, vyombo vya usalama n.k. Hakuna balozi wa state au state inayofanyakazi na Unicef kama state bila kupitia federal.
Mifano hii ipo katika nchi kama India, Nigeria n.k

Swali:
Kwa mtazamo wa znz kama nilivyoainisha paragraph ya pili, wananchi wake wanataka kuwe na serikali tatu, yaani ya Tanganyika, Zanzibar na ya shirikisho.
a)Je, ni mambo gani ambayo znz inadhani inaweza kuwa na ushirikiano na Tanganyika katika hicho kinachoitwa serikali ya shirikisho?
Hapa hakuna siasa, ni swali na jibu na mwenye uelewa nifahamishe tafadhali.

b)Hiyo serikali ya shirikisho itakuwa na rais mtendaji (executive) au rais wa mfano (ceremonial figure)?
Kumbuka mambo muhimu znz imeshayaondoa na inataka kuyaondoa mengine

c) Hiyo serikali ya shirikisho itagharamiwaje na kwa utaratibu gani?
Kumbuka zitakuwa ni nchi mbili tofauti zilizotengeneza shirikisho.

Nawaombeni mnisaidie kujibu haya ili tuweze kuendelea na mjadala ukiwa na dira. Kusema serikali tatu bila ya ku 'define' ni upungufu wa kujenga hoja, na tusije kujikuata nasi ni sehemu ya wale wanaodai Tanganyika irudi wakiulizwa ili iwe nini hawana jibu!!! Tukiuliza mnataka Tanganyika irudi ili muungano uvunjike au kuwe na shirikisho! wanasema shirikisho, sasa kama ni shirikisho mbona hatupewi maswali ya majibu hapo juu?

Maelezo yangu hayakinzani na hoja ya znz kuvunja muungano kwa vile ni haki yao, na hakika nasisitiza waanze na mswada BLW, halafu, maandamano Dar es salaam walipo wengi ili tuwaunge mkono.Uwezo wanao kwa kutumia mbinu zile zile za marekebisho ya katiba, walivyorudisha wimbo wa taifa, bendera yao, wakajitoa hadi ligi ya soka, wakaanzisha bandari huru, mashirika yao n.k. Hili linawashinda nini?
(Huu ni ufafanuzi tu usivuruge maswali yangu na kugeuzwa hoja)
 
The ZNZ issue always AMAZES me!
Sijawahi hata siku moja kuelewa nini kinatakikana na kila mhusika na kwa sababu gani!

SEHEMU MBILI ZIKIUNGANA/KUUNGANISHWA KISHA IKATOKEA KUWA HAZISHIKAMANI - JE NI VEMA KUONGEZA GUNDI KULAZIMISHIA KUUNGANISHA..AU NI KUANGALIA NI VIPI SEHEMU HIZO ZIBAKIE KIVYAKEVYAKE?

HUENDA GUNDI IMECHOKA, KUONGEZEA ZAIDI HAKUTATUA SABABU INAYOFANYA GUNDI KUACHIA...


Wazanzibar kuna jinsi wahisi sisi watu wabara(watanganyika) tunafaidi sana nchi yao. Wanafikiri tumenufaika zaidi kuliko wao. wakati mwingine wanafikiri tumewazuia kuwa huru kufanya maamuzi ambayo wanafikiri yana manufaa kwao na kwamba kama siyo muungano leo hii wangekuwa matajiri kama Qatar au UAE(United Arab Emirates).

Wanahisi kujiunga na OIC na FIFA na kuwa mabalozi wao moja kwa moja basi ni chanzo cha maendeleo. Ninataka waone mbele zaidi waseme wanataka nini au waseme Muungano umewakwamisha wapi wakati wapemba wamejaa tele na maduka makubwa Kariakoo na vitongoji vya Dar mpaka wametungiwa nyimbo.
Mbona kuna nchi kama Komoro wana uhuru wao, Sychelles nao ni kisiwa na wana uhuru wao lakini bado hawako mbali sana kiuchumi? Wasifikiri

Tungefanya jaribio la kuingia mkataba mwingine wa kuwaruhusu kwa miaka kumi wajitenge ili tushuhudie watakavyo JUMP kiuchumi.

Mimi ningefurahi kuwa bila hawa watu kwani ni wasumbufu na sijawahi ona faida yoyote ya Muungano zaidi ya kugawanya kile kidogo tulicho nacho kama madini na kuwagawia . Waachiwe wajiondokee.
 
Ni Zainzibar ipi WANAITAKA?
Ikiwa swali hili lilikusudiwa Wazanzibari, basi hakuna ambaye angelitoa maoni angalau yanayofananafanana na matakwa ya Wazanzibari kama Wazanzibari wenyewe. Vyenginevyo, kwa wasiokuwa Wazanzibari kujibu swali hili itakuwa ni kuwasemea na pengine kusemewa huko kusioane na matakwa au mawazo yao.

Imani yangu ni kuwa kama ingepigwa kura ya maoni na swali kama hili lililoulizwa na MwanaKijiji wangeulizwa Wazanzibari, na wakawa huru kutoa maoni yao, kila kundi lingepata wafuasi wake japo wachache: Wanaotaka Usultani, Ubwana na Utwana, Ukoloni wa Mwingereza, Zanzibar ya kabla na baada ya Mapinduzi, wanaotaka Unguja na Pemba kila mtu kivyake n.k., lakini ninachoamini, ni kuwa Wazanzibari waliowengi wanaelewa faida na hasara za Muungano (na naomba niwe nimekosea lakini kwa mtazamo wangu faida ni nyingi kuliko hasara), kwa hiyo naamini pia kuwa katika kura hiyo ya maoni waliowengi watachagua kubakia katika Muungano LAKINI katika misingi ileile iliyomo katika Hati ya Muungano na mambo kumi na moja, huku kukiwa na uwezekana wa kutaka yafanyiwe masahiisho hata hayo kumi na moja, kulikoni Muungano huu tulionao sasa ambao viepngele vya mambo ya Muungano vimekuwa mara mbilo zaidi.

Pengine mawazo yangu hapo juu yameathiriwa na kuwa kwangu M(tanzania wa)zanbari, na kutokana na maoni yangu binafsi kama mtetezi wa Muungano, sio wa Tanzania tu bali wa Afrika yote. Kwa hiyo, kwa kujibu swali la MKJ, nikiwa ninatoa maoni yangu binafsi na wala sio kuwajibia Wazanzibari wote, Zanzibar ninayoitaka ni Zanzibar ya Muungano baada ya Muungano, nikiwa na maana ya Zanzibar ambayo Wazanzibari wataulizwa na kutoa maoni yao juu ya Muungano gani wanautaka, na kama ilivyo katika demokrasia, Zanzibar itakayokuwa mshindi ni ile iliyoamuliwa na Wazanzibar waliowengi (hata kama wataamua Kiongozi wao awe Raul Castro, Hugo Chavez, Malkia wa Uinerza, Qaboos, Hu Jintao au ******, ni uamuzi wao, halmuradi tu wameamua kidemokrasia na wala sio maaumuzi ya Zanzibar kuamuliwa Chamwino.
 
Kweli bro kwani hata waandishi wa habari wanashindwa kutofautisha Unguja ni ipi na Zanzibar ni nini! Kisiwa cha Unguja sawa sawa na mkoa wa Kilimanjaro ( Moshi) au Mara (Musoma) nk. Na bahati mbaya mno kwa vyombo vya habari huwapa nafasi wachache wapenda umimi kuzungumza lakini walio wengi Unguja na Pemba twapenda Muungano kwa muundo wowote ule.
Haaa haaa haaa! Nipo Mkuu, naona ulisahau kuwa kuna Tanzania visiwani kama ilivyo Tanzania bara, katika Serikali ya Muungano. Binafsi ninapenda kuwa na Tanzania Visiwani, ambayo inaundwa na Unguja na Pemba. Zanzibar ni jina la mji mkuu wa Unguja.
 
Back
Top Bottom