Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

Lahaullah! busara ituongenze katika majadiliano inshallah.

Suala lililopo mbele yetu ni kuwa wznz waliopo South Africa wanajinasibu hivyo. Hata kama ni wamakuwa bado ni wznz kwasababu wapo wanyasa na wameongoza znz wakiwa na hadhi ya uzanzibar. Ukianza kusema wamakuwa basi hakutakuwa na Znz kwasababu hakuna anayeweza kusema yeye ana asili ya znz, mathalani wapo wenye asili ya Oman, Yemen, Saudia, India n.k

Hao Waznz wa South Africa walitaka wawe na vitambulisho vya 'Asiatic' ndipo swali linazuka, je ina maana gani wao kunasibishwa na waasia kuliko wabantu na wakabaki kubeba vitambulisho hivyo vifua mbele!

Je, si kweli kuwa asili hufuata asili na haya tunayoyaona yanashabihiana na kile kilichotokea South Africa? Nikimaanisha wznz kutaka kubaki Tanganyika lakini wakiwa na vitambulisho vya uznz a.k.a 'asiatic'

Je, kutamani kufutiwa visa za Oman (mzalendo forum) sio aina nyingine ya 'modern Asiatic'?

Hizi ndizo hoja za kujadili na kutufikirisha.

Pili, mambo ya znz yananihusu kwasababu nimeishi znz nina marafiki, ndugu n.k. Hapa bara naishi na wznz ni ndugu na marafiki. Muhimu zaidi mambo ya kisiasa mengi ni sehemu ya ushirikiano na znz. Ni kweli znz inaweza kuwa hainihitaji kwa nywele zangu za kipipili, lakini inanihitaji kwa kodi yangu. Zaidi ya yote nchi yangu Tanzania inahitaji mchango wangu wa hali na mali pamoja na fikra.

Inshallah, tumuombe mwenyezi Mungu S.W.T atujaze hekima na busara katika ilm na mulankasha ili tunapohitilafiana kwa hoja, jazba iwe mbali nasi, nasi tuwe mbali nayo.

Mkuu naomba unifahamu kua, kutaka mtu atambulike kua nani, haimaanishi kua ndivyo alivyo.

Hao waliomba kutambuliwa hivyo, kwa sababu walikuwa wanataka kupata priviledges fulani katika mfumo huo wa apartheid.

Mimi nnao rafiki zangu huko bara, ambao walishikwa wakati wa mutiny ya 1964 na kwa mujibu wa prison regulations za wakati huo, walitaka watambuliwe kama Indians ili badala ya kula dona, wale chapati. Jee iliwageuza kua Wahindi?

Hapa Zanzibar pia wapo watu ambao wanapenda kujiona au kujiita Waarabu kwa maslahi yao fulani tu.

Wapo pia Waarabu waliojiita Waafrika kwa maslahi fulani ya wakati fulani tu.

Huko bara wako Waislamu waliobadili majina ili waonekane ni Wakristo kwa maslahi fulani.

Jee wale Watanganyika wa Fiji nao warudi?

Kutamani kwa watu kufutiwa visa ya Oman ni sawa na pale nyie wabara mlipotamani kufutiwa passport kuja Zanzibar.

Na mmeingia mpaka Zanzibar yote mshaichukua, wenyewe hatuna pa kukaa.
 
Mkuu naomba unifahamu kua, kutaka mtu atambulike kua nani, haimaanishi kua ndivyo alivyo.

Hao waliomba kutambuliwa hivyo, kwa sababu walikuwa wanataka kupata priviledges fulani katika mfumo huo wa apartheid.

Mimi nnao rafiki zangu huko bara, ambao walishikwa wakati wa mutiny ya 1964 na kwa mujibu wa prison regulations za wakati huo, walitaka watambuliwe kama Indians ili badala ya kula dona, wale chapati. Jee iliwageuza kua Wahindi?

Hapa Zanzibar pia wapo watu ambao wanapenda kujiona au kujiita Waarabu kwa maslahi yao fulani tu.

Wapo pia Waarabu waliojiita Waafrika kwa maslahi fulani ya wakati fulani tu.

Huko bara wako Waislamu waliobadili majina ili waonekane ni Wakristo kwa maslahi fulani.

Jee wale Watanganyika wa Fiji nao warudi?

Kutamani kwa watu kufutiwa visa ya Oman ni sawa na pale nyie wabara mlipotamani kufutiwa passport kuja Zanzibar.

Na mmeingia mpaka Zanzibar yote mshaichukua, wenyewe hatuna pa kukaa.

Nimeshukuru umekiri kuwa colonial mentality and superiority complex ni matatizo makubwa sana znz.
Watanzania walioko fiji wakitaka kurejea Rufiji walikotoka hewala na waje, tena tunawakaribisha kwa furaha kutokana na uzalendo wao wa kukubali kuhusishwa na wabantu wamatumbi wenzao ambao waznz walioko South Africa wanawaona ni binadamu wa kiwango dhalili.Wafiji hawafikirii kuwa sehemu ya philipino, malaysia aua Oman.

Kuna Jambo ambalo hulielewi au unajaribu kulibadilisha . Mjadala wa kufuata visa za znz niliuona kwa macho, kusoma na kuuliza binafsi. Siku simuliwa na labda nikupe kilichojiri ili usiendelee kudanganywa zaidi.
Tanzania bara kwa miaka mingi walitakiwa kwenda znz kwa passport na wakiwa huko wanakuwa 'treated' kama wageni kutoka nchi nyingine. Walitakiwa kupata work permit, kulipa malipo yote kama foreigners ikiwa ni pamoja na huduma za elimu na afya.
Wakati hayo yakitokea wznz walikuwa wanaingia kama mtu anayetoka mkoani, kufanya kazi bila kuulizwa, biashara, kupata huduma zote kama mtu mwingine. Mfano mzuri ni wasomi wa znz ambao wengi ni graduate wa UDSM akiwemo Maalim Sef. Hawa walisoma bure bila kulipa hata senti tano.
Bara wakahoji, endapo sisi ni JMT iweje kuwepo na vikazwo upande mmoja na mteremko upande wa pili?
Tanzania bara wakasema, kama tunaenda znz kwa passport basi nao waje kwa passport. Narudia wakaweka condition kuwa wznz waje kwa passport. Hawakuomba kufutiwa pasport bali walisema utaratibu wa kawaida unaotumika duniani ni passport kwa passport au bila passport kwa wote.

Wznz wakabaini kuwa wao watakuwa waathirika wakubwa wa mfumo huo kupoteza haki za uhamiaji na makazi ya kudumu(ndio maana leo nusu wanaishi bara), ajira, mafao ya huduma za kijamii ikiwemo elimu bure (angalia CV ya viongozi wa znz ),umiliki wa ardhi na kupoteza idadi ya watalii. Wao wenyewe wakaondoa hiyo passport. Hakuna mahali Tanzania bara ilipeleka ombi, ila iliweka masharti mkuki kwa mkuki, period!

Inachekesha sana kusikia wabara wameichukua znz, ni wapi? maana ajira hawapewi isipokuwa sekta binafsi ambayo wznz wengi hawataki kufanya kazi wanazoita za kitumwa. Lakini muhimu hatuhitaji hoja za maskani, tupe takwimu za wabara waliopo znzna wznz walipo bara.

Kama kuna kitu kinawatisha wznz wengi kuhusu kuvunja muungano ni kuelewa kuwa wataondoka bara na kama ni ukaaji basi nao watakuwa kama mgeni mwingine. Hawa waoapiga kelele ni kama 200 tu, wale wa kawaida msasani, kigamboni, makorora, Ilala n.k hawataki kusikia kitu kuvunja muungano. Mvuvi anayeleta pweza zake feri umwambie aje kama mganda atakumwagia uchafu usoni.
Huko mawizarani ndio usiseme, ni ninyi wachache wenye kutamani rangi na madaraka ndio mnaifikiria kanaani, wenzenu wengi wanayo kanaani hata kama hawasemi.
 
Wenye asili ya bara kule Zanzibar ni kina nani hasa?

Jamani hebu MM nisaidie kuna jambo naona kama linajificha vile na linatumika na baadhi ya wabaguzi kama fimbo ya kuudhalilisha Muungano.

Hivi kinachotakiwa ni Zanzibar kujitenga na bara au kinatafutwa watu wana nywele za aina gani na rangi gani? Na kama ndiyo hivyo mbona ka harufu ka ubaguzi waziwazi! Na kama tunabaguana kwa mtindo huo hata wao wenyewe tukiwaachia Zanzibar yao watabaguana tu na hata kupigana
 
Bila shaka kitendo cha ndugu zetu wa bara kuchomewa mali zao na ndugu zetu wa huko zanzibar kimetusononesha sana, tena kwa matusi na kejeli kuwa wamewachoka, na wanataka waondoke warudi bara, swali ni je sisi wa huku bara tukiamua kulipa kisasi wale wazenji wa pale kariakoo watapona kweli?? na tukiamua kufanya hivyo si itasababisha madhara makubwa sana kwa nchi yetu...? zanzibarians should wake up, kama hawataki muungano wa andamane na kuwakilisha kilio chao kwa amani na si kwa ubaguzi wa ubara. huu ni upumbavu wa hali ya juuu.. kwenu wadau.
 
wanavielement vya ugaidi so sijui kwa nini tunalazimishiana muungano nao
 
Na Wapemba walivyo jazana huku bara ndio itakuwa balaa,lakini kwa kitendo walicho fanya inasikitisha sana,kuna umuhimu wa kura ya maoni kwa pande zote mbili Bara na Zanzibar kama huu muungano una tufaa au vipi,na kama unatufaa ukae vipi..
 
Na Wapemba walivyo jazana huku bara ndio itakuwa balaa,lakini kwa kitendo walicho fanya inasikitisha sana,kuna umuhimu wa kura ya maoni kwa pande zote mbili Bara na Zanzibar kama huu muungano una tufaa au vipi,na kama unatufaa ukae vipi..

Kweli kabisa, kuliko kukaa na kufanya vurugu zisizo za msingi. hata civil warz cku zote huanza ivi, na mwisho wake tatizo hili litaleta shida pande zote, bara na visiwani.
 
Jamani hebu MM nisaidie kuna jambo naona kama linajificha vile na linatumika na baadhi ya wabaguzi kama fimbo ya kuudhalilisha Muungano.

Hivi kinachotakiwa ni Zanzibar kujitenga na bara au kinatafutwa watu wana nywele za aina gani na rangi gani? Na kama ndiyo hivyo mbona ka harufu ka ubaguzi waziwazi! Na kama tunabaguana kwa mtindo huo hata wao wenyewe tukiwaachia Zanzibar yao watabaguana tu na hata kupigana

Ya Zanzibar inawahusu nini?
 
Nimeshukuru umekiri kuwa colonial mentality and superiority complex ni matatizo makubwa sana znz.
Watanzania walioko fiji wakitaka kurejea Rufiji walikotoka hewala na waje, tena tunawakaribisha kwa furaha kutokana na uzalendo wao wa kukubali kuhusishwa na wabantu wamatumbi wenzao ambao waznz walioko South Africa wanawaona ni binadamu wa kiwango dhalili.Wafiji hawafikirii kuwa sehemu ya philipino, malaysia aua Oman.

Kuna Jambo ambalo hulielewi au unajaribu kulibadilisha . Mjadala wa kufuata visa za znz niliuona kwa macho, kusoma na kuuliza binafsi. Siku simuliwa na labda nikupe kilichojiri ili usiendelee kudanganywa zaidi.
Tanzania bara kwa miaka mingi walitakiwa kwenda znz kwa passport na wakiwa huko wanakuwa 'treated' kama wageni kutoka nchi nyingine. Walitakiwa kupata work permit, kulipa malipo yote kama foreigners ikiwa ni pamoja na huduma za elimu na afya.
Wakati hayo yakitokea wznz walikuwa wanaingia kama mtu anayetoka mkoani, kufanya kazi bila kuulizwa, biashara, kupata huduma zote kama mtu mwingine. Mfano mzuri ni wasomi wa znz ambao wengi ni graduate wa UDSM akiwemo Maalim Sef. Hawa walisoma bure bila kulipa hata senti tano.
Bara wakahoji, endapo sisi ni JMT iweje kuwepo na vikazwo upande mmoja na mteremko upande wa pili?
Tanzania bara wakasema, kama tunaenda znz kwa passport basi nao waje kwa passport. Narudia wakaweka condition kuwa wznz waje kwa passport. Hawakuomba kufutiwa pasport bali walisema utaratibu wa kawaida unaotumika duniani ni passport kwa passport au bila passport kwa wote.

Wznz wakabaini kuwa wao watakuwa waathirika wakubwa wa mfumo huo kupoteza haki za uhamiaji na makazi ya kudumu(ndio maana leo nusu wanaishi bara), ajira, mafao ya huduma za kijamii ikiwemo elimu bure (angalia CV ya viongozi wa znz ),umiliki wa ardhi na kupoteza idadi ya watalii. Wao wenyewe wakaondoa hiyo passport. Hakuna mahali Tanzania bara ilipeleka ombi, ila iliweka masharti mkuki kwa mkuki, period!

Inachekesha sana kusikia wabara wameichukua znz, ni wapi? maana ajira hawapewi isipokuwa sekta binafsi ambayo wznz wengi hawataki kufanya kazi wanazoita za kitumwa. Lakini muhimu hatuhitaji hoja za maskani, tupe takwimu za wabara waliopo znzna wznz walipo bara.

Kama kuna kitu kinawatisha wznz wengi kuhusu kuvunja muungano ni kuelewa kuwa wataondoka bara na kama ni ukaaji basi nao watakuwa kama mgeni mwingine. Hawa waoapiga kelele ni kama 200 tu, wale wa kawaida msasani, kigamboni, makorora, Ilala n.k hawataki kusikia kitu kuvunja muungano. Mvuvi anayeleta pweza zake feri umwambie aje kama mganda atakumwagia uchafu usoni.
Huko mawizarani ndio usiseme, ni ninyi wachache wenye kutamani rangi na madaraka ndio mnaifikiria kanaani, wenzenu wengi wanayo kanaani hata kama hawasemi.

Mkuu Zanzibar ina matatizo mengi si hayo tu, moja ni huu "muungano" feki.

Hili la paspoti kuja Zanzibar sikupingi maana ndio umeona kwa macho, kusoma na kusikia lakini ujue kuwa Zanzibar ni pahala padogo, ni tatizo kuachia watu mpaka kutoka Congo DRC, Burundi na Rwanda kuingia tu kwa sababu wanazungumza Kiswahili.

Wazanzibari hawako Tanganyika tu Mkuu.
 
Katika hali isiyo ya kawaida huko Zanzibar watu wengi wamefurika na wamehudhuria mhadhara ya kupinga muungano uliofanyika viwanja vya Lumuba mjini Zanzibar na hivyo kupelekea mpaka Polisi nao kushiriki katika uchukuaji picha za video katika mhadhara huo.

Kwa kweli Wazenji wamevunja ukimya na kuiweka SMZ katk hali ngumu ya mchakato wa katiba mpya licha ya kuwa kuna polisi wengi waliopelekwa kutoka Tanganyika kwa hofu ya kutokea fujo.
 
Katika hali isiyo ya kawaida huko Zanzibar watu wengi wamefurika na wamehudhuria mhadhara ya kupinga muungano uliofanyika viwanja vya Lumuba mjini Zanzibar na hivyo kupelekea mpaka Polisi nao kushiriki katika uchukuaji picha za video katika mhadhara huo.

Kwa kweli Wazenji wamevunja ukimya na kuiweka SMZ katk hali ngumu ya mchakato wa katiba mpya licha ya kuwa kuna polisi wengi waliopelekwa kutoka Tanganyika kwa hofu ya kutokea fujo.


I really support guys in their struggling....Najua mafanikio yao ya kuuvunja MUUNGANO, nitapata nafuu na mimi, maana SIUPENDI MUUNGANO KAMA NINAVYOICHUKIA CCM, Let them struggle maana sisi, kama vile tumeridhika na Muungano huu...tuko kimya kabisa.
 
weka picha tuone. wewe unaongelea mambo hadi ya video hadi unatutamanisha. weka picha mkuu.
 
Wazenji bwana ni vichwa maji! wakisha vunja muungano watageukiana. wapemba nao wataivunja zanzibar halafu itafuata chakechake mwisho mzigo utakuwa wa kwetu tena! hakyamungu nawaapia muungano ukifa zanzibar itakuwa somalia ya pili!
 
Wazenji bwana ni vichwa maji! wakisha vunja muungano watageukiana. wapemba nao wataivunja zanzibar halafu itafuata chakechake mwisho mzigo utakuwa wa kwetu tena! hakyamungu nawaapia muungano ukifa zanzibar itakuwa somalia ya pili!

Kichwa maji cha kwanza ni chako. Usojua kitu! Kabla ya muungano ilikuwepo zanzibar na ipo na itaendekea kuwepo, labda tanganyika ndo itokee dar kwake, arusha kwake, mtwara kwake na sehemu nyengine. Mnyamwezi ajitangazia urais, mchaga nae hakubali, wamasai kutaka mkoa wa kilimanjaro uwe kenya etc!!
 
Back
Top Bottom