Ni wakati sasa wa Dr. Rioba kujitathmini

Ni wakati sasa wa Dr. Rioba kujitathmini

Siasa inatoka wapi mkuu wakati mambo yako wazi tuambie nilini TBC wamepigiwa simu kwa staili kama hii
Sasa wapigiwe simu kwa uendeshwaji wa kipindi kipi haswaa?
Hata wakiwahita watu kuja kuwahoji haipiti dk 5 na zinaishia kwa wao wenyewe maana wanaongea hao, "mara tumpishe Asha Haji kwa kutusomea vichwa vya magazeti" mara "habari za michezo"
Kwa ujumla bado mabadiliko na ubunifu wa vipindi haujafanywa na Rioba

Na tatizo kubwa hawajataka kujishughulisha kujua watazamaji wanahitaji nini zaidi ya kutujazia bango kubwa la PPRA

TBC aliondoka nayo TIDO MHANDO.
 
Tido aliondoka kwa shindikizo LA mahojiano ya kampeni za ugombea Urais kinyume na matakwa ya chama tawala. Hawataki kuambiwa HAO waache waboronge muda unaisha.
 
Ni vigumu TBC kubadikika. Tangu ikiwa RTD, kilikuwa ni chombo cha propaganda cha CCM. Wakati magazeti ya Uhuru na Mzalendo yakiwa ni "handouts" za CCM, RTD (na sasa TBC) ikawa ni "mouthpiece" ya chama.

Tangu zamani, waandishi na watangazaji
wa RTD/TBC wamekuwa wanafanyiwa "orientation" ya brainwashing ili waitetee CCM tu bila kutafakari.

Tido alijaribu kubadilisha hii hali lakini akatumbuliwa fasta kwa kutuhumiwa kuwa hakuweka maslahi ya chama mbele.

Sasa Dr. Rioba afanye nini? Hoja hapa ni kwamba ili kuifanya TBC iwe na mvuto kwa wasikilizaji/watazamaji, ni lazima iachane na mwelekeo wake wa kipropaganda. Na katika mazingira ya sasa ambapo kuna vyombo lukuki huru vya habari na mtandao wa internet usiohaririwa, hakika propaganda haiwezi kufanya kazi na kwa hivyo anayewekeza katika propaganda imekula kwake!
 
Tbc ilishapote kitambo,
na sababu kubwa ni kutosahihisha makosa yanayotokana na utendaji wa serikali
kila kinachofanywa na serikali wao kazi ni moja tu kusifia bila kufanya uchambuzi ulio huru.
Nani ataangalia au kusikiliza habari ambayo tayari unajua itakavyokuwa?
Kwani Clouds wanaikosoa Serikali?
 
Clouds kazi yake kwa sasa Ni kumfagilia Magufuli. .......wanatumia fursa
Na yeye kwa vile kama kiongozi anapenda kusikia wanaomsifia
 
pesa wandugu pesa ndio inayonifanya ning'anie kwani hata mimi moyo unaniuma ila ndio hivyo tena nitafanyaje na ubunifu wangu ndio umeishia hapo
Duuu pole!
 
Ni vigumu TBC kubadikika. Tangu ikiwa RTD, kilikuwa ni chombo cha propaganda cha CCM. Wakati magazeti ya Uhuru na Mzalendo yakiwa ni "handouts" za CCM, RTD (na sasa TBC) ikawa ni "mouthpiece" ya chama.

Tangu zamani, waandishi na watangazaji
wa RTD/TBC wamekuwa wanafanyiwa "orientation" ya brainwashing ili waitetee CCM tu bila kutafakari.

Tido alijaribu kubadilisha hii hali lakini akatumbuliwa fasta kwa kutuhumiwa kuwa hakuweka maslahi ya chama mbele.

Sasa Dr. Rioba afanye nini? Hoja hapa ni kwamba ili kuifanya TBC iwe na mvuto kwa wasikilizaji/watazamaji, ni lazima iachane na mwelekeo wake wa kipropaganda. Na katika mazingira ya sasa ambapo kuna vyombo lukuki huru vya habari na mtandao wa internet usiohaririwa, hakika propaganda haiwezi kufanya kazi na kwa hivyo anayewekeza katika propaganda imekula kwake!
Wakitaka kubadilika wanaweza kwa ruzuku wanayoipata nikubwa na fursa walizinazo ni nyingi tatizo nikukubali kuendeshwa toka kwa watu ambao hata taaluma ya habari Hawana nawao wamebweteka
 
Leo mkuu kapiga simu redio Clouds na kusema yake machache na kuwapongeza watendaji wa ATCL na wengineo kwa kazi nzuri wanaoifanya. Hii inamaanisha Mh. Rais ni msikilizaji mzuri wa radio hii na inavyoonekana amevutiwa na ubunifu wao katika kuandaa vipindi.

Ni wazi kuwa kule kwingine hakuna mvuto na ubunifu na hii inaashiria kuwa waliopewa dhamana si wabunifu. Sasa kwanini waendelee kukalia hivyo vyeo?

Dkt. Rioba jipime kabla hujapimwa!

HERI YA MWAKA MPYA
Huenda Mkuu wetu ana Maslahi na Clouds Media sio bure
 
TBC km sekta nyingine za umma ambazo zote zime shindwa kufanya kazi. mana hapa bongo hakuna hata sekta moja iliyo fanya powa so hata ukipewa wewe bado itabuma tu.
 
Mkuu siyo clouds radio bali ni clouds TV kipindi cha clouds 360 ndo mkuu alipiga simu kuwapongeza waandaji wa kipindi na wadau wote in fact hata mm nilivutiwa na Sera au maelezo ya yule jamaa wa atcl alisema "Sikuja Tanzania kufanya kazi ya serikali bali kufanya biashara, nitatuma vijana wangu kwa Mengi,vodacom, kwa bhakharesa etc wakajifunze
 
Back
Top Bottom