Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 6,376
- 6,720
Habari za siku nyingi wana jamvi. Naomba niingie kwenye hoja moja kwa moja. Baada ya kufariki kwa John Magufuli ambaye serikali yake 'haikuwa' na uwezo wa kuwatambua na kuwashughulikia watu wasiojulikana ambao walitesa na kuua watu wetu wengi, sasa ni wakati muafaka wa kuwaumbua na kuwajua wale wasiojulikana. Ni wakati muafaka kwa wana jamvi na watanzania wote kuanza kuwaweka hadharani wale wote waliotenda maasi kwa kisingizio cha kutojulikana wakati wanajulikana. Mie naanza na kumtaja mmojawapo ambaye ni Daudi Bashite aka Paul Makonda. Je wewe unaye wa kuongezea kwenye expose hii? Ushahdi kuhusiana na Bashite ni namna alivyokuwa akijibizana na wahanga wa maangamizi pale walipojaribu kulalamika. Tuanzie hapa.