Ni vyema serikali, Wananchi tukatambua ugonjwa wa akili na viashiria vyake

Manifestation

Senior Member
Jan 22, 2020
193
315
Kwanza ugonjwa wa akili ni kitendo cha kuanzia kufanya matukio kinyume na utaratibu na Kwa kujiamini sana bila wewe kujijua unakosea Ila jamii inakuona wewe unakosea, unaweza ukawa unasikia sauti za watu wanakuita Ila huwaoni, unaweza ukawa unajibizana na sauti ambazo huzioni, unaweza ukawa mhubiri WA uongo ukawa unatamka maneno ya kwenye biblia na Qur'an amabayo hayaendani na ukweli.

Changamoto kubwa kwetu Tanzania ukiugua ugonjwa WA akili watu wanaanza kusema umelogwa na kubatiza majina kama saa mbovu/ dish limeyumba/ kichwa/ hajielewi nk Ila ukweli wa dhati huu hi ugonjwa kama magonjwa mengine na unatibika kama unavyoona malaria; kaswende na mengine mengi yanayotibika kutegemea umekuathiri kiasi na sababu zilizofanya upate na kama unaendelea kujihatarisha Kwa kuendelea na visababishi kama pombe/ sigara/ bangi/ msongo/ kujitenga na jamii.

Kwa uzoefu wangu baada ya kuugua ugonjwa huu na kupona unaweza ukawa unatukana serikali au kusifia; unaweza ukawa unahubiri injili ya kweli au ya uongo, unaweza ukawa unaongea Mambo ambayo hayapo kabisa, unaweza ukachoma vyeti vyako vyote, unaweza haribu vitu vya nyumbani, unaweza ukachoma Qur'an, biblia, unaweza ukavua nguo zako zote barabarani; unaweza ukawapiga watu, unaweza ukawa na overdriving kila mahali unapita kama upo na gari, unaweza unapita katikati ya barabara na unakimbia kuface mahari.

wagonjwa wa akili Wana Mungu sana na huwa mara nyingi wengi wanakuwa na wito na hawatembei katika wito ndio maana wanapata misukosuko ili waweze kujijua wao ni WA kina Nani na wanatakiwa wafanye nini.

Sababu ya kuandika ujumbe huu ni baada ya kuona Jana mtumishi WA serikali amefukuzwa kazi Kwa sababu ya kuchana Qur'an, Ila ukimuangalia kwa makini yule jamaa aliyechana Qur'an hayupo Sawa na akienda polisi huko anaweza akaambulia kipigo na mateso na ukakuona jamaa yupo Sawa Ila kama ukimuangalia kwa makini na kumtuatilia sana utakuja gundua Yule ni mgonjwa.

Mfano wa watu wengine ambao Nina hakika nao ni wagonjwa WA akili ni Dr shika & mchungaji/nabii Tito hawa ni wagonjwa wanaotembea barabarani ni wa kuwaangalia sana sio WA kutengwa wala kunyanyapaliwa na vizuri jamii ikawaweka karibu ili waweze kutengamaa Huku wanatibiwa katika hospital za karibu Yao,.

Nilitibiwa muhimbili nikapona Kwa dawa ziitwazo olanzapine n haloperidol kama utakuwa na maswali kuhusiana na ugonjwa huu Kwa uzoefu ninaweza kushare ili kuweza kupanua uelewa.
 
Wewe Waziri Pamoja Na Kumsimamisha Kazi, Mimi Namfukuza Kazi. Mwandikie Barua Ashinde/Ashindwe Kesi Siyo Mtumishi.

Hatuwezi Kufanya Kazi Na Watumishi Wapumbavu
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
😗😑🤨😶😏😐🤔😉✍
 
Yule jamaa alihitaji msaada badala ya adhabu ya kifo (termination). Kibaya zaidi hata ikithibitika alikuwa insane basi hatarusiwa tena maana aliye juu ya sheria ameshatoa tamko la kujiongezea political popularity.

Inauma sana kwa mtu ambaye alipaswa kuwa mfano wa kuigwa katika kufuata sheria lakini bila hata chembe ya aibu anatoa tamko la kisiasa lenye mrengo wa kutafuta umaarufu at the expenseya MGONJWA WA AKILI.

Tanania bado tuna safari ndefu ya kuendelea.
 
fokonola bokoyoka,
Dhana ya utambuzi wa mtu mwenye matatizo ya akili ina utata sana,kwani kila jamii/mtu wana mitizamo yao juu ya "mwenye akili". Sikiza mtazamo huu; "Mtu mwenye akili ni ametambua lengo la kuumbwa kwake na kuishi kwa kufuata maelekezo ya Muumba. Wasiokuwa hivyo woote wehu!
 
Mtoa hukumu nae aende hospitali kuna dalili nyingi umezitaja zinamhusu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mi sipo hapo Mkuu, Yule ana madaktari wanamsaidia Ila kuna kitu kimoja naweza mshahuri kama ni kweli Halali kisa sijui ni mzalendo au anapewa taarifa ni vitu vya kuacha au kupumzika, vizuri akawa anapewa brief asubuhi awape watu mamlaka ya kuamua
 
fokonola bokoyoka,
Ni kweli bro, jamaa atakuwa ndo kashatoka kwenye reli ya serikali ingawa ninajua jamaa hatofeli maisha maana wengi wanaopata changamoto ya akili wakipona wanaenda kwenye wito na vipawa vyao
 

  1. Dhana ya utambuzi wa mtu mwenye matatizo ya akili ina utata sana,kwani kila jamii/mtu wana mitizamo yao juu ya "mwenye akili". Sikiza mtazamo huu; "Mtu mwenye akili ni ametambua lengo la kuumbwa kwake na kuishi kwa kufuata maelekezo ya Muumba. Wasiokuwa hivyo woote wehu!
SASA kuna Ile Hali ya kutokuwa kawaida, kuanzia kuongea/kujibizana mwenyewe, kutopata usingizi, kutukana, kuvua nguo, nk
 
Hata mimi nina muheshimu sasa huoni anaingilia uhuru wa mahakama Waziri mwenye dhamana alichukua hatua stahiki za kumsimamisha kazi akimanisha kuwa yawezekana jamaa kapatwa na wenda wa zimu sasa yeye kaja na conclusion ndo maana rais wetu anaanza kuvuma kimataifa kwenye mambo ambayo yanaweza kuepukika.
Ni vizuri kuheshimu kiti chake Mkuu, Ila ni ukweli ushahuri ni WA muhimu sana, watu wengi wanaweza wakawa wanajipendekeza bila kumwambia ukweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe Waziri Pamoja Na Kumsimamisha Kazi, Mimi Namfukuza Kazi. Mwandikie Barua Ashinde/Ashindwe Kesi Siyo Mtumishi.

Hatuwezi Kufanya Kazi Na Watumishi Wapumbavu
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
😗😑🤨😶😏😐🤔😉✍

Nina mashaka kuwa hata jiwe anaweza kuwa mgonjwa wa akili.
 
Back
Top Bottom