Ni vibaya binti kumnunulia baba yake boxer?

Ni vibaya binti kumnunulia baba yake boxer?

Serikali ya familia yako unaijua wewe vizuri kuliko mtu yoyote, unajua preferences na dos and don'ts za familia yenu, kumbuka Taboo kwangu au kwa yule sio Taboo kwako...
 
Na umesema pia shemeji yetu(mumeo) huwa anamnunulia mama yake nguo za ndani au sijaelewa? kama nimeelewa basi ni dharau kwa bi.mkubwa kabisa.

simaanishi nguo za ndani zawad nyingine tu kama vitenge viatu n.k
 
Wana MMU naombeni msaada wa ushauri..
Kabla sijaoewa nilikua na tabia ya kuwanunulia wazazi wangu zawad mbalimbali..mfano nikimnunulia mama vitenge au makatalogi yaliyotoka baba nae humnunulia mashati, suruali, viatu, mikanda n.k nikinunua underware za mama na nguo nyingine za ndani bas na baba namnunulia vilevile boxerz, pants,vest n.k na huzipeleka kwa pamoja..walikua wameshazoea na kuzifurahia zawad..na nilifanya hivi kwa muda mrefu tu na nlikua sina ubaguz wa mzaz yeyote.wote wanapata.
baada ya kuchumbiwa pia sikuacha hata mchumba wangu aliona wakat nanunua zawad.hizo na wakat mwingine tunachagua wote nae akimnunulia.mama yake.

Baada ya.kuolewa sasa..siku moja nikanunua kama kawaida makadet na mashati pamoja na nguo za mama na wakwe zangu kama zawadi nikamwita mdogo wangu aje dukani kuchukua za wazaz wangu awapelekee.sasa rafiki yangu nliekua nae akanambia unafanya nini? unamnunulia babako nguo mpaka leo? wewe mke wa mtu acha mke wake (mama yangu) amnunulie! hutakiwi kumnunulia tena! mnunulie mama tu! mh na.maneno mengi tu aliongea yaliyonikatisha tamaa mpaka ikabidi nisitishe zawad hizo mpaka leo sijawahi tena kuwanunulia sio baba wala mama kwani naogopa kumpa mama bila baba kwani nilishazoea kuwapa wote.

Nauliza jamani;: kuna ubaya wowote kwa binti alieolewa kumnunulia baba yake zawadi kama nguo na nguo za ndani n.k?
sina amani najisikia vibaya kwani wazaz wangu wataona nimewatelekeza tangu niolewe hakuna zawadi tena..naombeni mnisaidie wale wenye uzoefu na haya mambo jamani.

Kwani wewe umekulia wapi? hizo tamaduni sio zetu baba yako mpe hela atanunua mwenyewe.
 
umnunulie babako boxer na mamako afanye nn?c bure kuna namna hapa.inamana ww unajua size ya kiuno cha baba ako kuliko mama ako anavyomjua.fanya ukafunzwe

simaanishi hivyo wala sina nia mbaya..jujua viuno vya suruali si tatizo kwani nauza nguo na najua kama anavaa 38 kiuno bas boxer itakua size gani..ndo maana nikauliza kama ni vibaya kumnunulia mzazi mavazi yeyote ni kosa haijalishi ya ndani ama ya nje
 
Rukhsa hata mama mtoto wa kiume kumpelekea bikini haina tatizo. Jaribu uone baraka zitakavyomiminika...
 
Nadhani zawadi si lazima iwepo boxer, waweza kununua vitu vingine na bado daddy yako akafurahi na kukupa kheri.

Ila swali kama hilo jaribu kumuuliza mama yako, kama yeye anaona ni sawa, unaweza kununua.

Asante ndugu..mimi zawadi zote humpa mama nae ndo huchukua zake zingine humpa baba..nia yangu nliona kama nafanya usawa..kumnunulia mama underware na bra nkaona baba nae apate viboxer na vest..na mama hajawah kunigombeza ama kunikataA zaid huambiwa asante tu..ila kwa mawazo ya wengi naona nguo za ndani ndo shida ila nyingine kama mashati au trousers ni sawa..
 
Zawadi zoteee sawa ila sio zinzolinda nyeti za mtu. Hapa ni lazima mhusika mwenyewe ahusike. Kwa mama bado unaweza kumnunulia. Nguo za ndani kwa baba zinaweza kuleta suala la research!

asante ndugu nitaacha kabisa sikujua kama nlikua nafanya kosa
 
Wewe mtoto umejuaje size ya chupi ya baba yako....????????...........

jamani nina uzoefu wa kuuza nguo hasa za kiume so wanaume wanaovaa viuno mbalimbali nao huwauzia boxer na underware pia so nlishajua mtu anaevaa kiuno 38 boxer za turkey size XXL au 43 inamtosha kabisa..na ndivyo nlivogundua kiuno gani kitamtosha..sina nia yeyote mbaya na mzazi wangu huyo nawapenda wote na ninawaheshimu.nimelelewa maadili mazuri na wala sijakulia mjini..sikujua ni kosa miaka yote hiyo mpaka nlivokuja kuambiwa ni kosa..na kwakua nimegundua ni kosa bas sitarudia tena...
 
Mimi naona ingekuwa kosa basi mama yako ndo angekuwa mtu wa mwanzo kukukataza...anyway wengi wape acha kununua hizo boxer
 
Mimi naona ingekuwa kosa basi mama yako ndo angekuwa mtu wa mwanzo kukukataza...anyway wengi wape acha kununua hizo boxer

asante ndugu kwa mawazo ya wengi nayazingatia sikujua kama ni kosa na kwakua sasa nimegundua nilikua nafanya kosa nitaacha.
 
Wana MMU naombeni msaada wa ushauri..
Kabla sijaoewa nilikua na tabia ya kuwanunulia wazazi wangu zawad mbalimbali..mfano nikimnunulia mama vitenge au makatalogi yaliyotoka baba nae humnunulia mashati, suruali, viatu, mikanda n.k nikinunua underware za mama na nguo nyingine za ndani bas na baba namnunulia vilevile boxerz, pants,vest n.k na huzipeleka kwa pamoja..walikua wameshazoea na kuzifurahia zawad..na nilifanya hivi kwa muda mrefu tu na nlikua sina ubaguz wa mzaz yeyote.wote wanapata.
baada ya kuchumbiwa pia sikuacha hata mchumba wangu aliona wakat nanunua zawad.hizo na wakat mwingine tunachagua wote nae akimnunulia.mama yake.

Baada ya.kuolewa sasa..siku moja nikanunua kama kawaida makadet na mashati pamoja na nguo za mama na wakwe zangu kama zawadi nikamwita mdogo wangu aje dukani kuchukua za wazaz wangu awapelekee.sasa rafiki yangu nliekua nae akanambia unafanya nini? unamnunulia babako nguo mpaka leo? wewe mke wa mtu acha mke wake (mama yangu) amnunulie! hutakiwi kumnunulia tena! mnunulie mama tu! mh na.maneno mengi tu aliongea yaliyonikatisha tamaa mpaka ikabidi nisitishe zawad hizo mpaka leo sijawahi tena kuwanunulia sio baba wala mama kwani naogopa kumpa mama bila baba kwani nilishazoea kuwapa wote.

Nauliza jamani;: kuna ubaya wowote kwa binti alieolewa kumnunulia baba yake zawadi kama nguo na nguo za ndani n.k?
sina amani najisikia vibaya kwani wazaz wangu wataona nimewatelekeza tangu niolewe hakuna zawadi tena..naombeni mnisaidie wale wenye uzoefu na haya mambo jamani.
Nguo za ndani unaruhusiwa kumnunulia ila unatakiwa usimpe mkononi ukifika pale kwake unamrushia na wewe unaondoka halafu unaenda tena kwake baada ya wiki.
 
Nguo za ndani unaruhusiwa kumnunulia ila unatakiwa usimpe mkononi ukifika pale kwake unamrushia na wewe unaondoka halafu unaenda tena kwake baada ya wiki.

asante kwa mawazo yako ila kuyazingatia ni ngu..ila naomba uweke heshima.ingekua ni swala la utani ningepeleka chitchat..
 
Kibongobongo wengine wanaona mishe, nlivokua korea ni kama tradition mtoto wa kike na kiume wote wakipata mshahara wao wa kwanza wanawanunulia wazazi wao nguo za ndani...
 
yeye ameshawahi kukununulia sidiria na ch*pi akakupa wakati huu ukiwa mtu mzima. Kama hajawahi jiulize kwa nini?
 
simaanishi hivyo wala sina nia mbaya..jujua viuno vya suruali si tatizo kwani nauza nguo na najua kama anavaa 38 kiuno bas boxer itakua size gani..ndo maana nikauliza kama ni vibaya kumnunulia mzazi mavazi yeyote ni kosa haijalishi ya ndani ama ya nje
wala hatujakuuliza km unauza ama huuzi nguo.ww elewa ni makosa acha ubishi
 
Back
Top Bottom