Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,707
Nimelazimika kujiuliza maswali mengi zaidi leo alfajiri baada ya tukio la kusikitisha; usiku wa leo saa tano nikiwa nimelala niliamshwa ili kumkimbiza hsptl bint aliyekunywa betri acid baada ya aliyekuwa boyfriend wake kumuacha huku akidai bado "anampenda" hivyo kuamua kunywa acid hiyo iliyoutoa kikatili uhai wa binti huyo aliyekuwa anatarajiwa kujiunga na chuo.
Kwani kabla hajakata roho alfajiri ya leo alikuwa anatapika utumbo na vingine vingi, binti huyu alidai upendo ndo ulimpelekea kujitoa uhai kikatili kwani ndivyo alivyokuwa anasema katika masaa machache ya mwisho ya uhai wake na tunamzika leo saa saba.
Hivi upendo una ukatili huu au ni tafsiri yetu mbovu ya upendo? Hebu tueleze wewe unajua nini kuhusu UPENDO ili utusaidie kupunguza majanga haya au kuyamaliza kabisa, binafsi siamini kama upendo unaweza kumpelekea mtu kushindwa kujithamini na kuwathani wengine pia!
Tafadhali naomba maoni au tafsiri yako uwasaidie wengine na tatizo hili.
Kwani kabla hajakata roho alfajiri ya leo alikuwa anatapika utumbo na vingine vingi, binti huyu alidai upendo ndo ulimpelekea kujitoa uhai kikatili kwani ndivyo alivyokuwa anasema katika masaa machache ya mwisho ya uhai wake na tunamzika leo saa saba.
Hivi upendo una ukatili huu au ni tafsiri yetu mbovu ya upendo? Hebu tueleze wewe unajua nini kuhusu UPENDO ili utusaidie kupunguza majanga haya au kuyamaliza kabisa, binafsi siamini kama upendo unaweza kumpelekea mtu kushindwa kujithamini na kuwathani wengine pia!
Tafadhali naomba maoni au tafsiri yako uwasaidie wengine na tatizo hili.