Baada ya kuchoshwa na tuhuma nyingi zinazoelekezwa kwake kupitia magazetini, muda mfupi uliopita spika samwel sitta amesema tuhuma hizo zinapikwa na watu wasiompenda wakiyatumia magazeti ya tanzania daima na tazama. Huko nyuma tuliwahi kusikia kuwa wahariri wa gazeti la tanzania daima (absalom kibanda na charles mulinda) wamenunuliwa na mafisadi wakiongozwa na r.a. Ili kuwashambulia maadui zao, akiwemo spika sitta. Hawa wamekuwa pia wakilitumia pia jamvi hili la jf kupenyezaa upuuzi wao. Akizungumza kwa kujiamini spika ameonyesha kukerwa zaidi na tuhuma kwamba anapanga njama za kuchoma ofisi za bunge ili kuharibu ushahidi wa baadhi ya tuhuma. Sasa amemuomba waziri mkuu amuongezee ulinzi kwani anadhani watu hao ni hatari.