Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Sisi ni wafanyakazi wa Bunge la Jamhuri ya......
Hii sentensi si sahihi...labda ungesema.....''sisi baadhi'' ungeeleweka zaidi kwa sababu hapo chini kuna baadhi yao mnawatuhumu tayari so definately hao wakoexcluded!
Tunaomba watanzania waelewe kuwa kuanzia sasa ofisi hizo zitaungua moto wakati wowote. .
Isije kuwa mna mpango wa kuchoma moto kujustify madai yenu......!

.....imekuwa ikikaliwa na mafisadi wanaojificha katika jina la vinara wa mapambano dhidi ya ufisadi, na kiongozi wao wa Mkuu ni Spika wa Bunge, Samuel Sitta.
Mmejificha hivi tena bado mnaogopa? taja majina.....pamoja na ufisadi wao bana....acha umbea vinginevyo!

Analazimisha kupatiwa fedha kutoka katika ofisi ya bunge anapokuwa katika ziara zake binafsi katika Jimbo lake la Urambo Mashariki. Ushahidi wa haya upo katika vocha za malipo haya. Tunaomba wakaguzi waje wakague watakuta haya
Kupatiwa fedha kivipi? Kama masurufu au kama malipo yake halali au kama advances/loan au kama any other benefits.....elezeni vizuri hapo, kama hamjui taratibu za pesa tulia!

*Spika Sitta amekula akilazimisha kukiukwa kwa kanuni za bunge ili tu kuwapa nafasi wabunge wenzaki walio katika kambi moja kuisulubu serikali ili kuwaaminisha wananchi serikali ni ya hovyo bali yeye na wabunge hao ndiyo wana uchungu wa kweli na taifa hili.
Huu ni umbea kabisa.....wabunge wote niliowasikia ''wakiisulubu serikali''walifanya hivyo kwa sababu za wazi kabisa....kama Richmond, Radar, Twin tower, Buzwagi etc....na ni ukweli kuwa serikali yetu ni hovyo kwa sababu imeshindwa kupambana na ufisadi na kuwainulia kipata na maisha bora wananchi wake!

*Spika Sitta hafuati taratibu za uchukuaji fedha za ofisi. Huwa anaamrisha apewe hata fedha za kununua vifaa muhimu vya ofisi akiwa hana fedha na anapokuwa akizihitaji. Fedha zilizopotea kwa njia ni mabilioni, lakini hakuna anayemuhoji.
...Haya maneno yenu yamekosa mfupa kabisa......totally umbea!

*Spika Sitta hata siku moja tangu aliposhika wadhfa huo, amekuwa hafuati taratibu za kawaida za sheria ya manunuzi umma katika mambo mengi hapa bungeni. Yota haya ushahidi wake upo ofisi ya uhasibu lakini analindwa na kundi la wabunge wanaodai kuwa wanapoambana na ufisadi kwa* sababua anakula nao.
Rejea hapo juu...hakuna kitu kama hiki....kweli tangia aingie madarakani....HAFUATI kabisa sheria za manunuzi? kuna weza kuwa na kasoro...lakini si kwa kiasi hiki!
*Spika Sitta ameshinikiza kukodishiwa nyumba ya gharama kubwa. Dola za Marekani 8,000 kwa mwezi wakati alikuwa amepewa nyumba nzuri tu ya serikali huko Oysterbay. Baada ya kukodishiwa Nyumba hii, alilazimisha pia Ofisi ya Bunge itoe sh milioni 250 kwa ajili ya kununua samani za ndani alizodai kuwa ndizo zinazolingana na hadhi yake ya Spika.
Hili limeshajadiliwa sana hapa JF .....rejea michango ya members kny thread husika!

*Spika Sitta ambaye baada tu ya kuingia katika wadhfa wake alinunuliwa gari jipya aina ya benz. Sasa amelichoka likiwa hata halijamaliza miaka mitatu, anataka kununuliwa jingine na amekwishamuarua Katibu wa Bunge, Thomas Kahililah ambaye ni swahiba wake mkubwa kwa sababu wanakula pamoja kutoa kiasi cha sh milioni 367 kwa ajili ya kununulia gari hilo . Tayari zimekwishalipwa sh milioni 270. wakati haya yakifanywa na Spika, anajua fika kuwa taifa liko katika hali mbaya kifedha na bunge liko katika hali mbaya zaidi kiasi kwamba vikao vyake vinakatishwa.
Kama hayo madai ya kununua gari la zaidi TZS 360 ni kweli....hapa kuna concern kubwa sana ya viongozi wetu kuhusu suala la kupambana na umasikini.

Hata na hivyo hii imekuwa ndo trend ya viongozi wetu wote wa ngazi ya juu. Ebu niambie, kiongozi gani wa ngazi ya juu TZ unayemfahamu ambaye hajabadili gari lake tangia aingie madarakani 2005?....so nothing new here!

*Spika Sitta ana sifa mbaya ya ukware. Tangu ameshika wadhfa huo amekwishatembea na wabunge wanawake wa bunge la Jamhuri ya Muunagni ambao ni wake za watu zaidi 12 na ushahidi wa hili upo kwao wenyewe wabunge. Akikanusha hili tunaomba watumwe maofisa usalama waje wafanye uchunguzi kwa siri, watabaini jinsi anavyofanya ufirauni na wake za watu ambao ni wabunge. Anatembea mpaka na wabunge wa upinzani halafu anajitapa kuwa ni Spika wa wote hivyo lazima awalee. Ni aibu lakini huo ndio ukweli.
Nyie mlikuwa mnashikilia miguu ya hao wanawake eeeh? au nyie ni washenga? Hata kama ni kweli, je, hao wanawake wanabakwa au wanakubaliana? acha kutuletea Ze utamu hapa bana!

*Ni mtu anayevidhalilisha vyombo vya ulinzi na usalama kwa sababu amekuwa akisema wazi kuwa hakuna chombo chenye nguvu za kumchunguza yeye na bunge kwa sababu bunge ni dola.
Kama vyombo hivyo havijui kazi zao.....vinajidhalilisha na kudhalilishwa kwa kufindishwa what they are supposed to be doing!
Na ukweli sasa umeanza kubainika kwa sababu ni dhahili kuwa serikali inamuogopa Spika na timu ya wabunge wake.
Safi sana kama this is true aisee!

Ndiyo maana licha ma malalamiko na ushahidi mwingi tuliokwishatoa toa kuhusu ufisadi wake, si TAKUKURU, polisi waka usalama wa taifa waliothubutu hata kumuhoji.
Ushahidi upi waungwana? .....hayo maneno yenu ya umbea ndo mnayaita ushahidi eeh?

*Spika amewagawa wafanyakazi wa Bunge wa Idara ya Uhasibu. Wapo ambao amewateua kuwa watu wake ambao wanashughulika na malipo yake yeye, makamishina wa tume ya huduma ya bunge ambao wanakula naye pamoja, pamoja na wabunge kadhaa ambao uchunguzi wa kina ukifanyika watafahamika.
...nyie kama mpo utawala, au mipango au huduma za bunge...acheni kuwaonea wivu wenzenu wa uhasibu...! Kama kuna mhasibu anamhudumia spika wholly & exclusively hii ndo nzuri zaidi....inaonyesha kuna umakini kwa upande wa spika kuhakikisha pesa zinakuwa properly accounted for!

*Wahasibu hawa pamoja na Kashililah ndiyo wanaolipwa mishahara mikubwa,
Kama wamekuzidi cheo na uzoefu kazini ni dhahiri watalipwa zaidi yako mkubwa!
wanalipwa posho hata kama hawakufanya kazi za ziada
hili halina ushahidi kabisa!
na wanasafiri na Spika kila anapokwenda nchi za nje.
Hili si kweli....yaani kila spika akienda nje anaenda na delegation yote hiyo ya wahasibu for what?
 
Naona kama ni majungu yanapikwa alivyogusia kuwa anaurafiki na wabunge wa Kambi moja kusudi waongee bungeni kuhusu ufisadi ..... hawa watu watakuwa wamechanganyikiwa kama sio kupunguzwa au watakuwa wamebadilishwa nafasi zao iko namna. Spika ni Mtu mkubwa sana na anaheshima zake, waache kuchafua watu, Ovyo

Mtoa hoja kasema pamoja na utitiri wa maneno yenye mtiririko wa kuelezea kinachotokea. Kwa wahasibu wameelewa kinachotokea na inawezekana kutokea kwani viongozi wengi walio ngazi za juu huwa hawapendi kufuata sheria za fedha na manunuzi kwani ni kama kwamba wanaona wapo juu ya sheria, na hii inatokana labda na wao kuziona au kufahamishwa ukubwani. Kikubwa mtoa hoja ajaribu kuthibitisha kwa japo vielelezo kadhaa.
 
Kama ndugu zetu mmehamua kutoa shutuma nyingi kiasi hiki na nyie mpo ndani ya hiyo ofisi nyeti, mbona hamjatupenyeshea viambatanisho muhimu ambavyo tutavitumia kama vielelezo kuliko maneno matupu?

Tunasubiri ili tuweze kuwaelewa vinginevyo!
 
Lol! Hii ni kali. Inawezekana ukawemo ukweli katika baadhi ya mambo lakini naona limekaa kama bomu la kumlipua spika. Maana amekuwa mwiba kwa mafisadi kwa kuruhusu hoja nzito zunazowahusu zijadiliwe kinyume na matarajiao yao ya wana CCM kulindana. Hilo la kuchoma moto ni hatari na vyombo vya ulinzi na usalama vinapaswa kuilinda vyema ofisi hiyo maana isijekuwa hawa watu wanataka kuchoma moto hiyo ofisi kuthibitisha tu haya madai yao.

Hoja imekosa nguvu sana kwa kuwashambulia wabunge waliomstari wa mbele kuichachafya serikali katika utendaji wake mbovu maana hawakufanya hivyo from no where bali kwa mifano hai.
Kaaazi kwelikweli.
 
bora sie mchungaji wetu amekutwa na viungo vya albino...kwi kwi kwi kwi
Hivi mnashikilia hayo ya mchungaji wa albinooooo, hadi lini, hivi si iko obvious kabisa kuwa waislam ndo wenye dini ya kichawi na mashetani? nani hajui kuwa kwa kutumia koran mtu anao uwezo hata kutengeneza jini lake yeye mwenyewe?

na je, vipi yule shehe wa kibaha aliyeshikwa ameweka kichwa cha mtu ndani ya chumba chake, amekiingiza kwenye mafuta ili kisinuke? tumenyamaza tu kwasababu tunajua kwa waislam hakuna jipya,ni uchawi na ukatili kwenda mbele kwao, ndo dini yao. cha maana ni kwamba, mtu awe mkristo au mwislam kama ni mchawi basi huyo mtu ni mbaya. na hii haiwezi kukwepeka kuwa shehk wenu msoma nyota ni mchawi,mla watu na mwenye mabaya yoote hapa dunian. siku zake ziko kwenye kiganja hata hivyo. Mungu atamwondoa hapa tz, na hamtamsikia tena.
 
Nina imani kubwa kwamba, nia ya Pengo ya kutoa waraka huo ni kutetea masilahi ya Wakristo," alisema Sheikh Yahya.

Wasaalam!

Na lengo kubwa la Mahakama ya Kadhi ni kutetea masilahi ya waisilamu?

Chakushangaza hakuna mwenye kuwa na masilahi ya 'Mtanzania'?

Sasa hizi purukushani za kuvaana...tetetetthhhhee😛

Karibu kinaiva!
 
ALELUYAH!
SHALOM!
Ndugu zangu wana JF nikiwa natamani kwenda kwa Chakula cha mchana nika enjoy Chapati kwa samaki mara email inaingia ikiwa na ujumbe huu, nami naona kuwa mahali pake ni hapa ili tuudadadue na tuupembue kwa kina tuone kama mambo haya ni kweli au la. Kwa ufahamu wangu naona mzee wetu huyu tunayemheshimu sana Mr Six hawezi fanya haya kwani anaonyesha anauchungu na nchi yake na ndiyo sababu Bunge lilimpa dhamana ya kuliongoza hili behewa ambalo ndilo injine ya taifa. Soma mambo haya hapa chini.Kama nimefanya vibaya kuuleta ujumbe huu hapa naomba mnikosoe jamani!

Kama Mungu wangu aishivyo nawatakia kila la kheri kwenye hili tulinusuru taifa letu.
Mungu wangu na awabariki sana

 
Haya tunaweza kuyaweka kwenye kundi la "majungu Kazini" + "Kitchen sink politics". Ili hii e-mail iwe na uzito hawa wanaojiita wafanyakazi walitakiwa kuscan hizo docs za ufisadi zinzotarajiwa kuchomwa kama walivyodai na kuzi-attach kwenye hii e-mail kama proof of their allegations. kama wanajua ofisi itachomwa, je wamechukua hatua gani?. Panga la Yesu thanks kwa kuiweka hapa JF, ila naona kama imepwaya vile. Maana hapa ni docs tu ndizo zinazoweza kuwa analysed kwa undani zaidi ya haya maneno ya kwenye vijiwe vya kahawa.
 
dis is terrible japo si ajabu kwa mtu km six kufanya hayo kwani ndo yaliyomkuza,ni aibu tupu kwa bunge, sasa mbona anakuwa mnafiki?au ndo kusema anao ulinzi wa kutosha? hata aibu?bona hatoki hadharani kutetea kulipiwa hse 10mil? tena dodoma?bado furniture ziwekwe? hiyo hse hata states itakuwa ya maana sana! labda beverly!!so kura yenu jamani watanzania tuchague nanai sasa?
 
Tatizo letu kubwa ni dharau, kejeli nk. mtu ametoa data, mwingine anasimama ghafla kidedea kuponda kabla ya kufanya utafiti maana yake nini? faida ya utandawazi ndo huu hakuna cha kuficha wala nini, mzee kama anachemsha ajitokeze mtu wa kukanusha haya na si vinginevyo
 
..kama mwanajamvi ninafarijika kuona JF ikizidi kuaminika na kutumika kama pahala penye wigo wa kuwafikia Watanzania walio wengi.....Ila wasiwasi wangu ni kwamba hili la Mh.Six....WHY NOW????
 
DU nashindwa kuamini au la lakini waswahili wana msemo " Lisemwalo........." na ukisikia maisha aliyokuwa nayo Mr six kabla ya kuokolewa na Muungwana pengine na tutege shikio.
 
Tatizo letu kubwa ni dharau, kejeli nk. mtu ametoa data, mwingine anasimama ghafla kidedea kuponda kabla ya kufanya utafiti maana yake nini? faida ya utandawazi ndo huu hakuna cha kuficha wala nini, mzee kama anachemsha ajitokeze mtu wa kukanusha haya na si vinginevyo

Huwezi kufanyia utafiti maneno ya udaku, unafanyia utafiti documents genuine. Hii e-mail haina credibility wala uzito. Kumbuka hapa halaumiwi "Panga la Yesu", yeye katimiza wajibu wake. Lawama ni source of the e-mail, kwa nini imekaa kimajungujungu tu aweke documents hapa. Usidhani JF watu wote ni very cheap wa kuamini maneno ya kwenye vigenge vya kahawa, hapa ni source au documents.

Vinginevyo huu ni Udaku period. Mimi simfahamu Sitta, wala si shabiki wa chama chochote zaidi ya kuwa shabiki wa haki na uhuru wa kuchagua. Hii e-mail ni maji taka, vinginevyo walete ushahidi wa documents, kama vouchers, pay-slips n.k.
 
hiyo document ilitolewa jana kwenye forum ya mwanakijiji inayoongozwa na administrators wehu kimsingi madai mengi humo ni uzandiki mtupu na ni kampeni ya mafisadi walioumizwa na Bunge including EL na RA AMBAO WAMEUNGANA NA BAADHI YA WATUMISHI WA BUNGE waliokosa vyeo vya ukurugenzi kwenye appointment ya hivi karibuni na vingine vya juu kueneza mambo ya uongo na unafiki tu lakini ukisoma kwa makini utajua uongo wa wazi kwani hakuna any bold evidence ya kuthibitisha hayo .
 
Huwezi kufanyia utafiti maneno ya udaku, unafanyia utafiti documents genuine. Hii e-mail haina credibility wala uzito. Kumbuka hapa halaumiwi "Panga la Yesu", yeye katimiza wajibu wake. Lawama ni source of the e-mail, kwa nini imekaa kimajungujungu tu aweke documents hapa. Usidhani JF watu wote ni very cheap wa kuamini maneno ya kwenye vigenge vya kahawa, hapa ni source au documents.

Vinginevyo huu ni Udaku period. Mimi simfahamu Sitta, wala si shabiki wa chama chochote zaidi ya kuwa shabiki wa haki na uhuru wa kuchagua. Hii e-mail ni maji taka, vinginevyo walete ushahidi wa documents, kama vouchers, pay-slips n.k.

Hii iliypletwa hapa inajionesha wenyew. Si kila dai litakuwa well documented au likiwa na vielelezo kamili. Uandishi na yaliyomo yanaonyesha jinsi gani hili suwala si rahisi kutolewa vielelezo kamili la msingi ni kuwa hili dai limekuwa Fair kwa kutaka kufanywe uchunguzi wa wazi wa madai hayo.
Tumekuwa tukipokea madai ya ufisadi hapa na kuyajadili wala huwa hatuna documents. Maadam message imeshafika huo unaouita udaku unaweza ukawa na ukweli ndani yake la muhimu ni kuchunguzwa.
 
Huwezi kufanyia utafiti maneno ya udaku, unafanyia utafiti documents genuine. Hii e-mail haina credibility wala uzito. Kumbuka hapa halaumiwi "Panga la Yesu", yeye katimiza wajibu wake. Lawama ni source of the e-mail, kwa nini imekaa kimajungujungu tu aweke documents hapa. Usidhani JF watu wote ni very cheap wa kuamini maneno ya kwenye vigenge vya kahawa, hapa ni source au documents.

Vinginevyo huu ni Udaku period. Mimi simfahamu Sitta, wala si shabiki wa chama chochote zaidi ya kuwa shabiki wa haki na uhuru wa kuchagua. Hii e-mail ni maji taka, vinginevyo walete ushahidi wa documents, kama vouchers, pay-slips n.k.
watu wajungu utajua tu jamaani mue na ma documento sio mna weka tu vitu ama tuseme muache Tabia ya ku copy na ku paste vihadisi mnavyo okota kama alivyo andika HOFSTEDE ,mimi naona hapa watu wanapakana matope tu kwa ajili ya uchaguzi mwakani 2010 hakuna la ziada. eti wafanyakazi wa bunge lol, moderator funga upuuzi huu
 
Duh,
Mungu aingilie kati mabadiliko yaje, aliyesema watufulani walaaniwe alikuwa sahihi as far as they know each other well....!
 
Back
Top Bottom