Ni sawa wizara kutumia kodi ya wananchi kutumika kwenye mazishi ya Kanumba?

Kuna profesa mmoja pale muhimbili amefariki usiku wa kuamkia jana, ngoja nione responsi ya selikali
 
Kitendo kilichofanyika ni cha busara,kubali ukatae Kanumba amewasaidia kwa njia moja ama nyingine vijana wengi kujiajiri kwa sababu ya kazi zake na pia amelitangaza soko la nchi yetu(la filamu) kwa kiasi kikubwa.usiwe mtu wa kupinga tu mambo ndugu yangu kama kusoma huwezi hata picha huoni,hawezi kuwa kama wewe kiukweli vinhinevyo uniambie ni nin ulishafanya kwa nchi yako chenye manufaa kimataifa

Ni mwalimu huyo! Amefuta ujinga na UPUMBAVU wa watanzania kwa miaka 24 sasa! Alifanyie nini zaidi taifa hili.
 
Hicho kitendo cha serikali kutumia mchango wa wananchi kwny msiba kawaida wa mtu binafsi si shabikii. Ktk hilo serikali iwe makani kesho atafariki msanii mwingine maarufu wasipotoa je?. Tusifanye vitu tu ushabiki 2we watu wa reason kwanza.
 
Sitaki kupuuzia mchango wa Kanumba katika sanaa yake (sanaa na si lazima taifa kwa ujumla). Ila linapo kuja swala la kodi tutambue kwamba kodi ni kwa manufaa ya wananchi wote. Kwa maana si kila huduma lazima imfaidishe kila mtu ila iwe na manufaa kwa taifa. Kwa maana nadhani tuna changanya umaarufu na mchango kwa taifa.

Linapo kuja swala la Kanumba si kwamba pesa zinge kosekana za kuendesha msiba wake. Wasanii wenyewe, ndugu, jamaa na marafiki wange weza pata pesa za kutosha kuendesha shughuli. Kwa hiyo si kwamba serikali imesaidia katika jambo ambalo otherwise linge kwama.

Pia kuna watu kibao ambao wana hitaji pesa kama hizo. Kuna watu hawana chakula, malazi, pesa za ada. Kweli waliona matumizi ya dharura ni kwenye msiba huu?

Piakuna member mmoja kwenye hii thread kasema kitu cha maana sana. Kwamba kuna precedence zingine tuna tengeneza zita leta matatizo. Sasa ina maana serikali itakua ina gharamia misiba yote ya namna hii? Wakifa wasanii wengine wenye kutoa mchango sawa sawa na Kanumba zita tumika pesa za serikali?

Mimi nadhani serikali imetumia ishu hii kisiasa sana. Sikuona haja ya JK kuahirisha safari kwende kuhudhuria msiba wa mtu mmoja wakati haku ahirisha safari wakati wa mgomo wa madaktari walipo kufa mamia ya watanzania. Pia sikuona haja ya viongozi wa kiserikali kujazana pale leaders club.

Anyway najua kuna wengine wata nipinga. Haya ni maoni yangu tu.
 
Mkuu kila binadamu ana both positive na negative side,hivyo tuna judge kwa kutathmini both sides,kimsingi Kanumba amechangia mengi kwa nchi hii,tatizo akili ya binadamu inawaza zaidi negative side kuliko positive that's why wengi wanaponda kila kitu. Wengi wanafanya maovu kama hayo sema hawajagundulika that's why wanaonekana wasafi.
 
Vijana wa siku hizi bana.....

Hivi mtu mwenye akili timamu anaweza kushabikia serikali kutoa 15m kwa mbakaji wa watoto kisa tu eti ni maarufu? Wizara hiyo hiyo imeitelekeza timu ya taifa ya netball na kumchoresha mke wa Pinda kutembeza bakuli la ombaomba kuinusuru timu.....

Kwamba unaweza shabikia mama wa mhuni apewe 15m za kodi yetu wakati mama zetu wanatembea zaidi ya 10km kwenda kutafuta maji machafu vijijini huko?

Nalishangaa sana taifa langu hili....
Serikali legelege utaijua kwa matendo yake.
 
Sitaki kupuuzia mchango wa Kanumba katika sanaa yake (sanaa na si lazima taifa kwa ujumla). Ila linapo kuja swala la kodi tutambue kwamba kodi ni kwa manufaa ya wananchi wote. Kwa maana si kila huduma lazima imfaidishe kila mtu ila iwe na manufaa kwa taifa. Kwa maana nadhani tuna changanya umaarufu na mchango kwa taifa.

Linapo kuja swala la Kanumba si kwamba pesa zinge kosekana za kuendesha msiba wake. Wasanii wenyewe, ndugu, jamaa na marafiki wange weza pata pesa za kutosha kuendesha shughuli. Kwa hiyo si kwamba serikali imesaidia katika jambo ambalo otherwise linge kwama.

Pia kuna watu kibao ambao wana hitaji pesa kama hizo. Kuna watu hawana chakula, malazi, pesa za ada. Kweli waliona matumizi ya dharura ni kwenye msiba huu?

Piakuna member mmoja kwenye hii thread kasema kitu cha maana sana. Kwamba kuna precedence zingine tuna tengeneza zita leta matatizo. Sasa ina maana serikali itakua ina gharamia misiba yote ya namna hii? Wakifa wasanii wengine wenye kutoa mchango sawa sawa na Kanumba zita tumika pesa za serikali?

Mimi nadhani serikali imetumia ishu hii kisiasa sana. Sikuona haja ya JK kuahirisha safari kwende kuhudhuria msiba wa mtu mmoja wakati haku ahirisha safari wakati wa mgomo wa madaktari walipo kufa mamia ya watanzania. Pia sikuona haja ya viongozi wa kiserikali kujazana pale leaders club.

Anyway najua kuna wengine wata nipinga. Haya ni maoni yangu tu.

well said
 
Duuu aisee kweli kua uyaone, yaani sijawahi kuona nchi yenye watu wenye mawazo mgando km TZ!! Yaani msanii tu serikali inamgharamia mazishi yake du! Hivi wasanii km Michael Jackson, Luck Dube, whitney Houston, Bob Marley, Maria Makeba n.k, Serikali za nchi zao ziligharamia mazishi yao?
 
Jamani mbona sijajibiwa swali langu?nauliza tena. Serikali ya marekani ilitoa sh.ngapi Michael Jackson au whitney houston walipokufa?
kumlinganisha kanumba na hao mabilionea ni sawa na kulinganisha sisimizi na tembo. hao hawakuhitaji msaada wa serikali yao. kanumba was a pioneer, but relatively poor. he deserved what was offered.
 
Kitendo kilichofanyika ni cha busara,kubali ukatae Kanumba amewasaidia kwa njia moja ama nyingine vijana wengi kujiajiri kwa sababu ya kazi zake na pia amelitangaza soko la nchi yetu(la filamu) kwa kiasi kikubwa.usiwe mtu wa kupinga tu mambo ndugu yangu kama kusoma huwezi hata picha huoni,hawezi kuwa kama wewe kiukweli vinhinevyo uniambie ni nin ulishafanya kwa nchi yako chenye manufaa kimataifa

huyo kanumba alisaidiwa vipi na serikali kufikia hapo alipofikia? jibu kama ni ndi,mbona wengine hawapati msaada na jibu km ni hapana bado nitauliza kwa nini huo msaada utolewe sasa wakato muhusika ni marehemu...think!
 
Nimehuzunika sana na kifo cha mpendwa wetu na kijana mwenzangu Steve Kanumba.BUT kunakitu hakijaniingia akilini pale waziri wa vijana na utamaduni alipotangaza kwamba wizara yake itatoa sh.milioni 15 kwa familia ya kanumba,nilimshuudia kwa macho yangu kupitia tv.Then nilisoma gazeti la mtanzania nikakutana na habari inayosma 'serikali itagharamia mazishi yote ya kanumba.'.nauliza je hii bajeti hiyo inatolewa kwenye fungu gani la bajeti ya serikali ukizingatia Kanumba ni raia wa kawaida kama mimi ? Na je huyo waziri alitoa rambirambi yake binafsi?
Ukisikia wizara itatoa jua hapo hakuna ubinafsi! Wazazi wapewe pesa hizo na serikali; za nini? watanzania wangapi wanafiwa tena na watu wanaowategemea lakini serikali haiwasaidii. Ningeielewa serikali kama ingesema itasimamia kuhakikisha wazazi wake wanapata haki kutokana na mikataba yake na kazi zake.
 
Vijana wa siku hizi bana.....

Hivi mtu mwenye akili timamu anaweza kushabikia serikali kutoa 15m kwa mbakaji wa watoto kisa tu eti ni maarufu? Wizara hiyo hiyo imeitelekeza timu ya taifa ya netball na kumchoresha mke wa Pinda kutembeza bakuli la ombaomba kuinusuru timu.....

Kwamba unaweza shabikia mama wa mhuni apewe 15m za kodi yetu wakati mama zetu wanatembea zaidi ya 10km kwenda kutafuta maji machafu vijijini huko?

Nalishangaa sana taifa langu hili....
Serikali legelege utaijua kwa matendo yake.
Hatuna vipaumbele basi. Kila kitu ni siasa.
 
kumlinganisha kanumba na hao mabilionea ni sawa na kulinganisha sisimizi na tembo. hao hawakuhitaji msaada wa serikali yao. kanumba was a pioneer, but relatively poor. he deserved what was offered.

Yeye alisaidiwa vipi ilhali hana uhai? Wasanii wengi ni poor na wanajitahidi kugangamala kama alivyokuwa Kanumba. Serikali ilipaswa kuwasaidia wakiwa HAI kwa kuwalindia kazi zao na kuwasaidia kupromote kazi zao na si kuggaramia mazishi yao pale wanapokufa!

Nafikiri hiyo point unamiss!
 
kuna watu wanashabikia mambo ya kijinga ambayo yameanzia kwa jk nao wanayakubali. Hivi hii si ndo wizara ilifukuzwa nhc kwa kutolipa kodi? Ukienda dawasco na tanesco hawa ni wadaiwa sugu. Leo mnaniambia kuchezea kodi zetu kwa mambo ya mazisho ya mtu asiye na mchango wa kitaifa ni halali! Tusiwe wavivu wa kufikiri kiasi hicho, hivi huo ujinga wanaoufanya unatuingizia dola ngapi kwa mwaka? Serikali nzima imehamia kwenye msiba wa watu waliouana wakizini, na vyombo vya habari vingine hata wakati wa ajali ya meli hawakutangaza lakini leo wamepata airtime? Hawa viongozi mi najiuliza kwenye bajeti walizomia wameandika nini? Ni emergence ngapi za kitaifa zinatokea tunaambiwa hakuna hela? Hospitali ngapi leo hazina ultrasound,dawa,? Rais,makamu,pm,mawaziri vichwa vyao wote vimeoza. Wameshindwa kuwaletea wananchi maendeleo wameamua wawe wanawalisha wali kwenye misiba? Au ndo mwendelezo wa majibu mepesi kwenye maswali magumu? Ndo yale ya tacaids kutaka kodi za vinywaji zipande ili wao wapate za kununulia v8 na kusomesha watoto wao nje huku waathirika wakihangaika na lishe na complications za dawa?Tuacheni kutetea upumbavu,fedha zetu nyingi zimetumika pasipo kufuata matumizi yanayoeleweka. Fedha zenyewe za mkopo bado tunafanyia ujinga. Naomba wafadhili waendelee kujitoa ili tupate akili. Narudia HUU NI UPUNGUANI WA WALE WOTE WALIOTUMIA KODI ZETU KWENYE HUU MSIBA!.

Mapenzi yetu hata yangekuwa makubwa vipi sii sawa kuyatumia kufanya maamuzi ya fedha/mali za umma bila kufuata sheria, kanuni na taratibu. tofautisha na kama fadha zingekuwa ni kutoka kwa Mengi(Mtu binafsi mwenye maamuzi binafsi) bado haiko sawa na tumbuke wingi wa wapenzi kamwe siyo msingi wa maamuzi ya matumizi ya mali ya umma- je, waziri angeweza pia kuipa familia yake nyumba ya serikali kwa sababu alikuwa maarufu na kipenzi cha watanzania?
Lets not be emotional in seeing this point.
 
Mtu wa kawaida tu kama watz wengine, sijaona cha kufanya taifa limwangaikie, hawa wakubwa ukiwaita kuchangia laptop kwa ajili ya chekechea wanatoa elfu 40, lakini wanawachangia wahuni pesa zetu.
 
Hilo la wizara kulipia mazishi ya kanumba si rahisis kuingia akilina ila limefanywa kisiasa mno, watanzania lets try ro wake up nchi yetu bado ni maskini mno tunahitaji maendeleo ya nchi yetu no need of much politics. Amerca nchi yanye maendeleo na wasanii wanaingizi pato marekani kiasi cha dola trilioni 1.5 kwa mwaka lkn hatuwaona kina obama kwenye msiba wa michael jackson, sasa leo every one yuko pale kweli waziri wa utamaduni si yupo na anatosha kuwakilisha kwa niaba ya serikali,,,,. hii ni kero especially pale unatumia kodi za wananchi wakati watoto hawana vitabu wala madawati shuleni hii imefanyika ki campein. na hii serikali iliyokuwa madarakani inaongoza kwa kutumia pesa za wananchi ovyo
 
Back
Top Bottom