Ni sahihi kumkaribisha Muislamu nyama ambayo haikuchinjwa kidini?

Mimi nachinja mwenyewe ukija nakwambia ukitaka kula ukitaka acha......nikija kwako nakula vizuri tu sana mno na sitakufa.....complication nyingine hazifai .....
 
Hilo liko wazi kwa hapa Tanzania. Ninachojiuliza tu ni huwa wanafanyaje pindi wawapo kwenye nchi zisizo na huo utaratibu?

Je, bidhaa imported zilizotokana na nyama kama soseji wanafanyaje?
Ukienda huko unakuwa vegetarian au unakomaa na seafood tu au unatafuta maduka ya halal food
 
Kuheshimu imani ya mtu, hasa katika nchi isiyo na dini, ni suala nyeti sana. Ndiyo maana Watanzania wengi wanapotaka kufanya sherehe, kama si Waislamu, huhakikisha kuwa mchinjaji wa nyama itakayotumika ni Muislamu.

Lakini itakuwaje ikiwa wewe si Muislamu na ukatembelewa ghafla na rafiki Muislamu wakati unamla kuku uliyemchinja mwenyewe?

1. Utamkaribisha kujumuika nawe pamoja na kuwa unajua ulichinja bila kuzingatia imani ya Kiislamu?

2. Utamjulisha ukweli kuwa ulimchinja wewe mwenyewe ili aamue mwenyewe?

3. Utamwambia asubirie umwandalie cha kwake?

Upi utakuwa uamuzi wa busara?
Pombe wanakunywa sembuse nyama tena ya kuku. Wengine hata kitimoto wanakula.
 
kibudu ni mnyama aliyekufa ..Hakuna dini inayoruhusu kula kibudu wala wanyamapori labda Fisi tu.


Nyamafu ni nyama ya mnyama aliyekufa (kibudu) bila kuuliwa kwa asili (yaani kuchinjwa). Mungu aliwakataza wana wa Israeli katika agano la kale wasile nyama ya mnyama yoyote aliyekufa bila kuchinjwa..
Sasa Wakristo wanakula wanyama waliokufa wenyewe au wanachinja? Kwanini Wafia dini wa kiislam hawali nyama ya mnyama aliyechinjwa na Mkristo ilihali sio kibudu?
 
Sasa Wakristo wanakula wanyama waliokufa wenyewe au wanachinja? Kwanini Wafia dini wa kiislam hawali nyama ya mnyama aliyechinjwa na Mkristo?
Uislamu ni mfumo mzima wa maisha ya mwanadamu,una taratibu zake na sheria zake

Ili kichinjo kiwe halal hakina budi kuchinjwa na muislamu ambaye anamwamini Allah mmoja asiyeshirikishwa na yoyoye katika ufalme wake

Kuchinja ni ibada na inataratibu zake,ikiwa ni pamoja na kuelekea kibla wakati wa kuchinja na kutaja jina la Mwenyezi Mungu

Kwakuwa wasio waislamu hawana taratibu hizi basi ni haramu kula mnyama aliyechinjwa nje ya taratibu za kiislamu
 
Hatakufa, lakini unafikiri atakuchukuliaje siku akigundua kuwa ulimlisha "haramu" kwa makusudi?

Masuala ya imani yapo very complicated. Si ya kuyachukulia kirahisi.
Haramu kwa maana kwamba umemlisha nguruwe kwa makusudi au ulikuwa na maana nyengine?

Na kwanini kwanza mimi Mkristo nimlishe kwa makusudi mwenzangu kitu asichokitumia?unadhani sitakuwa na busara ya kuamuru kipikwe chakula kingine kwa ajili yake au iwepo option anywe maji au juice maisha yaende?
 
Uislamu ni mfumo mzima wa maisha ya mwanadamu,una taratibu zake na sheria zake

Ili kichinjo kiwe halal hakina budi kuchinjwa na muislamu ambaye anamwamini Allah mmoja asiyeshirikishwa na yoyoye katika ufalme wake

Kuchinja ni ibada na inataratibu zake,ikiwa ni pamoja na kuelekea kibla wakati wa kuchinja na kutaja jina la Mwenyezi Mungu

Kwakuwa wasio waislamu hawana taratibu hizi basi ni haramu kula mnyama aliyechinjwa nje ya taratibu za kiislamu
Sawa, sio vibaya wasipokula
 
Kuheshimu imani ya mtu, hasa katika nchi isiyo na dini, ni suala nyeti sana. Ndiyo maana Watanzania wengi wanapotaka kufanya sherehe, kama si Waislamu, huhakikisha kuwa mchinjaji wa nyama itakayotumika ni Muislamu.

Lakini itakuwaje ikiwa wewe si Muislamu na ukatembelewa ghafla na rafiki Muislamu wakati unamla kuku uliyemchinja mwenyewe?

1. Utamkaribisha kujumuika nawe pamoja na kuwa unajua ulichinja bila kuzingatia imani ya Kiislamu?

2. Utamjulisha ukweli kuwa ulimchinja wewe mwenyewe ili aamue mwenyewe?

3. Utamwambia asubirie umwandalie cha kwake?

Upi utakuwa uamuzi wa busara?
Karibu sana. Huyu kuku nimemchinja mwenyewe. Pole sana ngoja nikuandalie mabamia
 
Muislam anaruhusiwa kula alichochinja asiyekuwa Muislam. Ila tu mchinjaji awe amechinja kweli. Wasio waislam wana tabia ya kuwapiga wanyama au kuku wanamtumbukiza kwenye maji moto anakufa kisha wanaanza kumkata kata. Muislam hali kibudu tu, kitu ambacho hakikuchinjwa. Kama umechinja vizuri kabisa yafaa kula.
Kuna shida Gani?

Kuchinja sio kuua?

Unajua logic za Dini sometimes ni ujinga sana😂😂😂 so ua Lakini ua kistaarabu
 
Back
Top Bottom