Ni rahisi kwenda kuliko kurudi

Ni rahisi kwenda kuliko kurudi

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,520
Reaction score
830,064
Waulize watalaka na watalikiwa watakuambia. Kwenda kwenye ndoa ni rahisi kuliko kurudi kwenye ndoa baada ya kuondoka kwenye ndoa.

Kijana wangu alipewa suspension shuleni nikaambiwa nikamchukue nirudi naye nyumbani. Kwenda kumchukua ilikuwa rahisi. Kumrudisha imekuwa ngumu sana.

Mambo yalipoharibika Sodoma Lutu aliondoka na familia yake lakini mkewe akataka kurudi hivyo akageuka nyuma na kugeuka kuwa jiwe la chumvi.

Kipigo kwenye ulingo wa ndondi kikikupeleka chini na ukachelewa kusimama hutaweza tena kurejea ulingoni uendelee na mapigano. Hata mpiganishi akikuhesabia mpaka kumi.

Kuna kitu kwenye saikolojia kinaitwa confidence. Wana usalama wanalifundishwa sana. Kumwangalia mtu usoni machoni bila kupepesa, akiangusha tu macho chini hawezi kurudi kukuangalia tena!

Mashindano hayakimbiwi. Ukiyakimbia tambua umekubali kutema bungo

Mtunzi mahiri JAMES HADLEY CHASE ana riwaya yake moja inaitwa THE GUILTY ARE AFRAID! yaani wenye hatia wana hofu na hukimbia hata wasipokimbizwa.

Hatia humfanya mtu akimbie hata kivuli chake mwenyewe!

Ni sawa tu na, kunguru mwoga ambaye hukimbiza bawa lake. Maana hajiamini amejawa hofu na kujihisi mwenye hatia

Kwenda ni rahisi kuliko kurudi!!!
 
Trump alipigwa KWENYE uchaguzi akakubali hakufanya fujo akugoma, akaenda kujipanga upya na akarudi na akshinda kwa kishindo. Nilicho jifunza ukiona ugumu usilazimishe nenda kajipange rejea TENA KWENYE MAPAMBANO ukiona pumzi imekata sepa utaumia ukilazimisha, we nenda kajipange RUDI upya MPAKA KIFO kikuzuie rasmi. Bahati haiji mara mbili no ushapitwa na wakati huo msemo dunia IKO spidi mambo yanabadilika zamani stendi ILIKUA ubungo SIKU HIZI HAIPO TENA IKO mbezi.


Bro Alex on da beats
 
Trump alipigwa KWENYE uchaguzi akakubali hakufanya fujo akugoma, akaenda kujipanga upya na akarudi na akshinda kwa kishindo. Nilicho jifunza ukiona ugumu usilazimishe nenda kajipange rejea TENA KWENYE MAPAMBANO ukiona pumzi imekata sepa utaumia ukilazimisha, we nenda kajipange RUDI upya MPAKA KIFO kikuzuie rasmi. Bahati haiji mara mbili no ushapitwa na wakati huo msemo dunia IKO spidi mambo yanabadilika zamani stendi ILIKUA ubungo SIKU HIZI HAIPO TENA IKO mbezi.


Bro Alex on da beats
Kwenye sanaa ya mapigano ya ndondi kuna terminology wanazitumia..
Kuna pigo la ngumi linaitwa upper cut hilo hupiga chini ya kidevu.. Ukiotewa ukatandikwa nalo ukaenda chini kusimama ni majaliwa... Utakuwa umepigwa kwa KO na si TKO

Halafu kuna sucker punch.. Hili huwa ni pigo la kuotea lililojaa woga lakini kali sana.. Mpigaji anakuwa keshapokea kichapo hasa. Sasa hujiandaa na sucker punch akifanikiwa ame win akikosa ndio basi tena!
 
Lakini huwa kuna muda wa mapumziko ukijipanga ukabuni mbinu nzuri unatoboa. Kinacho tuangusha sisi huwa nikuishi kwa kukalili misemo, Mwigulu alipigwa chini akajipanga akabuni mbinu ANAYO ijua YEYE aka Rudi KWENYE ramani. Kujua muda SAHIHI wa kufanya kipi na kipi USIFANYE ni ushindi tosha haijalishi umepigwa JE.

Bro Alex on da beats.
 
Waulize watalaka na watalikiwa watakuambia... Kwenda kwenye ndoa ni rahisi kuliko kurudi kwenye ndoa baada ya kuondoka kwenye ndoa.

Kijana wangu alipewa suspension shuleni nikaambiwa nikamchukue nirudi naye nyumbani.. Kwenda kumchukua ilikuwa rahisi.. Kumrudisha imekuwa ngumu sana.

Mambo yalipoharibika Sodoma Lutu aliondoka na familia yake lakini mkewe akataka kurudi hivyo akageuka nyuma na kugeuka kuwa jiwe la chumvi.

Kipigo kwenye ulingo wa ndondi kikikupeleka chini na ukachelewa kusimama hutaweza tena kurejea ulingoni uendelee na mapigano.. Hata mpiganishi akikuhesabia mpaka kumi.

Kuna kitu kwenye saikolojia kinaitwa confidence.. Wana usalama wanalifundishwa sana.. Kumwangalia mtu usoni machoni bila kupepesa, akiangusha tu macho chini hawezi kurudi kukuangalia tena..!

Mashindano hayakimbiwi.. Ukiyakimbia tambua umekubali kutema bungo

Mtunzi mahiri JAMES HADLEY CHASE ana riwaya yake moja inaitwa THE GUILTY ARE AFRAID! yaani wenye hatia wana hofu na hukimbia hata wasipokimbizwa.

Hatia humfanya mtu akimbie hata kivuli chake mwenyewe!

Ni sawa tu na,kunguru mwoga ambaye hukimbiza bawa lake.. Maana hajiamini amejawa hofu na kujihisi mwenye hatia

Kwenda ni rahisi kuliko kurudi..!!!
sijaelewa code hata kidogo
 
Back
Top Bottom