Kaka
Mshana Jr kwa heshima kabisa naomba nikukosoe mambo kadhaa kwa faida ya wote pia.
Kwanza kabisa Mahakama ya Mafisadi ile ni divisheni ya ahakama Kuu, hoja ya kusema.kuwa haipo kikatiba sio kweli kwani Mahakama Kuu imeanzishwa na katiba ya Jamhuri.
Ile Mahakama ya mafisadi jina lake ni Mahakama Kuu divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi. Hivyo ile ni Mahakama Kuu na Mahakama Kuu ni moja tu ila ina divisheni na hukaa sehemu tofauti tofauti nchini.
Pili hii divisheni inayosikiliza kesi za ufisadi imeanzishwa na sheria ya bunge chini ya sheria ya makosa ya uhujumu uchumi na magenge ya uhalifu, hivyo hoja ya kuwa haitambuliki na sheria za nchi sio kweli, hii inatambulika kwani imeanzishwa na sheria ya bunge.
Kuna watu wanafikiri Magufuli ndiye aliyeleta makosa ya uhujumu uchumi kitu ambacho sio kweli kabisa, sababu sheria hiyo ipo tangu miaka ya 1980+ na ile ya utakatishaji fedha ipo tangu miaka ya 2000+
Alichokifanya Magu ni kusema majengo ya Shule ya Sheria yatumiwe kama makao ya hii Mahakama, jambo ambalo pia limewakosesha wanafunzi wa uwakili wasaha wa kujifunza kwa vitendo uendeshaji wa kesi katika mazingira rasmi ya kimahakama. Badala yake wanajifunzia madarasani kwa kupanga meza
Jambo ambalo lipo wazi ni kuwa kuna namna hizi sheria zinazohusika na uhujumu uchumi na ufisadi zinaweza kutumika vibaya na pia weledi ukiwa hafifu hatari ndio huwa kubwa zaidi, ni kweli tunahitaji mabadiliko makubwa ya sheria zaidi ya haya yaliyofanywa kwasasa.
Tuna kesi nyingi za Uhujumu uchumi zinazotokana na makosa ya ujangili ambayo yakisomwa vizuri mtu unakuja kugundua.hayo sio makosa ya uhujumu uchumi kwa dhana pana ya uhujumu.
Mfano, Mganga kakutwa serengeti na mkia wa nyati anapewa uhujumu uchumi, kivipi huu ni uhujumu uchumi? au mkazi wa serengeti katafuta kitoweo cha sungura pori kakamatwa kapewa uhujumu uchumi, ni uhujumu uchumi kivipi?. Hawa watu wameishi maisha yao hivyo karne na karne leo hauwezi waita wahujumu. Ni sawa na kusema wamasai wa Ngoro ngoro ni majangili na wahujumu uchumi kwa sababu wapo ndani ya hifadhi (Hii mada pana), hizi sheria kweli zinatakiwa kubadilika sana na Bunge lifahamu hasa dhamira ni nini zinapotungwa hizi sheria.
Mimi ni hayo tu.