Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,791
Hii mahakama iliasisiwa na Mwendazake Pombe Magufuli John alipokuwa Rais kwa kulazimisha wa awamu ya tano.
Haipo kikatiba
Haipo kisheria
Haipo kwenye ilani ya chama. Iliasisiwa kwa maono kimo cha mbilikimo! Kwa kutumia nguvu kubwa na maarifa kidogo.
Sikumbuki kuona kesi zilizohukumiwa na hii Mahakama (nakubali kukosolewa). Nyingi ushahidi umekuwa ni changamoto hivyo kufanya zisuesue. Nyingi ni za kisiasa na kukomoana. Nyingine zilikuwa za visasi na kubambikiwa.
Matendo ya Mungu si ya binadamu. Pombe Magufuli hatunaye tena na zimeshatimia siku 100 na ushee toka atwaliwe kutoka maisha haya. Mama Samia Rais wa sasa ameonesha nia njema ya kutofautiana na mtangulizi wake. Walioitwa mafisadi na kupewa kesi kubwa kubwa za uhujumu uchumi wanafutiwa mashtaka na kuachiwa huru.
Waliokuwa wamehukumiwa kisiasa na kulipishwa faini za dhuluma wanarudishiwa pesa zao! Huu ni mwanzo wenye nia njema..Kazi bado ni pevu na kuna mengi ya kuweka sawa. Na mojawapo ya hayo ni hii mahakama ya mafisadi! Tunasubiri kuona hatima yake na hasa ikivunjiliwa mbali na kuokoa kodi zetu
Mama unapitapita huku. Naamini utasoma na hili.
Haipo kikatiba
Haipo kisheria
Haipo kwenye ilani ya chama. Iliasisiwa kwa maono kimo cha mbilikimo! Kwa kutumia nguvu kubwa na maarifa kidogo.
Sikumbuki kuona kesi zilizohukumiwa na hii Mahakama (nakubali kukosolewa). Nyingi ushahidi umekuwa ni changamoto hivyo kufanya zisuesue. Nyingi ni za kisiasa na kukomoana. Nyingine zilikuwa za visasi na kubambikiwa.
Matendo ya Mungu si ya binadamu. Pombe Magufuli hatunaye tena na zimeshatimia siku 100 na ushee toka atwaliwe kutoka maisha haya. Mama Samia Rais wa sasa ameonesha nia njema ya kutofautiana na mtangulizi wake. Walioitwa mafisadi na kupewa kesi kubwa kubwa za uhujumu uchumi wanafutiwa mashtaka na kuachiwa huru.
Waliokuwa wamehukumiwa kisiasa na kulipishwa faini za dhuluma wanarudishiwa pesa zao! Huu ni mwanzo wenye nia njema..Kazi bado ni pevu na kuna mengi ya kuweka sawa. Na mojawapo ya hayo ni hii mahakama ya mafisadi! Tunasubiri kuona hatima yake na hasa ikivunjiliwa mbali na kuokoa kodi zetu
Mama unapitapita huku. Naamini utasoma na hili.