Ni nini hatma ya Mahakama ya Mafisadi?

Ni nini hatma ya Mahakama ya Mafisadi?

Haha. Kwamba mafisadi wajiachie? Ila nyiee watanzania hamutakaa mukapiga hatua Moja mbele maana mnapenda kurudi rudi nyuma Sana.
Kuna shida kwenye heading na nimesharipoti .. Ilipaswa kuwa NININI HATIMA YA MAHAKAMA YA MAFISADI
cc: Moderator
 
Hii mahakama iliasisiwa na Mwendazake Pombe Magufuli John alipokuwa rais kwa kulazimisha wa awamu ya tano..!
Haipo kikatiba
Haipo kisheria
Haipo kwenye ilani ya chama...! Iliasisiwa kwa maono kimo cha mbilikimo! Kwa kutumia nguvu kubwa na maarifa kidogo...!

Sikumbuki kuona kesi zilizohukumiwa na hii mahakama..(nakubali kukosolewa).. Nyingi ushahidi umekuwa ni changamoto hivyo kufanya zisuesue.. ! Nyingi ni za kisiasa na kukomoana..!!! Nyingine zilikuwa za visasi na kubambikiwa...!!!

Matendo ya Mungu si ya binadamu... Pombe Magufuli hatunaye tena ... Na zimeshatimia siku 100 na ushee toka atwaliwe kutoka maisha haya...!!!...Mama samia rais wa sasa ameonesha nia njema ya kutofautiana na mtangulizi wake... Walioitwa mafisadi na kupewa kesi kubwa kubwa za uhujumu uchumi wanafutiwa mashtaka na kuachiwa huru...!
Waliokuwa wamehukumiwa kisiasa na kulipishwa faini za dhuluma wanarudishiwa pesa zao! Huu ni mwanzo wenye nia njema..Kazi bado ni pevu na kuna mengi ya kuweka sawa... Na mojawapo ya hayo ni hii mahakama ya mafisadi! Tunasubiri kuona hatima yake na hasa ikivunjiliwa mbali na kuokoa kodi zetu!
Mama unapitapita huku.. Naamini utasoma na hili!!!!!
Ile mahakama ilianzishwa kwa sababu ya kumkomoa mtu mmoja tu, ENL.. Sasa baada ya kuhamia kwao, haina wa kumshiki kule
 
I wish angekuwepo ili nimuulize kuhusu matokeo ya ile tume iliyo ongozwa na "Mjamaa na Comrade" Dr. Bashiru Ally akishirikiana na Wajumbe wake akina Albert Chalamila, kuchunguza mali za chama!

Sijawahi kusikia kuna Kigogo yoyote ndani ya chama akifikishwa kwenye hiyo mahakama kwa ufisadi, ubadhirifu, matumizi mabaya ya madaraka, nk.
Mpuuzi kweli yule jamaa.Ukuu wa mkoa wa Comical Albert Chalamila ulitokana na hiyo kamati.Akaanza kuwatukana wazee wake kuwa ni walevi.😝😝😝😝😝
 
usisahau uwanja wa ndege Chato una harufu kali ya ufisadi + ununuzi wa ndege bila kufuata kanuni!
Sasa hapo umejibu nini mkuu, ufisadi wa EPA na ESCROW huwezi linganisha na ununuzi wa ndege au ujenzi wa kiwanja cha ndege Chato vitu ambavyo ni mali ya umma.

Umeshindwa kujibu swali la msingi je ni kweli hapakuwa na mafisadi hapa nchini mfano , na hao waliokamatwa awamu ya tano Kama akina Seth wote walionewa?
 
Sa
Katika kampeni ya Urais Magufuli akiwa na Samia walituahidi watanzania kuwa wataanzisha mahakama ya mafisadi.
Ahadi ya Wagombea Urais ni swala la kiilani vile vile.
Samia alikua anapelekeshwa tu,alipojaribu kushauri alitukanwa kama mtoto na kuamua kurudi kwao Znz huku akilia.
 
Hii mahakama iliasisiwa na Mwendazake Pombe Magufuli John alipokuwa rais kwa kulazimisha wa awamu ya tano..!
Haipo kikatiba
Haipo kisheria
Haipo kwenye ilani ya chama...! Iliasisiwa kwa maono kimo cha mbilikimo! Kwa kutumia nguvu kubwa na maarifa kidogo...!

Sikumbuki kuona kesi zilizohukumiwa na hii mahakama..(nakubali kukosolewa).. Nyingi ushahidi umekuwa ni changamoto hivyo kufanya zisuesue.. ! Nyingi ni za kisiasa na kukomoana..!!! Nyingine zilikuwa za visasi na kubambikiwa...!!!

Matendo ya Mungu si ya binadamu... Pombe Magufuli hatunaye tena ... Na zimeshatimia siku 100 na ushee toka atwaliwe kutoka maisha haya...!!!...Mama samia rais wa sasa ameonesha nia njema ya kutofautiana na mtangulizi wake... Walioitwa mafisadi na kupewa kesi kubwa kubwa za uhujumu uchumi wanafutiwa mashtaka na kuachiwa huru...!
Waliokuwa wamehukumiwa kisiasa na kulipishwa faini za dhuluma wanarudishiwa pesa zao! Huu ni mwanzo wenye nia njema..Kazi bado ni pevu na kuna mengi ya kuweka sawa... Na mojawapo ya hayo ni hii mahakama ya mafisadi! Tunasubiri kuona hatima yake na hasa ikivunjiliwa mbali na kuokoa kodi zetu!
Mama unapitapita huku.. Naamini utasoma na hili!!!!!
Maono kimo ya mbilikimo😅😅
 
Sasa hapo umejibu nini mkuu, ufisadi wa EPA na ESCROW huwezi linganisha na ununuzi wa ndege au ujenzi wa kiwanja cha ndege Chato vitu ambavyo ni mali ya umma.

Umeshindwa kujibu swali la msingi je ni kweli hapakuwa na mafisadi hapa nchini mfano , na hao waliokamatwa awamu ya tano Kama akina Seth wote walionewa?
sumu ni sumu tu ili mradi inaua!
hakuna ufisadi mkubwa na mdogo kama kiwanja kilijegwa na ndege zili nunuliwa bila kufuta taratibu hakuna la zaidi apo zaidi ya ufisadi!
 
Eee..!.Mungu Baba Mwenyezi twakuomba uliepushe taifa letu lisije tena likapata watawala dhalimu kama jiwe milele na milele sio leo,kesho na hata vizazi vyetu vijavyo.Nafunga katika Jina la YESU jina kuu kuliko majina yote.Nikiomba na kuamini hakika hakuna kiongozi dhalimu tena ataketokea katika taifa hili katika Jina la YESU Kristo ulie hai.! Nateketeza kwa moto ulao ! roho zote chafu za viongozi kama Sabaya bashite zisiinuke tena katika taifa hili milele na milele.Tukiomba na kuamini.Na KILA mmoja na aseme.Amee...ni !
 
Back
Top Bottom