Ni nani yuko nyuma ya huu ujinga!?

Ni nani yuko nyuma ya huu ujinga!?

Shirika la Haki za binadamu Duniani la Amnesty International imeikana barua iliyodaiwa kuwa yao iliyokwenda kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), iliyokuwa ikilaani na kukemea kuhusu baadhi ya wanachama wao walioingia nchini Kenya, kujitambulisha kama wakimbizi wa kisiasa na baadae kurejea Tanzania bila ya kutoa taarifa na kulisababishia hasara shirika hilo kutokana na malipo waliyokuwa wakilipwa wahusika.

Shirika hilo limekanusha kuhusika na barua hiyo kupitia mtandao wake wa ‘X’ na kueleza kuwa barua hiyo ni bandia ‘fake’ na kuutaka umma kutohadaika kwa kuwa imelenga kuchafua taswira ya viongozi wa Chadema.

Barua hiyo iliyotengenezwa kwa lengo la kuonekana kuwa imesainiwa na Tigere Chagutah, ilidai kuwa Brenda Rupia, Gervas Lyenda, Zacharia Obad na Lucas Ngoto walifanya tukio hilo baada ya kudai kuwa hawapo salama nchini Tanzania na kisha kupewa hifadhi na kuanza kulipwa Shilingi 1,800,000 kwa kila mwezi.

Barua hiyo ya Amnesty International imesambaa mitandaoni na baadhi ya watu, akiwemo mfuasi wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Yericko Nyerere ambaye amekuwa akikishambulia Chadema na viongozi wake.

Ofisa mmoja wa Amnesty ameiambia MwanaHALISI kuwa jambo hilo halina ukweli na siasa ya kukichafua Chadema “Sio kweli na hiyo barua sio yetu na kwamba tayari tumeshakanusha suala hilo” .

Kama ingekuwa barua yetu sisi tunajua itifaki za kisiasa tungemuandikia katibu mkuu wa chama na sio kumuandikia John Pambalu ambaye ni mkurugenzi wa mafunzo “

Basi hawa watu wangekuwa wanaakili angalau kidogo wangemuandikia barua mkurugenzi wa mambo ya nje tungesema wamejaribu lakini kwa suala hili linawahusu viongozi wa Chadema limekigusa chama hicho moja kwa moja wangemuandikia katibu mkuu” alisema ofisa huyo.View attachment 3539386
Habib Mchange ndio anaepanga maujinga yote haya. Ndie ia anaepanga yale maandamano ya Wakatoliki wa kuchovya. Hayabypte yapo wazi kwenye social media. Anzia youtube umsikilize, ndio mpangaji wa ujinga wote huu
 
Shirika la Haki za binadamu Duniani la Amnesty International imeikana barua iliyodaiwa kuwa yao iliyokwenda kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), iliyokuwa ikilaani na kukemea kuhusu baadhi ya wanachama wao walioingia nchini Kenya, kujitambulisha kama wakimbizi wa kisiasa na baadae kurejea Tanzania bila ya kutoa taarifa na kulisababishia hasara shirika hilo kutokana na malipo waliyokuwa wakilipwa wahusika.

Shirika hilo limekanusha kuhusika na barua hiyo kupitia mtandao wake wa ‘X’ na kueleza kuwa barua hiyo ni bandia ‘fake’ na kuutaka umma kutohadaika kwa kuwa imelenga kuchafua taswira ya viongozi wa Chadema.

Barua hiyo iliyotengenezwa kwa lengo la kuonekana kuwa imesainiwa na Tigere Chagutah, ilidai kuwa Brenda Rupia, Gervas Lyenda, Zacharia Obad na Lucas Ngoto walifanya tukio hilo baada ya kudai kuwa hawapo salama nchini Tanzania na kisha kupewa hifadhi na kuanza kulipwa Shilingi 1,800,000 kwa kila mwezi.

Barua hiyo ya Amnesty International imesambaa mitandaoni na baadhi ya watu, akiwemo mfuasi wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Yericko Nyerere ambaye amekuwa akikishambulia Chadema na viongozi wake.

Ofisa mmoja wa Amnesty ameiambia MwanaHALISI kuwa jambo hilo halina ukweli na siasa ya kukichafua Chadema “Sio kweli na hiyo barua sio yetu na kwamba tayari tumeshakanusha suala hilo” .

Kama ingekuwa barua yetu sisi tunajua itifaki za kisiasa tungemuandikia katibu mkuu wa chama na sio kumuandikia John Pambalu ambaye ni mkurugenzi wa mafunzo “

Basi hawa watu wangekuwa wanaakili angalau kidogo wangemuandikia barua mkurugenzi wa mambo ya nje tungesema wamejaribu lakini kwa suala hili linawahusu viongozi wa Chadema limekigusa chama hicho moja kwa moja wangemuandikia katibu mkuu” alisema ofisa huyo.View attachment 3539386
Bila yaka ni wale wamiliki wa wakatoliki wa kuchovya wa Yombo kama sii Makangarawe!
 
Mbona kalipokuwa chadema kakiandika vijitabu vyake vya "ujasusi" mlikasifia sana?

Cc: Mimi Wewe Yule
Matipo karibu tuendelee na mjadala. Kwa nini umetumia neno "mlikasifia" kwani mshamalizana naye mshaona hana faida tena kwenu?

Unataka kusema ili project ndiyo imeshakufa au mnasubiri muilete kivingine? Maana hata wale wabunge wawili mliowapa kimagumashi watapingwa mahakamani siyo muda.
 
Hii nchi kuna vichaa tu ndo wanaweza kuwaelewa hao viongozi haramu yaan ukiangalia wale jamaa wanaongelea utekaji unafanywa na chadema na wanatamba kabisa fb huko ila tcra wala hawana mda na polisi wala hawana shida nao ila wajitokeze watu waiseme ccm km wale jamaa chap mtasikia wamekufa ama wamepotea hawajulikani walipo.. Njoo tena hawa wakatoliki wa buza kwa mparange hujakaa vizuri hiyo barua feki bado tu hujui ni kina nani wako nyuma ...!???
Na bila hata ya aibu, au hata kuheshimu tamaduni zetu tu; hao hao wanahimiza walioguswa na mkasa wa watoto wao kuuliwa waende kujisalimisha kwa wauaji hao hao kwa kutoa ushuhuda mbele ta tume feki ili wapewe chochote kwa kuwapoteza wapendwa wao!

Nchi imekuwa ya kijambazi sana hii.
 
Back
Top Bottom