Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,869
- 828,386
Shirika la Haki za binadamu Duniani la Amnesty International imeikana barua iliyodaiwa kuwa yao iliyokwenda kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), iliyokuwa ikilaani na kukemea kuhusu baadhi ya wanachama wao walioingia nchini Kenya, kujitambulisha kama wakimbizi wa kisiasa na baadae kurejea Tanzania bila ya kutoa taarifa na kulisababishia hasara shirika hilo kutokana na malipo waliyokuwa wakilipwa wahusika.
Shirika hilo limekanusha kuhusika na barua hiyo kupitia mtandao wake wa ‘X’ na kueleza kuwa barua hiyo ni bandia ‘fake’ na kuutaka umma kutohadaika kwa kuwa imelenga kuchafua taswira ya viongozi wa Chadema.
Barua hiyo iliyotengenezwa kwa lengo la kuonekana kuwa imesainiwa na Tigere Chagutah, ilidai kuwa Brenda Rupia, Gervas Lyenda, Zacharia Obad na Lucas Ngoto walifanya tukio hilo baada ya kudai kuwa hawapo salama nchini Tanzania na kisha kupewa hifadhi na kuanza kulipwa Shilingi 1,800,000 kwa kila mwezi.
Barua hiyo ya Amnesty International imesambaa mitandaoni na baadhi ya watu, akiwemo mfuasi wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Yericko Nyerere ambaye amekuwa akikishambulia Chadema na viongozi wake.
Ofisa mmoja wa Amnesty ameiambia MwanaHALISI kuwa jambo hilo halina ukweli na siasa ya kukichafua Chadema “Sio kweli na hiyo barua sio yetu na kwamba tayari tumeshakanusha suala hilo” .
Kama ingekuwa barua yetu sisi tunajua itifaki za kisiasa tungemuandikia katibu mkuu wa chama na sio kumuandikia John Pambalu ambaye ni mkurugenzi wa mafunzo “
Basi hawa watu wangekuwa wanaakili angalau kidogo wangemuandikia barua mkurugenzi wa mambo ya nje tungesema wamejaribu lakini kwa suala hili linawahusu viongozi wa Chadema limekigusa chama hicho moja kwa moja wangemuandikia katibu mkuu” alisema ofisa huyo.
Shirika hilo limekanusha kuhusika na barua hiyo kupitia mtandao wake wa ‘X’ na kueleza kuwa barua hiyo ni bandia ‘fake’ na kuutaka umma kutohadaika kwa kuwa imelenga kuchafua taswira ya viongozi wa Chadema.
Barua hiyo iliyotengenezwa kwa lengo la kuonekana kuwa imesainiwa na Tigere Chagutah, ilidai kuwa Brenda Rupia, Gervas Lyenda, Zacharia Obad na Lucas Ngoto walifanya tukio hilo baada ya kudai kuwa hawapo salama nchini Tanzania na kisha kupewa hifadhi na kuanza kulipwa Shilingi 1,800,000 kwa kila mwezi.
Barua hiyo ya Amnesty International imesambaa mitandaoni na baadhi ya watu, akiwemo mfuasi wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Yericko Nyerere ambaye amekuwa akikishambulia Chadema na viongozi wake.
Ofisa mmoja wa Amnesty ameiambia MwanaHALISI kuwa jambo hilo halina ukweli na siasa ya kukichafua Chadema “Sio kweli na hiyo barua sio yetu na kwamba tayari tumeshakanusha suala hilo” .
Kama ingekuwa barua yetu sisi tunajua itifaki za kisiasa tungemuandikia katibu mkuu wa chama na sio kumuandikia John Pambalu ambaye ni mkurugenzi wa mafunzo “
Basi hawa watu wangekuwa wanaakili angalau kidogo wangemuandikia barua mkurugenzi wa mambo ya nje tungesema wamejaribu lakini kwa suala hili linawahusu viongozi wa Chadema limekigusa chama hicho moja kwa moja wangemuandikia katibu mkuu” alisema ofisa huyo.
